Nyerere's best hotuba.


Okay, fine. But it shouldn't be mandatory as race is in some countries.

I mean, if I don't want to share what my religious beliefs (or lack thereof) are then I shouldn't be forced to.

It's none of anyone's business.
 
Sasa si ndo Nyerere anacho claim kukifanya?
mbona malalamiko yamezidi now?
si yangeisha basi?

Haya malalamiko Boss ni bogus. Hayana foundation yoyote ile katika facts.

Kuna watu wana ajenda zao. Stuka braza kaka....

Some people want to advance their agenda and who knows what's next....it could be a demand for Sharia law in some places.
 
Haya malalamiko Boss ni bogus. Hayana foundation yoyote ile katika facts.

Kuna watu wana ajenda zao. Stuka braza kaka....

Some people want to advance their agenda and who knows what's next....it could be a demand for Sharia law in some places.

Sijasema malalamiko ni valid
wala sipingi kuwa kuna hidden agenda....

Ninachokubaliana na Kiranga ni kitu kimoja tu
kuwa kama Taifa lazima tuwaamini watu kwa ujumla wao
na sio serikali ijfanye Godfather wa kuamua vitu vingine kwa hisia tu...

Watanzania walivyo dini ni cultural thing
majority ya Waislam hata msikitini mpaka mwezi wa Ramadhan...
Wakristo ambao wanaamini waganga kuliko Askofu ni wengi pengine kuliko vice versa
Hii fear haina maana....
Weka data tuone
 

Kama dini ina affect sera za uzazi wa mpango, ni muhimu kwa serikali kujua idadi ya watu na mtawanyiko wa watu kwa mujibu wa dini.

Huja address hilo.

Researchers wako UDSM, wanataka kuangalia correlation ya religious affiliation na reproductive rates all over Tanzania ili ku advise public policy, wanahitaji neutral credible data kama za sensa ili kufanya research vizuri.

Serikali imekataa kuhesabu watu kwa dini kutokana na upuuzi wa wachache.

Inakwamisha ufanisi mzima wa sera ya uzazi wa mpango kwa sababu haijakusanya data kwa kuogopa kivuli chake yenyewe.
 

Mimi kwa mtazamo wangu naona hao wanazi wa dini wanaijaribu tu serikali waone iko ngangari kiasi gani.

Licha hivyo, kama watu wanataka data za serikali basi hilo swali au hayo maswlai ya dini yawe voluntary.

Yasiwe ni ya lazima kujibiwa.

Nyerere made a good point. Makanisa, misikiti, na sijui ma Shri Swaminarayan temples si yana waumini bana? Basi hao viongozi wakusanye tu idadi ya waumini wao na habari yote kwisha.

They don't need to be causing a ferkukkle to the rest of us.
 

nakubaliana na wewe kuwa hii hoja ilishikiliwa sana na watu fulani wakiwa na agenda yao na si kwa maana ya takwimu tu, hivyo kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa majibu yasiyo sahii ili kutaka malengo yao kufikiwa.
 
...NN unachosema ni kweli kabisa kwamba kuna watu wanaweza kabisa kuwa na ajenda zao za siri ili kutumia takwimu za sensa kuanzisha madai mengine. Kwangu mimi madai yoyote yale ambayo yameegemea kwenye udini hayana msingi wowote ule. Madai yoyote yale dhidi ya serikali yasitubague Watanzania kwa kuwa huyu ni Muislamu, Mkristo, Chadema au Magamba.

Ila hii Serikali kama kawaida yake imechemsha sana ilipoamua kuhesabu nyumba za ibada lakini kutowahesabu wale ambao wanaenda kuabudu katika nyumba hizi za ibada. Tuchukulie mathalani katika sensa hiyo tukishajua Tanzania kuna misikiti 500,000 na makanisa 1,000,000 sijui takwimu hizi zinasaidia vipi katika mikakati ya kuleta maendeleo ya nchi.


