Notisi ya kuanzisha Mikoa na Wilaya

Na mimi naomba kijiji changu cha Nyakagwe kiwe Wilaya na Tarafa yangu ya Katoro iwe mkoa.
 
Hongera jk, wacha wapinzani wa maendeleo waseme au wabeze, kusogeza mamlaka jirani zaidi na wananchi ni muhimu sana. Hata hivyo tangu lini? Wapinzani wakapongeza kazi ya serikali iliopo itakuwa ajabu.
<br />
<br />

Mkuu maana ya aina ya upinzani unaouzungumzia unaijua!?Ni asilimia ngapi ya Watanzania wote (ktk mikoa yote)wanatumia umeme kwa shughuli za kuwaletea maendeleo achilia mbali matumizi ya kawaida!?.Pesa za kuwagharamia wakuu Wa mikoa,wakuu Wa wilaya,Wabunge na wengine wengi ili mkoa ukamilike Serikali inapata wapi hizo pesa!!?wakati hata pesa za kununulia mitambo mipya ya kufua umeme wanasema Serikali haina pesa!?Mitambo ya enzi za Mwalimu mpaka leo!!?
 
Kile kipozeo cha JK kimepangwa kupewa ukuu wa wilaya kati ya hizo mpya hapo
 
Mm kwa mtazamo wangu naona kama vile watu hawkufikiria mbali maana kama wenzetu wanatamani afrika yote iungani iwe kitu kimoja badala ya kupunguza wilaya na mikoa kwa ajili ya kupunguza matiumizi ya fedha watu ndio wanazidi kuongeza hata haiji akilini kwangu kwa kweli.
 
Morogoro na Mbeya ni Mikoa Mikubwa sana... naona hawawezi kuigawanya sababu ya Ardhi wamegawana hao wakubwa wa CCM

Wanaimaliza Mwanza sababu ya Upinzani, Wanaigawa gawa - vipi Majimbo yamekufa kabisa?
Lol! Sikujua, na Iringa je?
 
Du hii mikoa mingine,mfano kamkoa ka Pinda kana wilaya mbili tu,haiingii akilini,kupoteza hela ya walipa kodi kwa ajili ya kuanzisha mkoa wenye wilaya 2 tu heti tu kwasababu waziri mkuu anatoka mkoa huo,huo ni utumiaji mbaya wa madaraka,kama kila atakaye pata uwaziri mkuu atataka tarafa yake iwe wilaya na wilaya yake iwe mkoa ili wapate fungu kubwa basi kufikia 2050 Tanzania itakuwa na wilaya kama 130
Mkuu unataka kusema zitakuwa zimepunguwa maana kwa sasa idadi hiyo imeshavuka sana
 
Ongezeko la Mikoa 4 wilaya 19 ni ongezeko la wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, idara zake zote, Wabunge na madiwani na kadhalika wakati kichekesho ni kwamba pato la Taifa halijaongezeka kwa kiwango cha kutosheleza hata matumizi ya mikoa na wilaya zilizopo. Serikali imeshindwa kupeleka maendeleo mikoani kwa visingizio vya ukubwa wa nchi lakini wanachoshindwa kuelewa ni kwamba ukubwa ama idadi ya watu haviwezi kuwa suluhisho hata kwa kutumia mifano hai midogo sana...

Siku zote MAHITAJI hukabiliwa na USAMBAZAJI ambayo hutokana na UZALISHAJI.. kwa kidhungu wanasema DEMAND ndiyo hu determine SUPPLY ilotokana na PRODUCTION.. Sasa Tatizo la nchi yetu tunafikiria sana kutoa huduma (supply) mahala penye SHIDA (scarcity) na sii Mahitaji (demand)wakati hakuna ongezeko la Production.. Nitaendelea kusema kwamba huwezi kutumia mfumo wa Demand na Supply mahala penye SHIDA na ukosekanaji wa uzalishaji hata siku moja - Tutajiongezea matatizo zaidi.

