NSSF Mnatuyeyusha sana!!!

King Kong III

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
51,635
68,565
1.Hela nimeweka tangia 2002 lakini nikija kustaafu/kuresign napata hela hile hile niliyochangisha,hivi laki 2 ya 2002 ni sawa na hii ya 2012? Kwanin msifanye michakato ya kuwalipa watu mafao yao kwa ongezeko kulingana na thaman halisi ya sasa?

2.Michango yetu mnafanyia biashara na mnapata faida sana na mna-extend biashara hadi nchi za jirani,iweje sisi wadau wakuu,hamtuingizii bonus(faida) ya biashara yenu wakati sisi ndio wanahisa wakuu?

3.Inakuwaje hela zetu sisi wenyewe hatuwezi kukopeshwa? Lakin hizo pesa mnakopesha watu wengine ambao sio hata wanachama,kwanin msiweke mchakato wa kukopesha wanachama kama wanavyofanya saccos kwamba mkopo unapata kulingana na amount uliyochangia?

4.Yanini mtu akistaafu au kuresign anasubiri miezi sita yote hayo ya nini? Kwanin msiwabane waajiri kwamba kila mwisho wa mwezi wapeleke michango yao ambao inakua easy mtu ukiacha kazi upate stahili zako ndani ya wiki moja au mbili tu kama PPF wanavyofanya.

Nawaomba wadau wa NSSF myafanyie kazi hayo mambo la sivyo katiba mpya lazima iyaingize hayo mambo!!!

Nawasilisha.
 
Wewe umesema , hata mie huwa najiuliza, ni kwanini utasikia pesa za nssf zinakopeshwa watu ambao wala hawana uchungu nazo, lakini sisi wenyewe tunaambulia patupu, viji interest vinavotolewa ni viduuuuchu sana kulingana na pesa yenyewe. Kitu kingine mie huwa najiuliza utaambiwa hii ni benefit ya kitu fulani labda mafao ya uzazi halafu eti kama unachukuwa pesa yako kabla ya umri wa kustaafu kama umeacha kazi basi wanakata yale mafao! nashangaa kwanini waite mafao wakati wanamkata mwanachama au kwanini hawamuelimishi mwanachama kabla ya kuchukuwa?

Kuhusu mikopo nimesikia juzi wataanza kutoa mikopo kupitia sccos sasa sijui sie tusokuwa katika saccos inakuwaje ! hapa kuna kaujanja katatumika kunenepesha watu!

Khatariiiiii
 
Wewe umesema , hata mie huwa najiuliza, ni kwanini utasikia pesa za nssf zinakopeshwa watu ambao wala hawana uchungu nazo, lakini sisi wenyewe tunaambulia patupu, viji interest vinavotolewa ni viduuuuchu sana kulingana na pesa yenyewe. Kitu kingine mie huwa najiuliza utaambiwa hii ni benefit ya kitu fulani labda mafao ya uzazi halafu eti kama unachukuwa pesa yako kabla ya umri wa kustaafu kama umeacha kazi basi wanakata yale mafao! nashangaa kwanini waite mafao wakati wanamkata mwanachama au kwanini hawamuelimishi mwanachama kabla ya kuchukuwa?

Kuhusu mikopo nimesikia juzi wataanza kutoa mikopo kupitia sccos sasa sijui sie tusokuwa katika saccos inakuwaje ! hapa kuna kaujanja katatumika kunenepesha watu!

Khatariiiiii

Mkuu hawa NSSF lazima tuwaingize kwenye katiba mpya maana wanatufanya wanachama mapoyoyo,kwanin hyo hela waipeleke kwenye saccos? Hapo kuna wizi unataka kufanyika kumbuka mabilioni ya JK,fedha za EPA ndio huko huko,watukopeshe wanachama direct na sio kupitia saccos,mtaji wangu si upo kwao na kila mwezi nachangia mapato?
 
Kaka hawakati Mankato mie nimechangia toka 2004 na Jana nimekamata ila in Baaada ya mwaka wa kuhangaika
 
Kaka hawakati Mankato mie nimechangia toka 2004 na Jana nimekamata ila in Baaada ya mwaka wa kuhangaika

Cha kujiuliza kwanini wakuangaishe mwaka mzima wakati hela ni zako? Hivi amount uliyochangia 2004 thamani yake ni sawa na hii 2012? Enzi hizo mchele kilo sh600,unga 350 sukari 600!!!
 
halafu wewe ukitaka kukopa, lazima kutakuwa na riba. fedha hiyo hiyo wanawekeza na kupata faida kubwa, kwa nini sisiw anachama tusiwe sehemu ya faida hiyo?
 
Back
Top Bottom