Wale TBC waliomba samahani kwa kudai takwimu walizitumia zilikuwa na makosa. Hivyo kwa hili basi huu wakati wa sensa ungekuwa ni wakati muafaka kuhakikisha Serikali inapata takwimu sahihi zinazoonyesha wapagani ni wangapi, wakristo ni wangapi n.k. lakini kwa Serikali kukataa kuongeza hicho kipengele cha dini utata huu utaendelea kuwepo kwa miaka mingine 10 au zaidi kutegemea na hiyo sensa nyingine itafanyika lini tena na kama Serikali ya wakati huo itakubali kuweka kipengele hicho cha dini.


Haya malalamiko Boss ni bogus. Hayana foundation yoyote ile katika facts.

Kuna watu wana ajenda zao. Stuka braza kaka....

Some people want to advance their agenda and who knows what's next....it could be a demand for Sharia law in some places.
 
Unajua tatizo lenu hamtaki kutulia kwenye mada na kutoa hoja zenye nguvu ya kujibu mada inyohusika mnaishia kutukana na kukejeli. Toeni sababu za msingi za kuweka kipengele cha dini katika sensa. Mwalimu Nyerere aliuliza idadi ya kidini ni kwa ajili ya nini? Kama wakristo au waislamu wanataka idadi ya waumini wao si waipate kwa taratibu za dini zao? Shida hapa ni nini?

Kipengele cha dini kwenye dodoso ya sensa kinasaidia nini? Nchi hii sio ya kidini tukijua idadi ya waislamu itatusaidia nini? Maana hapa hatuhitaji kugawa Kurani wala kugawa Biblia hapa! Hakuna eneo la waislamu wala wakristo peke yao kwamba maendeleo au raslimali zitagawanywa kidini. Udini unasaidia nini?

Nyerere katika hotuba hii anasema hivyo ni vipengele vilivyowekwa na wakoloni na yeye haoni umuhimu wa kipengele hicho kuendelea. Hapo ana kosa gani? Tuache unafiki, kama kuna jambo lingine limejificha nyuma ya kutaka idadi ya watu kidini lisemwe wazi lisifichwe kwenye sensa. Huu ni uongo. Usikimbilie tu kunitukana maana ndilo unalojua, toa hoja acha mambo ya vijiweni.
 

Dini ni personal lakini wakati mwingine zinatuhusu woote chukulia mfano umehamia mtaa fulani ukakuta kuna Msikiti jirani na una loud speaker na wewe binafsi hutaki kusikia mawaidha ya msikiti huo unafanyaje? unahama? je kama nyumba umenunua?
Si utaangalia sheria za mipango miji zinasemaje?

Sasa ili sheria hizo ziwekwe si inabidi ziwepo data? Mfano kama sheria inasema nyumba ya ibada itakuwa na uhuru fulani kwa
mujibu wa watu wa eneo husika...si lazima ziwepo data?na data si ndo takwimu?

Au misamaha ya kodi ya Taasisi za dini? Ambayo ni moja ya tatu ya bajeti tunajuaje kama haiwi abused?data ziko fake?
 
nakubaliana na wewe kuwa hii hoja ilishikiliwa sana na watu fulani wakiwa na agenda yao na si kwa maana ya takwimu tu, hivyo kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa majibu yasiyo sahii ili kutaka malengo yao kufikiwa.

Kwa msingi huu utajuaje kwamba watu wa Mkoa fulani hawatafanya hivyo hivyo ili ku boost population ya mkoa wao?
 

Soma thread, hujaona watu tumeongelea research, public policy, need to know, denying conspiracy theory?

Au una selective dyslexia?
 

Hayo mambo ya makelele kwenye residential areas ni tatizo la utawala mbovu usiofuata sheria.

Sina shaka kuwa kuna angalau sheria ndogo za miji ambazo zina address mambo ya public nuisance n.k.

Kwenye makazi ya watu kero zipo nyingi tu mojawapo yakiwemo mabaa ambayo yamezagaa kama uyoga.

Nenda Sinza Boss....anzia Migombani, uende pale kwa Afande...upande juu kule karibu na Meeda....halafu hesabu katika hiyo vicinity kuna mabaa mangapi halafu ujiulize, je, hivi haya mabaa yamewekwa hapo kwa kufuata sheria kweli? Nadhani jibu unaweza ukapa mwenyewe bila hata ya kupekua kurasa za vitabu vya sheria za mipango miji.
 