Bajeti yetu ya Taifa ni Billioni 5 hadi 6 na haitoshi kabisa, yaani hii ni ndogo kuliko bajeti ya mji wa Toronto ambayo ni billioni 9..Sasa tunavyozidi kuigawa ktk mikoa mingi zaidi ndivyo tutavyoshindwa kutosheleza zaidi kwa sababu kila ongezeko la mkoa ni ongezeko la SHIDA ktk matumizi ya serikali wakati kipato hakikuongezeka. Tunagawa kidogo tulichonacho ktk mafungu mengi zaidi wakati serikali makini ingejijenga zaidi ktk kuongeza pato na uzalishaji..Umaskini wetu unatokana na PATO dogo na sii kugawana umaskini..

Tatizo la nchi yetu ni kwamba bado tunafikiria KIJAMAA (kikomunist).. Siasa ya Ujamaa bado haijaondoka akilini mwa hawa viongozi kiasi kwamba wanafikiria kwamba ni jukumu la serikali kupeleka maendeleo mikoani badala ya kupeleka huduma na kusimamia sera. Serikali kubwa haina maana kabisa ya usimamizi mzuri wa sera ikiwa hatuna uwezo mfukoni kukidhi matatizo yenyewe. Tunashindwa kabisa kufuata vitu vidogo na wazi kama SAFETY ya vyombo vya usafiri. Tunashindwa kuweka mfumo bora wa ukusanyaji wa kodi, Tunashindwa kuwahamasisha wananchi ktk Utajirisho, Tunashindwa kuweka sera na mikataba bora ktk Maliasili na Rasilimali zetu ili kutuletea maendeleo. Injini ya uchumi wetu inachemsha, inatakiwa kuwekwa Oil mpya, kufanyiwa service (maintanance) na sii kuongeza idadi ya watu kulisukuma gari...
 
ongezeko la idadi ya Mikoa na wilaya ni development indicator kwa wanasiasa!?
 
Shaka langu ni kwenye makao makuu ya baadhi ya wilaya au mikoa. Serikali hijajifunza bado matatizo mbalimbali nyuma tulikotoka kama uhamishaji makao makuu ya nchi kuwa Dodoma na sasa ni jambo linaloendelea kusuasua kwa wananchi kuendelea kuambiwa kuwa serikali ipo kwenye mchakacho huo.

Kati ya wilaya mpya zilizotajwa, bahati nzuri nimeshawahi kupita mara kadhaa ukanda wa kusini nyanda za juu. Mbambabay kuwa makao makuu ya wilaya ya Nyasa ni chaguo sahihi kwa vile pale pana historia na kupaendeleza kuna manufaa kwa ajili ya kupakuza kuwa bandari moja wapo muhimu katika mwambao wa Ziwa Nyasa kuwa kiungo cha biashara na nchi jirani za Msumbiji na Malawi. Ila kasoro moja tu ni kwamba mji mkuu kuwa mpakani itokeapo machafuko au vita huwa target kwa maadui.

Wilaya Mpya ya Wanging'ombe katika mkoa mpya wa Njombe si chaguo sahihi sana kwa maana kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa wa makao ya wilaya kuwa Makambako mji ambao umeshajengeka pamoja na miundo mbinu yake hivyo kuokoa pesa nyingi ambazo zitahitajika kujenga makao makuu mapya Wanging'ombe. Kuna wilaya nyingi tu ambazo zilianzishwa kwa mtindo huo mpaka leo utaona kama umefika tu tarafani au kwenye kata fulani. Makao ya wilaya pia kuwe na vigezo vya kuwa kitovu chenye mvuto kwa watumishi kuishi hapo kwani hilo lisipozingatiwa hali inayotokea Dodoma itajirudia kwamba Dodoma kwa kukutania mikutano na kisha makazi yanaendelea Dar es Salaam na serikali kuendelea kujenga nyuma za watumishi Dar badala ya Dodoma

 
Mkoa mpya wa Njombe kiuchumi uko juu kuliko mkoa mama wa Iringa, kwani nilipoingia Njombe kuna maeneo utadhani kama uko Europe vile na kabisa madhari yako, mashamba ya chai, mashamba ya miti nk, very interesting area. Ni kama Lushoto vile.
 
