wakuu
jana nilifanikiwa kuvushwa na demu wangu ambaye hapo awali alizoea kuja na kulala kwangu, migegedo yote huwa nafanyia kwangu
huyu mwanamke ananyodo na minato hatariii, yaani akija gheto anajifanya mjuvi wa kila kitu na aishiwi kunikosoa juu ya mambo ya usafi na jinsi ya kupanga vitu vya gheto
basi wikiend hii ndipo namimi nikakomaa kwamba lazima nikapumzkie kwake na ikiwezekana nilale huko hadi asubuhi
nilifanikiwa kulala huko, yaliyonikuta ni hatari tupu full tafrani na kunguni, yaaani kitanda kinakunguni kama majini wanyonya damu!
usiku kucha hakuna kulala, maana ukitulia tu umeng'atwa
nimekaa na kumtafakari leo siku nzima, inakuaje mademu mnajifanya wajuvi kwenye mageto yetu wanaume ilhali ya kwenu yanawashinda?
nimemwambia sitakubali na siwezi kuishi na mtu mchafu, maana kunguni ndio makazi yao hayo