Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Joined
Oct 25, 2013
Posts
63
Reaction score
262
Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha.

Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.

Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----
 
Safari njema Nyaronyo, huenda mtakuwa katika mahusiano mazuri na Kikwete, maana wiki iliyopita ulilalamika kuachwa katika uteuzi wa wajumbe wa Bunge la Katiba, licha ya kukidhi vigezo vyote
 
Sijamwelewa hapa. Is this really a parting shot?

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.
 
mwanasheria nguli mkali wa fasihi umefikisha ujumbe kwa mkuu wa kaya.mzee wa tabasamu,mtu wa kusamehe ingawa anawajua majangili,wezi ,wauza poda,.......kweli nyaronyooooo kicheeeeeeere umetisha
 
Naam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu
 
Jina lenyewe ukiita tu vidonda vya tumbo hapo hapo.Kwani akihama lazima kila mtu ajue au sifa za kijinga tuu.
 
Sidhani kama CCM wanaweza kumpokea huyu hata wakipewa bure. Huyu ni mmoja wa waliomwandikia Rais KIMEMO cha kutaka ateuliwe kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba, taarifa zimevuja.
 
Hawa walikuwa wanacheka cheka hovyo wakati wanadai uhuru, ama kuyakomboa mataifa yao kutoka kwenye makucha ya mabeberu weusi wanyonyaji? taifa letu linahitaji ukombozi wa kuwatokomoeza hawa mabepari weusi wanaolitafuta bila huruma.
images
images
images
images
images
images




Huyu kicheere ni MPIGANAJI hasa siku moja hawezi kwenda Lumumba!! someni tena hoja ya mlete hoja!!
 
Back
Top Bottom