NSSF Kimewaka

hakitaeleweka mpaka hii sheria waiondoe..... Watoe hela waache kutuchezea vichwa
 
Hivi tunakwenda wapi????? Yaaani baada ya serikali kukopa kwenye haya mashirika hadi kuyaacha hayana kitu wanakuja na sera dhulumati kwa wananchi wao wenyewe??? Hivi kweli hii ni haki??????? Kwa nini sisi watanzania tunaburuzwa kama kondooo wanaolekea machinjiaoni???? Hili hakika linaumiza, yaani mshahara wangu wanikate halafu pale ninapoitaji kurudishiwa hayo makato wao ndio wanaoamua wakati wa kunirudishia wana hakika gani kila mwanachama atafikisha miaka 55 au 60??? Jamani huu si wizi wa mchana kweupeeeeee?????? Watanzania kamata mwizi meeeeeen kamata mwizi meeeeeen????? Hivi wewe Rais J. M. Kikwete tuliyekupa dhamani ya kutuongoza pamoja na kwamba waliokuchagua hawafiki hata asimilia 40 ya watanzania wote, ndio kusema mmefika mwisho wa kufikiri namna ya kupata pesa za kuendesha nchi mpaka mtegemeee kodi za wafanyakazi na kuwaibia hakiba yao kupitia mifuko hii???????? Shame on you and your government????? This is toooo baaaaaaad for the country???? Why are you breeeeeeding us alive???????
 
Watu wanajichotea fedha nyingi katika mifuko hiyo,wanajifanya kujenga madaraja ili wapate jinsi ya kutafuna vzr,mfano mweshimiwa raisi akitaka tu pesa labda anataka mil 300 kwa mfano nssf anamwambia tu dau naitaji yy anakuja anachua anapeleka alaka iwezekanavyo si anateuliwa raisi hawezi kuleta ubishi hata siku moja zaidi na kusema na mm niongezee 50 mil ka kwangu.ila mtu kama ingelikuwa mtu anafanya interview huwezi ukampelekesha kama unavyotaka.na sasa hv kuna pesa nyingi sana zimechotwa mali ya watanzania zipo nje watu wanatuna miili yao yani janjajanja nyingi,wanaogopa kufirisika ndio maana wanasema ukifikisha miaka ya kustahafu.mm sitegemei kuendelea kufanya kazi kwa mwajili siku zote nimejipangia miaka 10 tu naanza biashara zangu na nategemea pension yangu niweze kuongezea niendele na mambo yangu,kibaya zaidi kwa kustukiza bora mtu angelekua anajua.na mm ambaye nimeshaacha kazi na asilimia kubwa ya mtaji wangu nategemea pension na nina miaka 30 nisubiri miaka 25 tena kama sio kuninyanyasa na jasho langu ni nn?.
 
