toroka uje mjini
JF-Expert Member
- Mar 29, 2017
- 1,584
- 2,118
Mimi sintomsamehe huyo mzee kwa jinsi alivyo wakandamiza wananchi kwa UHUJUMU UCHUMI na KUTAIFISHA MALI ZAO na NYUMBA ZAO
Yaani ulikua ndani ya utawala kwa muda mrefu Sana tena Kama miaka 22. Tena kipindi chako Chama kilishika hatamu yaani Chama kimoja.
Ulikuwa na madaraka yote na nguvu nyingi za kutenda na kusema lolote na likafanyika
Lkn ona umeondoka na umeacha mkoa wako pamoja na watu wako wakiwa masikini kabisa.
Hakuna uwanja wa ndege wa maana, Hakuna barabara za maana, Hakuna hospital yoyote ya maana, Hakuna huduma ya maji, umeme shida, shule zenyewe zinatosha, yaani nashindwa hata nisemeje.
Tazama mwenzako wa sasa ndani ya miaka Minne tu kijiji chake kilivyo badilika. Nasema kijiji wala sio mkoa
Tayari ana uwanja wa ndege wa kisasa, hotels kubwa kubwa za kufa mtu, mbuga yake ya wanyama tena ya kulazimisha inaendelea kutangazwa kwa nguvu, traffic light za maana hata Kama Hakuna Magari, umeme na maji ya kumwaga, hospital ya rufaa inajengwa, Benki zinafunguliwa kwa fujo duka kubwa LA dawa MSD, shule zinajengwa na Majengo ya kisasa ya kiutawala
Kwa haya yote kweli Nina haja gani ya kukusamehe wewe?
Ulisahau mchezo kwao hutuzwa hadi ukatuacha katika Hali hii dhaifu?
Mungu akurehemu
Mimi sintomsamehe huyo mzee kwa jinsi alivyo wakandamiza wananchi kwa UHUJUMU UCHUMI na KUTAIFISHA MALI ZAO na NYUMBA ZAO
Ndio maana tunamuombea atangazwe mtakatifu maana hakuwa mbinafsi kwa kujipendelea yeye, familia yake, kijiji au mkoa wake, bali alipenda watu wote sawa kiasi cha kusahau kwao. Huyu wa sasa ni mbinafsi, mchoyo, mpenda sifa na visasi kwa watu kiasi cha kudiriki kutoa uhai wa wakosoaji wakeYaani ulikua ndani ya utawala kwa muda mrefu Sana tena Kama miaka 22. Tena kipindi chako Chama kilishika hatamu yaani Chama kimoja.
Ulikuwa na madaraka yote na nguvu nyingi za kutenda na kusema lolote na likafanyika
Lkn ona umeondoka na umeacha mkoa wako pamoja na watu wako wakiwa masikini kabisa.
Hakuna uwanja wa ndege wa maana, Hakuna barabara za maana, Hakuna hospital yoyote ya maana, Hakuna huduma ya maji, umeme shida, shule zenyewe zinatosha, yaani nashindwa hata nisemeje.
Tazama mwenzako wa sasa ndani ya miaka Minne tu kijiji chake kilivyo badilika. Nasema kijiji wala sio mkoa
Tayari ana uwanja wa ndege wa kisasa, hotels kubwa kubwa za kufa mtu, mbuga yake ya wanyama tena ya kulazimisha inaendelea kutangazwa kwa nguvu, traffic light za maana hata Kama Hakuna Magari, umeme na maji ya kumwaga, hospital ya rufaa inajengwa, Benki zinafunguliwa kwa fujo duka kubwa LA dawa MSD, shule zinajengwa na Majengo ya kisasa ya kiutawala
Kwa haya yote kweli Nina haja gani ya kukusamehe wewe?
Ulisahau mchezo kwao hutuzwa hadi ukatuacha katika Hali hii dhaifu?
