No problem, God shall overcome
naona nijikalie tu kimya.
SERIKALI INAPOCHOMA NYUMBA ZA RAIA WAKE, KUBAKA WAKE KWA MABINTI, KUCHINJA VIJANA KWA WAJAWAZITO LINDI NA MTWARA SHAURI YA MAONI YAO WANANCHI SASA TUKIMBILIE WAPI
Jamani watazameni masiki wenzangu na mimi hawa kosa lao tu ni kule KUDIRIKI KUTOA MAONI YAO na sasa nyumba tu ya udongo unalazimika kuwatoka jumla hivi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Sasa WaTanzania tunatarajia matokeo ya aina gani kwa hicho kitoto hapo pichani anayelazimika kulala kwenye baridi porini kwa kuwa tu CCM na Rais Kikwete wachoma nyumba yao,
Je, tunatarajia kitu gani tukija kukutana na yule binti pale akijiuza Mtaa wa Ohio Dar usiku kwa kuwa tu serikali yake imevuruga kabisa misingi ya pato la familia?
Je, WaTanzania tunalo jibu gani endapo huyo mama hapo juu atakaposhindwa maisha kijijini kwa kuwa tu maoni yao tu kwa mradi wa gesi utakua umemfanya mumewe atolewe roho na Nchimbi na kisha akajichagulia kuja jijiji kujaribu bahati yake katika Umachinga wa Mama Nitilie pembeni mwa barara pale Ilala Boma????????
![]()
25th May 2013 12:25 Woman-May25-2013.jpg
Ni wakati mwafaka kwa NEC-CHADEMA kutuma ujumbe wa walau watu saba (Makamanda Marando, Prof Safari, Chiku Abwao, Mawazo wa Bukoba, Zitto, Ben Saanane, Makamu Mwenyekiti wetu Zanzibar na John Mnyika) kwenda Lindi na Mtwara kutathmini hali ilivyo kwa wananchi wenzetu wa kusini kisha kurejesha ripoti Makao Makuu ili watu tujue tunaamua kuchukua hatua gani juu ya sakata la gesi once and for all.
Udhalilishwaji wa familia mbalimbali huko kusini ikiwemo hii familia tuliojulishwa na mpiga picha wa IPP Media ni ushahidi tosha kwamba tusipochukua hatua hizi za haraka basi kama chama tutakua tumewasaliti mno wenzetu hawa ambao hivi sasa ni WAHANGA WA MAONI juu ya mradi wa gesi ya Kikwete na Wa-China wake.
Swali lenye thamani ya zaidi ya dola milioni moja kwa kila mmoja kwa nafasi yake katika taifa letu ni:
Je pindi unaposikia ya kwamba serikali inayosadikiwa kuwekwa madarakani kwa manufaa ya wapiga kura inapogeuka adui na kuchoma nyumba za raia wake, kubaka wake kwa mabinti, kuchinja vijana kwa wajawazito kwa mizinga ya kijeshi Lindi na Mtwara shauri tu ya kutoa maoni yao, wananchi sasa tukimbilie wapi???????????
Hii nimeitoa IPPMEDIA:
A woman shows her house alleged to be burnt by Field Force police during the operation to calm the situation erupted after anti-gas transportation from Mtwara to Dar es Salaam clashed by riot police on Wednesday at Magomeni in Mtwara region. Situation in Mtwara is calm but remains tense.
View attachment 95077
Akili za kimasaburi hizi.
Wakuu 'FundiMchundo', 'Dingswayo', 'Mtwaraboy' pamoja na 'Gesi-Mtwara'; hebu tusaidieni basi picha ya yule MAMA MJAMZITO anayedaiwa kubakwa kwanza kisha kufiatuliwa rundo la mi-risasi tumboni pale Magomeni-Mtwara juzi - ni muhimu sana picha hii wakuu.
Wananchi wakichoma nyumba, mahakama, magari, ofisi na kuharibu miundombinu mnashangilia tena kuhamasisha juu kuwa waendelee kuchoma. Ila ikisemwa polisi wamechoma mnawaandama polisi na kuwalaani kwa nguvu zote kana kwamba wakati nyumba inachomwa mlikuwa mnashuhudia na kuhakikisha kuwa kweli aliyechoma ni polisi.
Wananchi wakichoma nyumba, mahakama, magari, ofisi na kuharibu miundombinu mnashangilia tena kuhamasisha juu kuwa waendelee kuchoma. Ila ikisemwa polisi wamechoma mnawaandama polisi na kuwalaani kwa nguvu zote kana kwamba wakati nyumba inachomwa mlikuwa mnashuhudia na kuhakikisha kuwa kweli aliyechoma ni polisi.
picha za Mwangosi (1) Kijokisimba kazunguka nayo Dunia nzima (2) kumchafua Jakaya, aliporudi nyumbani Kaingia (3) Rais wa China na akahutubia Dunia kutokea Tanzania na sasa 1 st July Barack Hussein Obama anaingia kwa Jakaya kushuhudia maendeleo yasiyo mithilika!