Nyoka Koboko au Black Mamba

Nyoka Koboko au Black Mamba

Watu wengi waliokutana nae wakatulia wakasali sala zao mwisho wameokoka hakuwagusa, ila ukijifanya we ni mwamba, unakimbia huku unapiga makelele...ni anakukimbiza huku anakugonga double double mpaka unageuka rangi ya chungwa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
😀😀😀😀


Eti anakugonga double double hadi unageuka rangi ya chungwa.
 
1.kwa hiyo kama anamgonga mtu huwa kuna dawa yoyote
2.kama ikigundulika sehemu flani kuna koboko huwa mnachukua hatua gani??
1.Dawa iko hospitalini, na kijijini kwetu kuna mbibi alikuwa ana mitishamba wakikuwahisha utapona kabisa ila iwe within 20 mints..

2. Hakuna kupita maeneo haya

NB

Mpaka haya yakukute na mkutane nae ni very rare

Ila watu sio zaidi ya kumi naowafahamu waliuliwa na huyu nyoka na tahadhari walipewa, especially wachunga ng'ombe na mbuzi



Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Mi nakwambia ukweli....kijijini kwetu koboko wamejaa ka mchanga

Nikianza kuhesabu watu aliowaua sina hata idadi

Ishu iko hivi akikuona we hujamuona huwa hana time kabisa ( na ni lazima akuone kabla hujamuona)...balaa ni pale mtakapogonganisha macho, yaan akajua kuwa umemuona, hakuachi kwa sababu utaenda kutangaza huko kwa watu kuwa umeona nyoka mje wengi mumuue so anakuwahi... ( Ndo maana kijijini kwetu wanamhusisha na ushirikina kwa hizo akili zake

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
mtoto wa masaki wewe kijijini umekaa miaka ipi
 
Video kibao za huyo nyoka zipo youtube unaweza kuangalia na kujifunza maisha yake yalivyo hadi aina ya sumu aliyonayo wameelezea
 
Dawa nyingine chukua kundi la kondoo wengi waswage uwapitishe alipo atagonga mmoja tu na kuishiwa sumu na mnamuua Sasa bila shida,ila ukubali kupeteza kondoo mmoja.
Labda humjui huyu nyoka ,,huyu ni nyoka anayengata zaidi ya mara moja na anauwezo wa kuua watu zaidi ya kumi na tano,,Ikiwa Tembo mkubwa vile akingwata anakufa ndani ya saa moja vipi binadam....
 
Koboko au Black Mambo kisayansi Dendroaspis polyleps ni nyoka mwoga sana ila mkorofi hutumia speed yake Kali kukimbia pale anapohisi hatari na akikutana na Nyegere a.k.a Honey buger ni mchumba tu
 
Back
Top Bottom