Mungu akurehemu
Kuna shida gani haya yakifanyika huko Chato? Au ulitaka yafanyike Marangu? Sielewi watanzania wanavyolalamika maendeleo chato, kama ni maendeleo chato nayo ina deserve maendeleo, sioni shida ya huo uwanja, sababu tayari utatumika strategically kama uwanja wa mkoa wa geita pia
Kwa hiyo wa sasa barabara , maji, viwanja vya ndege, shule , miradi na huduma zote za kiuchumi na kijamii hapeleki sehemu zingine za Tanzania?! Je maraisi wengine kwao hawakufanya lolote?! Barabara ya Kwa Mwinyi Dovya ilifuata nini?, Barabara ya Msoga, umeme nk vilifuata nini huko? Lami ya kwanza kuiona mimi ni ya Mwanza Musoma ilifuata nini huko?! Tusiwachimbe viongozi wetu, hakuna aliyemkamilifu na maeneo yao pia yanastahili kupata huduma kama sehemu nyingine za Nchi yetu kabla ,wakati na baada ya viongozi hao kutoka madarakani!Umenisoma vizuri sio kuwa namlaumu Nyerere Bali nilitaka kuonyesha utofauti wa uongozi kwa ajili ya watu na uongozi kwa ajili ya mtu mbinafsi
Hivi anachofanya Magufuli leo kwa Wahujumu Uchumi kina tofauti gani na alichokuwa kifanya Baba wa Taifa?
Acheni unafiki enyi Mapoyoyo na Mabazazi wa CCM...!!!
Mwacheni Baba apumzike kwa amani msije mkazidi kujitafutia Laana bure ambayo tayari ina watafuna!!!
Sijui kikwete na mwinyi na wao kwao walifanya Kama mkulu!
Mkuu kwani ungeamua kukaa kimya ungepata hasara gani?Maana inaonekana unadhani katiba ni kitabu tu.Mkuu tusipokuwa na sheria nzuri na institutions za kuhakikisha hizo sheria zinafuatwa na kuheshimiwa na kila mtu tunajidanganya wenyewe.Hata maandiko matakatifu yanatuambia amelaaniwa mtu yule anaemtegemea mwanadamu.hakuna nchi iliyowahi kumtegemea mti na ikawa na sustainable development, Ya Libya umeshaona,ya Tanzania unayajua na ya Rwanda utayaona just waitNa uhuru ulipatikana kwa katiba ipi.
Tatizo ninyi kizazi cha sasa ni kufikiri kila kitu kinaenda katiba.
Hisia na uhamasishaji ndio msingi wa siasa zote, katiba ni matokeo.
Wakati huo huo watanzania milioni 55 ambao ndo wenye katiba yao wakiwa either wamelala usingizi mzito au wamekufa kabisaMzee Mwinyi ni mojawapo ya Marais waliokuwa na hekima na busara sana(Mzee Ruksa). Mzee wa Msoga aliingia kwenye Urahisi akiwa amebakiza ka-imini kadogo sana kalikobakia kutoka kwa Baba wa Taifa. Baadaye alijichanganya na kuzidiwa kete na Mahafidhina wa CCM na akapoteza mwelekeo kabisa....!!
Lakini bado huwezi kuwalinganisha na huyu bazazi Magufuli ambaye anaitawala Tanzania kama vile ni familia ya nyumbani kwake......Ninashangaa sana Rais aliyeapa kuilinda na kuitetea Katiba ya JMT leo anaikanyaga kwa kisigino kwa kupindisha Sheria ili kukidhi matamanio yake huku akizidi kuwaumiza na kuwatesa Watanzania wenzake kwa vile tu ati wako vyama pinzani...Hii ni akili ya matope ambayo inapashwa isafishwe na itakatishwe kwa moto wa chuma cha pua..!!