Mimi msingi wa kutaka watu wahesabiwe kwa dini ni ukweli kwamba dini ina influence public policy.

Huu ni ukweli usiopingika.

Kwa mfano, katika nchi yenye meagre resources kama yetu ambayo dini zinajenga mahospitali na mashule sawasawa na serikali, it pays kujua shule za kidini zitajengwa wapi ili kuepuka uneconomic redundancy.

Na katika kujua hili serikali inaweza kuhitaji habari za idadi na mtawanyiko wa watu kwa mujibu wa dini.

Nyerere kasema serikali haijengi misikiti na hivyo haina sababu ya kujua dini za watu.

Wengine tutamjibu dini zinajenga mashule na mahospitali, kwa hiyo serikali na dini kama zinataka kufanya kazi kwa ufanisi hazina budi kushirikiana kupata credible data zinazoonyesha wingi na mtawanyiko wa watu kwa mujibu wa dini.
 

Sasa mbona serikali hiyo hiyo inahesabu makanisa na misikiti?

Tatizo letu hatuna serikali, serikali inaenda kwa mapokeo kama dini. Kitu akisema Nyerere hakipingwi.

Mkapa kakataa kuweka picha yake kwenye noti kwa sababu anajiona mbaya hataki kutisha watu, Kikwete anayemfuatia ambaye hana sababu hiyo naye anaogopa kuweka picha yake kwenye noti, mwishowe noti zinabaki na wanyama tu, mpaka watu wanauliza kwani hii nchi haina rais zaidi ya hawa Nyerere Karume na Mwinyi?

Nyerere kasema mambo ambayo inawezekana yalikuwa sawa siku zake, nchi inabadilika kila siku, kuna haja ya kuyatafakari upya.
 
Reactions: BAK

sasa katika vurugu hiyo
mtu mwingine anaweza sema
Sheria za mipango miji zijali dini za watu

mfano mtaa wenye msikiti isiwepo bar
au kama kanisa limetangulia....kusiwepo disco karibu
sasa ili uweze influence yote haya takwimu first...
 
Wengine tutamjibu dini zinajenga mashule na mahospitali, kwa hiyo serikali na dini kama zinataka kufanya kazi kwa ufanisi hazina budi kushirikiana kupata credible data zinazoonyesha wingi na mtawanyiko wa watu kwa mujibu wa dini.

Basi serikali na hizo dini zishirikiane zijue kila dini ina waumini wangapi.

Mchakato wa kuhesabu waumini ufanywe na dini husika kupitia majumba yake ya ibada n.k.

Siyo watuwekee kwenye mifomu ya sensa.

Kuna wengine hapa tumezaliwa na kulelewa kwenye ukatoliki na mafundisho tukafanya (ingawa si kwa hiari yetu) na sasa tumeshakuwa watu wazima na hatuna dini wala nini.

Waende huko makanisani na misikitini watajua idadi ya wafuasi wa kweli wa dini ni wangapi.
 
Sasa mbona serikali hiyo hiyo inahesabu makanisa na misikiti?

Now, that is one of the most stupidest things I've ever heard.

Unahesabu majumba ya ibada halafu waumini huwahesabu? What sense does that make?

Ni kweli, hatuna serikali sisi.
 


Tayari sasa hivi
misamaha ya kodi ambayo ni almost moja ya tatu ya makusanyo
ni kwa mashirika ya dini...
what if wanawakilisha less than ten percent tu ya Wananchi?
Walipotaka kufutiwa walikuja juu mno hadi serikali ikanywea
but tunajuaje kuwa hiyo misamaha inawagusa hata robo tu ya populations?
data...sensa...
 
Outcome ya hiyo speech ni mh. Benjamin William Mkapa. Labda tujadili, je, Mkapa anafiti kwenye vigezo alivyovitaja mwalimu kwa asilimia ngapi?
In my view, katika swala la udini na ukabili amefit kwa asilimia 99.9 if not 100. Katika kuboresha maisha ya watanzania 65% na kuchukia na kuzuia rushwa 15%.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…