Zaydkhan
Member
- Mar 31, 2017
- 36
- 46
Kuna jamaa yangu kanipa mkasa wake kilichomkuta Nssf alipoenda kufuatilia mafao yake. Nimeona niilete humu;
Jamaa anasema miezi kadhaa huko nyuma alienda Nssf kwenda kufuatilia madai yake. Wakampa utaratibu wa kujaza. Wakamwabia aende stationary watamsaidia kufungua. Jamaa akaenda stationary akawachia taarifa zake ili wamjazie.Alivomaliza akawa anasubir hela zake.
Imepitia miezi miezi miwili akaona kimya, ikabidi aende kwenye TAWI kuulizia. Tawini wakamwambia hela tumeshaingiza ila utapokea kwa 33% sababu wewe umejaza una digrii.
Jamaa akalalamika kuwa hiyo kazi aliyoajiriwa haikuwa ya Elim na hiyo Elim hajafika itakuwa jamaa wa stationary alikosea kujaza. Mhudum akamwambia andika barua.
Jamaa akaandika akawapa. Wakamwambia Subiri Uchunguzi tutakupigia.
Baada ya kukaa muda mrefu alivoona kimya,hakuna majibu akawaendea. Yule mchunguzi akamwambia Mwajiri wako kasema una digrii kwa hiyo subiri tukuandikie barua ya majibu yako.
Jamaa akauliza alikuonesha kopi za vyeti, Mhudum akajibu hakunionesha.
Kwenye barua jamaa kaambiwa tumefanya Uchunguzi na uhakiki kutoka kwa Mwajiri wako ivyo wewe una digrii.
Jamaa akampigia simu yule mchunguzi akimuuliza huo Uchunguzi na uhakiki ulifanya vipi, Mimi nahisi wewe ndio ulimpa hizo taarifa zangu Mwajiri na yeye akajibu hivyo ili kunikomoa sababu nina migogoro nao mahakamani.
Mhudumu alisema alitumia njia ya ofisi akaandika barua na Mwajiri akajibu hivyo. Jamaa akataka mwajiri atoe uthibitisho wa taarifa zake alizozitoa, Mhudumu akamwambia aandike barua ya kukata rufaa.
Jamaa anasema hapa alipoanza kutaka Uchunguzi wa majibu ya Mwajiri wake ndo milolongo ikawa mingi. Akaandika barua. Imepita muda alivyoona kimya akampigia yule mchunguzi wao, akamwambia anafuatilia.
Akakaa tena muda alivompigia yule mchunguzi akasema kuwa lile jambo lipo nje ya uwezo wake, hivyo ishu wameipeleka makao makuu asubiri watampigia.
Akakaa muda mrefu ndio wakampigia hivi karibuni aende makao makuu. Kwenda kule mchunguzi wa kule akaanza kumhoji akitaka taarifa zake za shule ya msingi ili waende kufuatilia kuanzia uko shule.
Jamaa akakataa akamwambia mbona milolongo inakuwa mingi, hii kesi Ina miezi mitatu , mimi nilijua mmeniita mnipe majibu yenu ya Uchunguzi, Leo unataka taarifa zangu za shule ya msingi mkaanze kufuatilia, mlishaenda kwa Mwajiri akawaambia nina digrii, nilivyotaka uthibitisho wa mwajiri, Mwajiri kashindwa kuthibitisha.
Jamaa alikataa akamwambia hizo taarifa mnazozitaka zote zipo kwa Mwajiri wangu. Mlivyoenda kwa Mwajiri hajawapa?.
Jamaa anasema wakaanza mabishano na pale alipomwambia mchunguzi aende kuchukua hizo taarifa kwa Mwajiri wake, mchunguzi alikuwa mkali hataki suala la kwenda kwa Mwajiri.
Mchunguzi akamwambia jamaa kama hutaki kunipa hizo taarifa mi nafunga kesi na ukienda NSSF yoyote utaambiwa uje makao makuu.
Na Mimi nikiwa hapa utakuja kwangu lazima unijibu maswali yangu niendelee na Uchunguzi.
Nilimuuliza jamaa kwa nini haukujibu kama anavyotaka?
Jamaa anasema ile kesi ilikuwa ishaisha ila walikuwa wanataka kuniongezea milolongo, anaamini kuwa zile taarifa alizozitoa mwajiri wake alipata kupitia NSSF eiza Mfumo wao au mtumishi wao aliyekuwa anafanya Uchunguzi.
Hivyo, NSSF waliporudi tena kwa Mwajiri kutaka uthibitisho Mwajiri hakuwa na taarifa nyingine ya kutoa. Kwa vile Mwajiri ameshindwa kutoa taarifa kesi ilikuwa imeisha, wao wanakomaa kuzuia iyo hela waendelee kufanya Uchunguzi kwanini?.
My take.
Nssf punguzeni milolongo isiyo ya lazima, mnawapotezea watu muda kuja ofisini kwenu mara kwa mara na kuwapa depression tu.
Mwisho wa siku mtu kama huyu akiajiriwa tena anaweza kukataa mambo ya kufungua Nssf.
Binafsi nimeona ubabaishaji sababu Sheria inawaruhusu Nssf kwenda kwa Mwajiri na kuhakika taarifa za mwanachama. Sasa, sijajua kwa Nini mchunguzi alikuwa mkali na hataki suala la kwenda kuhakiki kwa Mwajiri, yeye anataka taarifa za shule ya msingi aende kufuatilia site.