1
Kumb. Na. AE/164/334/Vol.II/2 20 JULAI, 2012
Makamu wa Rais, Corporate Affairs
Barrick Gold
S.L.P 1081
Dar-es-Salaam
UFAFANUZI KUHUS FAO LA KUJITOA KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII.
Ufuatao ni ufafanuzi mfupi kuhusu marekebisho ya Sheria za Mifuko hasa kuhusu fao la kujitoa.
1. Kama mtakumbuka Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na Sheria ya Mamlaka zimefanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge tarehe 13 Aprili, 2012. Sheria hiyo tayari imeshasaininiwa na Mheshimiwa Rais na imeanza kutumika rasmi. Marekebisho haya yanawahusu wafanyakazi wote nchini mwetu bila kubagua sekta yoyote ile.
2. Kwa mujibu wa marekebisho hayo fao la kujitoa (withdrawal benefits) yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo. Mafao hayo yalikuwa yanatolewa pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi. Sasa mwanachama wa Mfuko atapata mafao yake pale atakopfikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka 55) au kwa lazima (miaka 60) au pale anapopata ulemavu wa kudumu.
3. Kwa kuzuia fao la kujitoa mwanachama anapata fursa ya kupata mikopo ya nyumba kwa kutumia dhamana ya michango yake kama ilivyoelezwa kwenye Sheria ya SSRA kipengele cha 38.
4. Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili kutimiza lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu maisha ya uzeeni wakati ambapo nguvu ya kufanya kazi tayari imeshamwishia. Mafao ya kujitoa yanapunguza na hata kuondoa kabisa kinga ya mfanyakazi pale anapoumia kazini au anapofika uzeeni.
5. Tunawaomba muwaelimishe wafanyakazi umuhimu na madhumuni ya mafao ya hifadhi ya jamii. Hifadhi ya jamii ni nyenzo mahususi iliyowekwa kuwasaidia
2
wafanyakazi kuendesha maisha yao wakati wanapokuwa wameishastaafu tayari. Umasikini wa kipato wakati wa uzee ni mojawapo ya changamoto ngumu kukabiliana nazo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Tunawasihi tena muelimishe wafanyakazi kuhusu jambo hili. Tafadhali msisite kuwasiliana na Mamlaka pale ufafanuzi zaidi utakapohitajika
6. Kwa kuwa marekebisho hayo yamesainiwa na kuanza kutumika rasmi kama sheria, mafao ya kujitoa hayawezi kutolewa tena na wafanyakazi watakaoacha kazi kwa sababu ya marekebisho ya kipengele hicho watakuwa hawajaijitendea haki wao wenyewe na pia itakuwa ni kunyume cha Sheria. Mamlaka inaandaa kanuni za mafao ambayo lengo lake ni kuboresha maslahi ya wanachama, kanuni hizo zitajadiliwa na wadau wakiwemo vyama vya wafanyakazi na waajiri ili kupata maoni yao.
7. Tafadhali muwaelimishe wafanyakazi kwamba pamoja na kuzuia fao la kujitoa, mafao mengine ambayo ni muhimu kwa sekta ya Madini yataendelea kutolewa kama kawaida. Mafao hayo ni Kama vile kuumia kazini pamoja na fao la ulemavu
8. Tumesikia kwamba tayari kuna hofu imejijenga kwa wanachama kuhusiana na fao la kujitoa. Ikumbukwe kwamba baadhi ya Mifuko ilikuwa inatoa fao hilo kinyume cha Sheria kwani katika Sheria zao hakuna fao la kujitoa. Tunapenda kusisitiza kwamba wanachama wawe watulivu wakisubiri miongozo.
9. Tunapenda kuwahakikishia kwamba katika hili maslahi ya wanachama yatalindwa na hakuna mwanachama atakayepunjika kutokana na utaratibu huo. Mamlaka imepanga kutembelea wafanyakazi wa sekta ya madini katika juma la kwanza la mwezi Agosti 2012 ili kutoa ufafanuzi zaidi kwa wanachama wote.
Tunatanguliza shukrani za dhati kwa ushirikiano.
Wenu.
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii
Irene Isaka
MKURUGENZI MKUU
3
 
afadhali waanze kudai, tutawaunga mikono na miguu, pumb..fu
 
Halafu nimesikia yua kwamba, sheria hiyo haiwaathiri viongozi waandamizi wa serikali kama Raisi, W/Mkuu, Wabunge, Mawaziri, Spika na M/Spika.
Nakumbuka ile kauli "sizitaki kura za wafanyakazi". Leo wameamua kuwasulubu wafanyakazi hii leo.
 
hela zimeenda wapi?

Kwa kujitakia sifa mkweree aliamrisha hela za wavujajasho zipelekwe kujenga UDOM ambayo wachina wamejenga majumba mengi chini ya kiwango hivi sasa mengi yana nyufa na kuvuja hata miaka mitatu haijapita!!! Sasa watu wanataka pesa yao toka NSSF wanawaletea mizengwe!! wametafuna fedha za NSSF na Dau kibaraka wao na sasa hawajui watazirejesha vipi hela za wafanyakazi.!!!
 
atakuwa ni yeye maana hii kitu inachanganya sana, pata picha uliacha kazi miezi mitano iliyopita hivyo unahesabu siku tu upate chako leo unaambiwa hunachako mpaka ufikishe miaka 60 wakati huo wewe una miaka 30..unaweza usirudi nyumbani

Ni kweli unaweza kujipeleka mwenyewe Mortuary Muhimbili ukamuambia mhudumu kuwa akufungulie uingie ukalale humo kuliko kwenda nyumbani ambako uliwaahidi wanaokudai kuwa mchana ukirudi aaaaaaah!!! wasiwe na hofu unawalipa zote.

Na pia mafundi uliwaambia "Fanyeni kazi nikirudi nawalipa na cement ikiisha nendeni mkachukue pale dukani nitalipa nikirudi........."

Ndugu yangu kwa nini usiende kujiingiza mwenyewe Mortuary Muhimbili?????



