Habari zenu wana jamvi,natumaini mko salama salimini kwa kudra za muumba wetu.
kuna baadhi ya wanaume mishipa ya aibu ilishakatika kabisa ikabakia kwenye dushelele zao tu,kuna bi shostito mmoja kaingizwa mkenge na mwanaume mchana kweupeeee wakati alikuwa akijitapa yeye ni mtoto wa mjini hakuna mwanaume anayeweza kumtapeli loh hebu tupate habari kamili.
Binti kapata mume wa mtu,kama mjuavyo wakishikwa wanashikamana hela ya kodi,mafuta,saloon,shopping n.k si haba kutolewa,kasheshe ikaja kama ifuatavyo ktk marafiki zake shostito kuna mmoja alikuwa anamfahamu yule baba kwa sababu walikuwa wakiishi mtaa mmoja, kumbe yule baba kapanga hana nyumba wala nini maisha yake ya kawaida sana lakini kamdanganya yule bi dada anaishi kwake kampeleka kumwonyesha nyumba ya watu mtaa mwingine kabisa.
bi dada bila hiyana akamuamini ukizingatia anapiga simu za kuzuga kuulizia mizigo yake bandarini n.k kubwa kuliko kamwambia bi shost anamtafutia nyumba ya kumpangishia ili asipate tabu hehehehehehe hapo ndo kasheshe ilipoanzia,dada kapelekwa kuonyeshwa nyumba,alivyo mbea kawachukua mashost wake kuwapeleka kupaona na kuwalingishia,yule best anayemjua yule bwana akatulia zake aone mwisho wa ngoma utakavyokuwa.
La haula ikaandikwa cheque sijui iliokotwa wapi, eti ndo ikipokelewa benki wampatie pesa aje kumlipia bi dada kodi yote,mmmmh katafuta na mkataba wa kughushi kaupeleka stationary wautype kumbe yule dada wa stationary na yeye anamjua akatype akaprint akampa huku nyuma akabaki anacheka eti mtoto wa kike kaingizwa mjini na mara kibao huwa anapeleka mikataba ya uongo pale ili mwanamke aliye nae ajue kweli kapata bwana kumbe hamna kitu,huwezi amini hadi muda huu ninavyoandika mwanaume kaishia mitini yule bestito kafyata mkia kwa mabest zake kawa mdogo kama piriton wenzake mbavu hawana,matambo yote yameisha dah nyie wanaume baadhi yenu hamfai kabisa