Tanzania raha sana. Wakati Italy, moja kati ya nchi nane tajiri zaidi ulimwenguni inapunguza mikoa, wilaya na mabaraza ya miji ili kupunguza matumizi. Soma hapa:
The adjustment plan Italian provinces and municipalities deleted to fit the budgets of 2013 Rome. (EFE) .- Berlusconi has taken the scissors. The Government of Italy yesterday approved a new budget adjustment plan of 45,500 million euros, which aims to achieve a balanced budget in 2013 to calm the markets concern over the situation facing the public finances country and will mean the elimination of more than 30 provinces, 1,500 municipalities and holidays.
[Source:
The adjustment plan Italian provinces and municipalities deleted to fit the budgets of 2013 | Economics Newspaper],
Wakati nchi tajiri ikibana matumizi, Tanzania ambayo inaingia katika nchi kumi masikini zaidi duniani, ndio kwana inaongeza utitiri wa wilaya na mikoa ili kuongeza matumizi. Moyo unaniuma sana.
 
Du hii mikoa mingine,mfano kamkoa ka Pinda kana wilaya mbili tu,haiingii akilini,kupoteza hela ya walipa kodi kwa ajili ya kuanzisha mkoa wenye wilaya 2 tu heti tu kwasababu waziri mkuu anatoka mkoa huo,huo ni utumiaji mbaya wa madaraka,kama kila atakaye pata uwaziri mkuu atataka tarafa yake iwe wilaya na wilaya yake iwe mkoa ili wapate fungu kubwa basi kufikia 2050 Tanzania itakuwa na wilaya kama 130

mkuu kwani sasa ziko ngapi?
 
Tanzania raha sana. Wakati Italy, moja kati ya nchi nane tajiri zaidi ulimwenguni inapunguza mikoa, wilaya na mabaraza ya miji ili kupunguza matumizi, [Gonga hapa: The adjustment plan Italian provinces and municipalities deleted to fit the budgets of 2013 | Economics Newspaper], Tanzania ambayo inaingia katika nchi kumi masikini zaidi duniani, ndio kwana inaongeza utitiri wa wilaya na mikoa ili kuongeza matumizi. Moyo unaniuma sana.
Hapo sasa mkuu wangu na sidhani kama kuna kiongozi wetu yeyote anafahamu kwa nini Italy wamefanya hivyo!
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
TAARIFA KWA UMMA




NOTISI YA KUANZISHA MIKOA NA WILAYARais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mamlaka aliyopewa chini ya Ibara ya 2(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaweza kuigawa Jamhuri ya Muungano katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Sheria au kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge.Katika kutekeleza Mamlaka hayo, Rais ametoa notisi ya kusudio la kuanzisha Mikoa minne (4) na Wilaya kumi na tisa (19). Notisi hizo ambazo zimetolewa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria ya Uanzishaji wa Mikoa na Wilaya Sura 397 ya Toleo la 2002 ni Tangazo la Serikali Na. 285 la tarehe 9 Septemba, 2011 kwa ajili ya uanzishaji wa Mikoa na Tangazo la Serikali Na. 287 la tarehe 9 Septemba, 2011 kwa ajili ya uanzishaji wa Wilaya.Madhumuni ya Notisi hizi ni kuzialika Taasisi na mtu mwingine yeyote ambaye ataathirika na uanzishaji huo kutoa maoni, mapendekezo au pingamizi iwapo yatakuwepo katika kipindi cha siku 21 kwa Mikoa mipya na siku 30 kwa Wilaya mpya kuanzia tarehe ya Notisi hizi.Baada ya muda uliowekwa kupita, Rais atachambua maoni, mapendekezo na pingamizi zilizotolewa na kuzitolea uamuzi kabla ya kuanzisha rasmi Mikoa na Wilaya hizo kwa kadri atakavyoona inafaa.Mikoa mipya inayoanzishwa na Makao Makuu yake ni kama ifuatavyo: -
MKOAWILAYA ZAKEMKOA ZINAKOTOKAMAKAO MAKUU
1.GeitaGeitaMwanzaGeita
Nyang'hwale(Mpya)Mwanza
ChatoKagera
BukombeShinyanga
Mpya/MbogweShinyanga
2.SimiyuBariadiShinyangaBariadi
Itilima (Mpya)Shinyanga
MaswaShinyanga
MeatuShinyanga
Busega (Mpya)Mwanza
3.NjombeNjombeIringaNjombe
Wanging'ombe(Mpya)Iringa
LudewaIringa
Makete Iringa
4.KataviMpandaRukwaMpanda
Mlele(Mpya) Rukwa