Jamaa anasema miezi kadhaa huko nyuma alienda Nssf kwenda kufuatilia madai yake. Wakampa utaratibu wa kujaza. Wakamwabia aende stationary watamsaidia kufungua. Jamaa akaenda stationary akawachia taarifa zake ili wamjazie.Alivomaliza akawa anasubir hela zake.
Imepitia miezi miezi miwili akaona kimya, ikabidi aende kwenye TAWI kuulizia. Tawini wakamwambia hela tumeshaingiza ila utapokea kwa 33% sababu wewe umejaza una digrii.
Jamaa akalalamika kuwa hiyo kazi aliyoajiriwa haikuwa ya Elim na hiyo Elim hajafika itakuwa jamaa wa stationary alikosea kujaza. Mhudum akamwambia andika barua.
Jamaa akaandika akawapa. Wakamwambia Subiri Uchunguzi tutakupigia.
Baada ya kukaa muda mrefu alivoona kimya,hakuna majibu akawaendea. Yule mchunguzi akamwambia Mwajiri wako kasema una digrii kwa hiyo subiri tukuandikie barua ya majibu yako.
Jamaa akauliza alikuonesha kopi za vyeti, Mhudum akajibu hakunionesha.
Kwenye barua jamaa kaambiwa tumefanya Uchunguzi na uhakiki kutoka kwa Mwajiri wako ivyo wewe una digrii.
Jamaa akampigia simu yule mchunguzi akimuuliza huo Uchunguzi na uhakiki ulifanya vipi, Mimi nahisi wewe ndio ulimpa hizo taarifa zangu Mwajiri na yeye akajibu hivyo ili kunikomoa sababu nina migogoro nao mahakamani.
Mhudumu alisema alitumia njia ya ofisi akaandika barua na Mwajiri akajibu hivyo. Jamaa akataka mwajiri atoe uthibitisho wa taarifa zake alizozitoa, Mhudumu akamwambia aandike barua ya kukata rufaa.
Jamaa anasema hapa alipoanza kutaka Uchunguzi wa majibu ya Mwajiri wake ndo milolongo ikawa mingi. Akaandika barua. Imepita muda alivyoona kimya akampigia yule mchunguzi wao, akamwambia anafuatilia.
Akakaa tena muda alivompigia yule mchunguzi akasema kuwa lile jambo lipo nje ya uwezo wake, hivyo ishu wameipeleka makao makuu asubiri watampigia.
Akakaa muda mrefu ndio wakampigia hivi karibuni aende makao makuu. Kwenda kule mchunguzi wa kule akaanza kumhoji akitaka taarifa zake za shule ya msingi ili waende kufuatilia kuanzia uko shule.
Jamaa akakataa akamwambia mbona milolongo inakuwa mingi, hii kesi Ina miezi mitatu , mimi nilijua mmeniita mnipe majibu yenu ya Uchunguzi, Leo unataka taarifa zangu za shule ya msingi mkaanze kufuatilia, mlishaenda kwa Mwajiri akawaambia nina digrii, nilivyotaka uthibitisho wa mwajiri, Mwajiri kashindwa kuthibitisha.
Jamaa alikataa akamwambia hizo taarifa mnazozitaka zote zipo kwa Mwajiri wangu. Mlivyoenda kwa Mwajiri hajawapa?.
Jamaa anasema wakaanza mabishano na pale alipomwambia mchunguzi aende kuchukua hizo taarifa kwa Mwajiri wake, mchunguzi alikuwa mkali hataki suala la kwenda kwa Mwajiri.
Mchunguzi akamwambia jamaa kama hutaki kunipa hizo taarifa mi nafunga kesi na ukienda NSSF yoyote utaambiwa uje makao makuu.
Na Mimi nikiwa hapa utakuja kwangu lazima unijibu maswali yangu niendelee na Uchunguzi.
Nilimuuliza jamaa kwa nini haukujibu kama anavyotaka?
Jamaa anasema ile kesi ilikuwa ishaisha ila walikuwa wanataka kuniongezea milolongo, anaamini kuwa zile taarifa alizozitoa mwajiri wake alipata kupitia NSSF eiza Mfumo wao au mtumishi wao aliyekuwa anafanya Uchunguzi.
Hivyo, NSSF waliporudi tena kwa Mwajiri kutaka uthibitisho Mwajiri hakuwa na taarifa nyingine ya kutoa. Kwa vile Mwajiri ameshindwa kutoa taarifa kesi ilikuwa imeisha, wao wanakomaa kuzuia iyo hela waendelee kufanya Uchunguzi kwanini?.
My take.
Nssf punguzeni milolongo isiyo ya lazima, mnawapotezea watu muda kuja ofisini kwenu mara kwa mara na kuwapa depression tu.
Mwisho wa siku mtu kama huyu akiajiriwa tena anaweza kukataa mambo ya kufungua Nssf.
Binafsi nimeona ubabaishaji sababu Sheria inawaruhusu Nssf kwenda kwa Mwajiri na kuhakika taarifa za mwanachama. Sasa, sijajua kwa Nini mchunguzi alikuwa mkali na hataki suala la kwenda kuhakiki kwa Mwajiri, yeye anataka taarifa za shule ya msingi aende kufuatilia site.