Poyoyo ni wewe enzi zake huyo wewe ulikua unanyonya maziwa huku sisi kaka zako tukitembea viatu vya makata mbuga,mara elf ya jiwe kuliko hicho kichuguu,kilichokua kikiwaweka watu kizuizini hovyo tu
Mkuu kwani ungeamua kukaa kimya tungepata hasara gani?Maana inaonekana unadhani katiba ni kitabu tu.Mkuu tusipokuwa na sheria nzuri na institutions za kuhakikisha hizo sheria zinafuatwa na kuheshimiwa na kila mtu tunajidanganya wenyewe.Hata maandiko matakatifu yanatuambia amelaaniwa mtu yule anaemtegemea mwanadamu na ikawa na sustainable development, Ya Libya umeshaona,ya Tanzania unayajua na ya Rwanda utayaona just wait
Msiojua misingi ya kulianzisha Taifa hili mtaweweseka sana.Mkuu kwani ungeamua kukaa kimya tungepata hasara gani?Maana inaonekana unadhani katiba ni kitabu tu.Mkuu tusipokuwa na sheria nzuri na institutions za kuhakikisha hizo sheria zinafuatwa na kuheshimiwa na kila mtu tunajidanganya wenyewe.Hata maandiko matakatifu yanatuambia amelaaniwa mtu yule anaemtegemea mwanadamu na ikawa na sustainable development, Ya Libya umeshaona,ya Tanzania unayajua na ya Rwanda utayaona just wait
Kila muwamba ngoma huvutia kwake
Nyerere yeye kipaombele chake ilikua kuikomboa afrika
Aaaaah Geita yote ni milima...aaaaaahaaahHaya maelezo yako ni ya uongo sana, eti kila Rais, hivi hizo barabara za lami zinazojengwa kila kona ya nchi hii kuna marais na huko? Mtwara iringa wanajenga uwanja mkubwa tu wa ndege, katavi wamejenga kwann chato ambayo ipo mkoa wa geita wasijenge? Utasema wangejenga geita, geita hamna eneo pale ni milima tu, labda wangejenga kuelekea Mwanza ndio unaweza pata eneo la kujenga uwanja wa ndege, sababu ndio utapata maeneo tambalale. Suala la katiba hilo nakuunga mkono , nyerere hapo alichemka.
Ebu sema sehemu gani ya geita karibu na geita mjini inafaa kujenga uwanja wa ndege ? Sababu geita naifahamu sanaAaaaah Geita yote ni milima...aaaaaahaaah
Mkuu hapa unataka kuongea nini? kwamba ujinga wa watanzania tulio wengi ndo misingi ya taifa letu au Tanzania ni mali ya nyerere na chama chake? By the way taifa ni nini na taifa la Tanzania lilianzishwa lini na nani?ujinga wetu na uendawazimu wa wachumia tumbo wa ccm usikufanye uone katiba si muhimu.Nchi nyingi zilizopiga hatua kimaendeleo na zenye sustainable development ni zile zilizowekeza kwenye katiba bora yenye institutions imara na independent za kuhakikisha inafuatwa ukilinganisha na shithole zinazotegemea fikra za watu.Hata home kwako kama hauna formula ya maisha na ukakubali kuifuata kwa dhati lazima ufe rofaMsiojua misingi ya kulianzisha Taifa hili mtaweweseka sana.
Katiba ni muhimu lakini bila kuelewa inapatikana vipi mtahangaika sana.
Hata leo nenda pale Kariakoo muimbie mmachinga juu ya katiba, kama atakuelewa una bahati.
Miaka ya 70s wakati wa Mwalimu ni wasomi wachache sana waliohamasika kumpinga Mwalimu, sembuse katiba.
Na chama kilikuwa kimoja TANU/CCM.
Ni watu wachache zaidi , kama James Mapalala, waliodiriki kuongea juu ya mageuzi ya kisiasa kwa ujumla.
Leo wasomi ni wengi na vyama ni vingi , na vyama vingi vilikuja kwa ruhusa ya Mwalimu.
Mazingira ya leo ukiongelea katiba na mageuzi yake, watu watakuelewa.