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Jamani tuache hata kufa tu, kampuni nyingi za private zinafanya kazi kwa muda fulani mfano kama miaka 15, 20 n.k. Kwa hiyo wanachosema mafisadi ni kwamba ukiachishwa kisa muda wa kampuni umeisha au umefukuzwa au umeacha kwa hiari basi uendelee kula nyasi weeeeeeeeeeee hadi 55-60. Nakwambia tutapigana, hili haliwezekani hata kidogo.

Wengi mnaonekana kupinga malipo ya uzeeni kutokulipwa kwa vijana; wawakilishi wetu walipitisha hili kwa maslahi ya wananchi wanaowawakilisha au kwa maslahi ya walioajiriwa katika hii mifuko?
 
wadau,hivi kweli hii serikali inaendashwa na watu wenye akili?.wanapoamua mambo haya bila kuwashirikisha wadau ambao ni sisi wanatutendea haki kweli??
We fikiria mimi nilipata kibarua mwaka jana kwa mkataba wa miaka miwili tu,na makato ya nssf yalianza mara moja baada ya kusaini mkataba huo je nitasubiri hadi nifikishe miaka 50 ndo nikadai mafao yangu hayo??
Kazi nimefanya 2011/2012 na nina umri wa miaka 20 so nitalazimika kudai mafao yangu ya miaka miwili niliyofanya kazi ifikapo mwaka 2062???
Haileti picha wala haikubaliki,kama wamezitafuna pesa zetu wakidai ni mali yao sasa wanaumbuka mchana kweupe!!!

tusikubali kwa kweli , vyam vyetu vya wafanyakazi na sisi wenyewe tufanyie kazi hii si sawa nasikia wao wabunge na wakubwa wengine haiiwahusu hii , inchi ya ajabu kabisa wale tuliowaajiri ndio wanatupelekesha na jasho letu !!!
 
Mwakilishi wa "wafanyakazi" bungeni (Angela Kairuki) amekabidhiwa u-naibu waziri and that is it... SOB...!
 
Natamani ningelijua tusi baya kuliko yote.... hilo ndo ningeipa hii serikali yenu harafu hata nisinge-log inn JF tena maana ningejua nina ban ya life time kwa kutoa tusi hilo! Too bad sina tusi ninaloweza kusema linaifaa sirikali yenu hii.... lolote unalolijua haliwafai!!!!!!!! Unajua hapa nilipo nilishakamilisha form zangu ilibidi next week nizipeleke NSSF! I hate this govt! Yes,.... with all my strength!
 
vyama vya wafanyakazi vinasubiri nini kutoa miongozo, tupo tayari kwa lolote.
 
Pension hapewi mrithi mkuu, ukiondoka dunia hii na pension kwishney! Assuming ulikuwa umeanza kupewa that is!
Mkuu sasa maandamano yetu yaanze lini maana hakuna tofauti na kuliwa 0713 huku unajiona na huwezi hata kujitetea.
 
wafanyakazi ndio tunalipa kodi kubwa bado mishahara yenyewe magumashi , uishi kwa shidashida nikisema kazi basi hela yangu nikatazwe kupewa huu i uonevu mkubwa sana.tusikubali hata kidogo
 
Hivi hili swala wapinzani wa kweli chadema huko bungeni hawajalisikia?ili waombe muongozo kwa spika lijadiliwe jamani,maana walalahoi wengi ndo wanakotegemea maana ajira zenyewe za wahindi hizi mwaka uko kazini mwaka nje.Hapa sasa kwa hili natarajia wazee wa magwanda watusaidie otherwise sitawaelewa.

Wingi wa Magamba ndio kuwepo kwa sheria hii kandamizi,2015 tukichukua madaraka tutaifuta hii sheria tupeni kura zenu ili tuwakomboe kutoka kwenye makucha yenye tetenasi na kutuuwa kabla ya wakati.
 
je ili suala linawahusu na wanasiasa ama wao wakimaliza tu term zau ubunge nk wanachukua? au wao wanasaini mikataba tofauti ya mifuko ya jamii kwamba watachukua? tueleweshane
 
Wameingia mkataba na Mungu kuwa watz wote wataishi hiyo miaka? wanataka jasho letu afaidi nani baada ya sisi kufa kabla ya hiyo miaka?
Je kama mtu ameamua kuachana na ajira akataka kujiajiri, hiyo si ndio mtaji wake wa kuanzia? lidandance linapotokea mtu anakua hakujipanga kimaisha, vipi wamzuilie pesa yake wakati hana ajira nyingine ya kumwezesha kuishi? akae na njaa mpaka hiyo miaka 55 atakuwa bado hai. Jamani! kwani TZ kuliukoni?
 
Back
Top Bottom