mafutamingi
JF-Expert Member
- Feb 14, 2011
- 2,775
- 2,198
Mwalimu Julius Nyerere katika kipindi chote cha uongozi wake alikataa kata kata kuigeuza Butiama ionekane kwamba pale ndipo nyyumbani kwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania.
Kwa mfano Mara kwa mara kulikuwa na mipango au hata shinikizo kutoka serikalini kujenga barabara ya lami hadi Butiama. Lakini kila mara suala la barabara ya lami lilipoibuliwa, Mwalimu aliendelea na msimamo wake.
Wakati fulani pendekezo hilo lilipomfikia aliuliza - "mnataka barabara ya lami iende kufuata nini Butiama? Kuna nini huko? Hakuna zao lolote la biashara huko. Hakuna kahawa, pamba, n.k.
Kuna mihogo tu! Sasa barabara ya lami iende kufanya nini!" Kwa hiyo Butiama iliendelea bila kuwa na barabara ya lami hadi alipofariki. Baada ya kifo chaketu Rais Mkapa akaweka lami.
Ifahamike kwamba Butiama iko takribani Km 15 kutoka Kiabakari ambapo barabara kuu itokayo Musoma kwenda Mwanza inapita. Lakini hii isitafsiriwe kwamba Mwalimu hakupenda maendelea ya Butiama.
Alipenda sana maendeleo na ndiyo maana aliweka mradi wa kilimo cha umwagiliaji pale Kyarano - jirani tu na Butiama. Kuna wanaomsifu kwamba alikuwa kielelezo cha kiongozi ambaye hajipendelei.
Lakini pia kuna wanaomlaumu kwamba alisahau nyumbani kwao kwa sababu "charity starts at home"! Kundi hili pia linasema hata Yesu alipowa wanafunzi wake kazi ya kueneza injili aliwaambia waanzie Yerusalemu. Wewe wasemaje kuhusu hili?
Kwa mfano Mara kwa mara kulikuwa na mipango au hata shinikizo kutoka serikalini kujenga barabara ya lami hadi Butiama. Lakini kila mara suala la barabara ya lami lilipoibuliwa, Mwalimu aliendelea na msimamo wake.
Wakati fulani pendekezo hilo lilipomfikia aliuliza - "mnataka barabara ya lami iende kufuata nini Butiama? Kuna nini huko? Hakuna zao lolote la biashara huko. Hakuna kahawa, pamba, n.k.
Kuna mihogo tu! Sasa barabara ya lami iende kufanya nini!" Kwa hiyo Butiama iliendelea bila kuwa na barabara ya lami hadi alipofariki. Baada ya kifo chaketu Rais Mkapa akaweka lami.
Ifahamike kwamba Butiama iko takribani Km 15 kutoka Kiabakari ambapo barabara kuu itokayo Musoma kwenda Mwanza inapita. Lakini hii isitafsiriwe kwamba Mwalimu hakupenda maendelea ya Butiama.
Alipenda sana maendeleo na ndiyo maana aliweka mradi wa kilimo cha umwagiliaji pale Kyarano - jirani tu na Butiama. Kuna wanaomsifu kwamba alikuwa kielelezo cha kiongozi ambaye hajipendelei.
Lakini pia kuna wanaomlaumu kwamba alisahau nyumbani kwao kwa sababu "charity starts at home"! Kundi hili pia linasema hata Yesu alipowa wanafunzi wake kazi ya kueneza injili aliwaambia waanzie Yerusalemu. Wewe wasemaje kuhusu hili?