Afadhari sasa, nadhani na siye wa sekta binafsi huku kunaweza kua na utulivu sasa; ukweli sielewagi kabisa kwanini SSRA wanao ishi kwa fadhila za hiyo mifuko ya jamii wanatupa shida sana wafanyakazi; wafanyakazi hatuna mkataba na SSRA, tuna mkataba na mifuko ya jamii kama NSSF, PPF, PSPF nk. Binafsi sioni umuhimu wowote wa shirika hilo, lipo kwa ajili ya kutengeneza matumizi tu na sio ku generate pesa. Nipo tayari kukosolewa kwa hilo, na ningekutana na mhe rais kwangu mimi hilo ndio lingekua wazo langu la kwanza kumpa. Hakuna mantiki yoyote ya kuanzisha shirika linalo tafuna tu pesa kwa TIJA ambayo wala haipo.