Nukuu ya DR.Ulimboka

Nukuu ya DR.Ulimboka

mbinguni

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2013
Posts
2,767
Reaction score
1,068
“Nathibitisha kwamba Ramadhan Ighondu alitambulishwa kwetu kwa jina la Abeid. Binafsi ninamfahamu sana bwana huyu kwa sababu alikuwa akitumwa mara kwa mara kuja kukutana na mimi na tumekutana mara kadhaa kabla ya tukio lile,” lilisomeka tamko hilo na kuongeza: “Nakumbuka kuwa Abeid alitambulishwa kwetu na kigogo mmoja, nikiwa pamoja na wawakilishi wengine wa madaktari kuwa yeye (Ramadhan Ighondu) ndiye atayehusika katika kuchukua madai na hoja za madaktari katika mgogoro kati ya madaktari na serikali.
“Nathibitisha kwamba mfanyakazi huyu wa Ikulu, ndiye aliyenipigia simu na kuniita kwenye kikao ambako muda mfupi baadaye nilitekwa. Katika mawasiliano hayo, Abeid alikuwa anatumia simu Na. 0713 760473,” alisongeza Dk. Ulimboka kupitia tamko hilo.
Wana JF naomba tuijadili nukuu hii kwa fikra mbadala.Karibuni.
Source:Tanzania Daima 18/1/2013.
 
tujadili na wagonjwa walioteseka kwa kukosa matibabu wakati madaktari wamegoma
 
wagonjwa zaidi ya mia tatu 300 walikufa kwa kukosa huduma za madaktari waliokuwa ktk mgomo wa kijinga
 
ulimboka ni muuaji wa watanzania wasiokuwa na hatia. roho za waliokufa bila hatia kwa kukosa huduma zitamdai haki hiyo hata mbinguni
 
watu waliokuwa wanapokea mishahara iliyotokana na kodi za watanzania halafu wanagoma kuwahudumia ni wasaliti na ni wauaji wakubwa
 
wagonjwa zaidi ya mia tatu 300 walikufa kwa kukosa huduma za madaktari waliokuwa ktk mgomo wa kijinga

Mbona wagonjwa wanakufa ovyo kwa kukosa huduma hata kama hakuna mgomo? Mwogope mungu walilokuwa wanafanya kina Uli ni kudai mazingira bora ya kazi ambayo yatasaidia kupunguza hivyo vifo unavyosema wewe. Aibu sana kwako kaka.
 
mwaka wa nguvu ya umma huu lazima tukumbushie matukio yaliyopita ili umma utuhurumie
 
wagonjwa zaidi ya mia tatu 300 walikufa kwa kukosa huduma za madaktari waliokuwa ktk mgomo wa kijinga

wewe na serikali mnaweza kuorodhesha wagonjwa waliokufa kwa sababu ya mgomo?au unashabikia tu kwa hisia,unajua madaktari walikuwa wanadai nini?je ni wagonjwa wangapi wanaokufa kwa kukosa vifaa tiba?au vifaa ulivyoonyeshwa MNH ndio ukaona viko kila hospitali?funguka ndugu,mbona serikali yako ilimpiga ulimboka?mbona wanaona makengeza kumhoji yeye mwenyewe?
 
Nakumbuka kuwa Abeid alitambulishwa kwetu na kigogo mmoja Tafadhali julisha kigogo ndio kitu gani kwanini Dakta anashindwa kutumia jina halisi la hiki kigogo?!
 
Mbona wagonjwa wanakufa ovyo kwa kukosa huduma hata kama hakuna mgomo? Mwogope mungu walilokuwa wanafanya kina Uli ni kudai mazingira bora ya kazi ambayo yatasaidia kupunguza hivyo vifo unavyosema wewe. Aibu sana kwako kaka.

wale walikuwa wanadai mishahara minono, mengine ilikuwa ni kuwadanganya watanzania. shame on you and them
 
mishahara ya 3.5ml/= huku watanzania wanateseka kwa kukosa panadol,hata huruma hatuna
 
Inaelekea wachangiaji wengi wana nia ya kupotosha mada, nadhani mleta mada anachosema kama Dr Ulimboka alifanyiwa attempt ya kuuawa, hilo ni kosa la jinai, sasa yeye mwenyewe aliyetendewa jinai hiyo anatoa clues, ambazo siku zote ndiyo polisi huwa wanasisitiza kutaka ushirikiano huo toka kwa raia wema. Sasa hapa swala la msingi ni kwa nini polisi hawataki kuzifanyia kazi taarifa za mtu aliyekumbwa na dhahama hiyo, na kumtia mbaroni huyo mtuhumiwa ili imhoji??!! Badala yake wamemng'ang'ania yule chizi wa Kova, ambaye naye ameomba ifanyike parade ya kipolisi,ili aitwe Ulimboka, amtambue mtuhumiwa wake, je ni kwa nini na hili Polisi haawataki kulifanya??!! Kweli nimeamini nchi hii inaendeshwa kwa staili ya kimazingaombwe!!
 
wagonjwa zaidi ya mia tatu 300 walikufa kwa kukosa huduma za madaktari waliokuwa ktk mgomo wa kijinga

Osama hufai kabisa je unajua ni watu wangapi wamekufa leo kwa kukosa panadol na akina mama kukosa cloves za kujifungulia na vifaa vingine.
 
tujadili na wagonjwa walioteseka kwa kukosa matibabu wakati madaktari wamegoma

Wagonjwa mbona wanateseka hata leo hii ambapo hakuna mgomo na walikuwa wakiteseka hata kabla ya Dr.Uli kutekwa!
Kwa sasa DCI Manumba yuko ICU anateseka kwa kupumlia mashine huku akiwa na vijidudu 500 vya Malaria! Nani wa kulaumiwa?Je, Dr.Uli na watumishi wengine wa afya wanahusikanaje hapa????

Hoja yangu ni kwamba mgomo wa Madaktari haukuhusika na mateso ya wagonjwa baali kile kilichokuwa kikipiganiwa na hao Madaktari ndiyo kingeliondoa mateso kwa wagonjwa. Bila vitendea kazi bora na muhimu afya ya Mtanzania siku zote iko rehani. Kama hakuna maabara zenye kupima ugonjwa husika kwa uhakika ni kazi bure. Kama hakuna CT-scan, hakuna X-rays machine, hakuna Ultra Sound, hakuna Stesoscape, hakuna Madawa muhimu ni upuuzi kumlaumu daktari! Bado kuna dada zetu na mama zetu wanajifungulia kwenye sakafu za hospitali na zahanati kwa kukosa vitanda au wanalala mzungu wa nne! Kila mtu analijua hili lakini kwa vile kuna watanzania wahuni na washenzi wanajifanya kuwa vipofu na kuamua kugandamiza haki za sekta muhimu kama hii!!Shame on them. naamini siku ya kiyama watajibu mbele za Muumba kwanini walisababisha vifo vya wagonjwa kwa maksudi!!!

Serikali ndiyo inayosababisha mateso kwa wagonjwa na ilikosea sana kutaka kuzima mgogoro huo wa Madaktari kwa nguvu ilhali Madaktari walikuwa na hoja za msingi.

Tafakari.
 
wale walikuwa wanadai mishahara minono, mengine ilikuwa ni kuwadanganya watanzania. shame on you and them

We unajua madokta wangapi sasa wanapiga part time kwenye hospital binafsi? Hivi wangelipwa mshahara wanaotaka unadhani isinge washawishi kutumika katika hosp za serikali mwanzo mwisho?

Chukulia mfano wewe kama Nape hajakupa posho yako leo utakubali?
 
Back
Top Bottom