Ndugu wanabodi,
Napenda kutoa zangu shukrani kwa jitihada zenu za michango ya mawazo kwa lengo la kuijenga na kuitetea Tanzania.
Kuna kitu kinanikera na naomba kukitoa wazi hapa JF.
Vita ya kupambana na mafisadi katika nchi yetu sioni kama imeanza pamoja na kelele zote za wananchi kwa serikali husika. Serikali imeanza kuwakamata watu na kuwapeleka mahakamani tokana na EPA pamoja na makosa mengine.
Lakini kwa upande wangu naona kwamba wanaokamatwa na kufikishwa mahakamani pamoja na kwamba kwa njia moja ama nyingine walihusika katika kulileta hasara Taifa bado wahusika wakubwa hawajaguswa.
Ningeomba serikali isione haya kuwaonea haya wahusika wakubwa kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Mramba na Yona walikuwa mawaziri chini ya Mkapa, bila shaka walichofanya kilipata baraka za Mkapa, sasa kwanini Mkapa hakamatwi?.
Mkapa ndiye chanzo cha wizi wote na matatizo yote yanayojitokeza sasa, kwanini tuone haya kumwonea haya mtu kama huyo?. Naelewa kwamba Mkapa kama Raisi mstaafu anakinga ya kupelekwa mahakamani, lakini kinga hiyo inakubalika katika makosa aliyoyafanya kama Raisi na si katika makosa aliyoyafanya kama Benjamini William Mkapa.
Mkapa alikula kiapo cha kuilinda katiba ya nchi, kuilinda nchi, wananchi na mali za nchi kwa akili yake yote, moyo wake wote na nguvu zake zote. Kwa kuitumia ikulu kwa kujinufaisha yeye na genge lake katika kuiba mali za nchi na wananchi tayari amekiuka katiba hivyo anapaswa kufikishwa mahakamani.
Hii kamatakamata ya vijifisadi inayoendelea haileti maana kama majifisadi yenyewe hayakamatwi hivyo ni bora kuwaachia wote huru. Ni kichekesho kuwakamata Mramba na Yona kumwacha Mkapa. HAPA NI SAWA NA KULIPIGA JOKA MKIANI KUMBE JOKA LINATAKIWA KUPIGWA KICHWANI.
Napenda kutoa zangu shukrani kwa jitihada zenu za michango ya mawazo kwa lengo la kuijenga na kuitetea Tanzania.
Kuna kitu kinanikera na naomba kukitoa wazi hapa JF.
Vita ya kupambana na mafisadi katika nchi yetu sioni kama imeanza pamoja na kelele zote za wananchi kwa serikali husika. Serikali imeanza kuwakamata watu na kuwapeleka mahakamani tokana na EPA pamoja na makosa mengine.
Lakini kwa upande wangu naona kwamba wanaokamatwa na kufikishwa mahakamani pamoja na kwamba kwa njia moja ama nyingine walihusika katika kulileta hasara Taifa bado wahusika wakubwa hawajaguswa.
Ningeomba serikali isione haya kuwaonea haya wahusika wakubwa kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Mramba na Yona walikuwa mawaziri chini ya Mkapa, bila shaka walichofanya kilipata baraka za Mkapa, sasa kwanini Mkapa hakamatwi?.
Mkapa ndiye chanzo cha wizi wote na matatizo yote yanayojitokeza sasa, kwanini tuone haya kumwonea haya mtu kama huyo?. Naelewa kwamba Mkapa kama Raisi mstaafu anakinga ya kupelekwa mahakamani, lakini kinga hiyo inakubalika katika makosa aliyoyafanya kama Raisi na si katika makosa aliyoyafanya kama Benjamini William Mkapa.
Mkapa alikula kiapo cha kuilinda katiba ya nchi, kuilinda nchi, wananchi na mali za nchi kwa akili yake yote, moyo wake wote na nguvu zake zote. Kwa kuitumia ikulu kwa kujinufaisha yeye na genge lake katika kuiba mali za nchi na wananchi tayari amekiuka katiba hivyo anapaswa kufikishwa mahakamani.
Hii kamatakamata ya vijifisadi inayoendelea haileti maana kama majifisadi yenyewe hayakamatwi hivyo ni bora kuwaachia wote huru. Ni kichekesho kuwakamata Mramba na Yona kumwacha Mkapa. HAPA NI SAWA NA KULIPIGA JOKA MKIANI KUMBE JOKA LINATAKIWA KUPIGWA KICHWANI.