Wilaya mpya zinazoanzishwa na Makao Makuu yake ni kama ifuatavyo: -
WILAYA MPYAWILAYA MAMAMKOAMAKAO MAKUU
1. BuhigweKasuluKigomaBuhigwe
2. BusegaMagu MwanzaIgalukilo
3. ButiamaMusomaMaraNyamisisi
4. ChembaKondoaDodomaChemba
5. GairoKilosa MorogoroGairo
6. IkungiSingidaSingidaIkungi
7. Itilima BariadiShinyangaItilima
8. KakonkoKibondoKigomaKakonko
9. KalamboSumbwangaRukwaKalambo
10. KaliuaUramboTaboraKalua
11. KyerwaKaragweKageraRubwera
12. MbogweBukombeShinyangaMbogwe
13. MkalamaIrambaSingidaNduguti
14. MleleMpanda RukwaInyonga
15. MombaMboziMbeyaNdalambo
16Nyang'hwaleGeitaMwanzaNyang'hwale
17. NyasaMbinga RuvumaMbamba Bay
18. UvinzaKigomaKigomaLugufu
19. Wanging'ombeNjombeIringaWaging'ombe



Kwa taarifa hii, Wananchi wote wanaalikwa kutumia haki yao ya kisheria kutoa kwa maandishi maoni, mapendekezo na pingamizi kama zipo kwa kuzingatia utaratibu uliwekwa kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi wa maeneo husika na maslahi ya Taifa kwa ujumla. Maoni, pingamizi au mapendekezo hayo yatumwe kwa kutumia anuani ifuatayo: -
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Waziri Mkuu,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,
S. L. P 1923,
DODOMA.

E-mail hakattanga@yahoo.com
Fax- 026-2322116
Imetolewa na: -
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Waziri Mkuu,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.




9 Septemba, 2011

*************************************************
Wakuu kwa kuangalia hali halisi ya uchumi wa Tanzania kwa sasa na jinsi Taifa letu linavyokabiliwa na matatizo mengi ya kiuchumi pamoja na kijamii; ni sahihi kwa wakati huu kuanzisha mikoa mipya na wilaya mpya tena kwa idadi kubwa kama hiyo (Mikoa MINNE na Wilaya KUMI NA TISA).

Lipi jambo la muhimu kwa sasa, kuanzisha wilaya na mikoa mipya ama kuangalia namna ya kutatua matatizo yanayolikabili Taifa kwa sasa?

Swali la kujiuliza, Mbona wakati wa utawala wa awamu ya kwanza hadi ya tatu Marais wa vipindi hivyo hawakuongeza mikoa na wilaya kwa idadi kubwa kama hiyo? Iweje wakati wa awamu ya JK ndiyo tunashuhudia kila kitu kikiongezwa kama Baraza la Mawaziri, Uteuzi wa majaji, na hata Mikoa pamoja na Wilaya Mpya.

Kwa wale wenye kuliona jambo hili na madhara yake naomba tupaze sauti kukemea na kulikataa mapema.

Source: PMORALG - Home -


4.
KataviMpandaRukwaMpanda


Mlele(Mpya) Rukwa


Hizi ni dalili za kuipeleka nchi babaya zaidi!We unaanzishha mkoa una wilaya mbili?what for?

Mkoa mmoja,una RC,RAS,Wasaidizi km sita wa RAS,....RPC, na mabosi kibao!Ukiacha mishahara na marupurupu yao,wanahitaji nyumba.....magari...wasaidizi....

Ulianzishwa mkoa wa Manyara....ukienda pale ukaona ofisi za serikali utasema kweli kodi za wananchi zimeeishia pale.Maaana kuna jengo la R.C (of about 4b construction cost) RPC(ndo wanaanza kujenga),PCCb-like 1Billion,TRA- like 1billion,Tanroads- like 2billions,Hazina-like !billion na mengine. Ni gharama kubwa kuanzisha mkoa mmoja tu! kwa hii minnne sijuhi! Labda faida ni nyingi kuliko hasara,lakini kwa umaskini huu!haifai.

M
 
Back
Top Bottom