Hii ni coment ya yangu nimecomment kwenye uzi mwingine kama huu naipaste hapa.
Wengi wenye umri mdogo humu hamuwezi kujuwa lakini nawakikishia hili ni tatizo la ccm kuuza au kupora viwanja vya wazi.
Zamani hakukuwa na uzuraraji wa kiholela nje ya wilaya zenu na tarafa zenu palikuwa panajengwa mabanda (Circus) basi hapo burudani zote hupatikana, ngongoti, korokoro, muziki theater groups and likes ali mradi ni burudani tupu, watoto kwa wakubwa hakika walifurahi sana, na kulikuwa na mzunguko mkubwa wa pesa kwa biashara zote za vinywaji na vitafunwa, yani ilikuwa Disney land fulani.
Kuna kina sisi wengine tuliokuwa wapenzi wa sinema tulikwenda kuangalia movie Avalon cinema, Empire, New chocks, Odeon, Cameo, Drive in and so on,
Kwa mfano viwanja vya mnazi mmoja, buguruni chama, Temeke kata ya 14, kiwalani kata ya kipawa, mwenge, hizi sehemu kwa uchache zilikuwa na circus zao kama Disney land fulani hivi, lakini kwakuwa kuna kundi la walafi ccm wakateka nyala haya maeneo ya wazi either kujimilikisha au kuyauza na hatimaye huu utamaduni ukayeyuka jumla jijini Dar.
Ni hatari sana siku za sikukuu kundi moja kubwa lote kuelekea out sehemu moja kwa kukosekana public area za community kukutana.
Kwa tuliofuta matongotongo na kutembea nchi zenye viongozi wenye akili na maono kila kata ina community center hall na park tena saa nyingine park zaidi ya moja, wakati Dar hiyo paki iliyobaki ya mnazi mmoja na bado inafungwa, very fun aisee.
Inshort tatizo siyo waislamu, tatizo ni ccm.
Halafu kingine zamani siku za sikukuu ndio zilikuwa ndugu na familia kutembeleana na ndugu kujuwana lakini umaskini umeondowa upendo na sasa tunaishi kama manyani tu, hata mpenzi wako anakugeuza wewe ndio source of income na siyo tulizo la moyo tena