Noti mpya hazina ubora?

Lakini si tuliambiwa kuwa make-up ya notes mpya ni sawa na US $? Jamani, Tanzania! TAnzania nani alikuroga?
 
Si unajua wabongo lazima wajaribu kitu kipya, tena na hivi walivyokuwa wanajigamba kuwa hauwezi kutoa noti feki kwenye hizi mpya ngoja uje uone mziki wake
Makanjanja watawaibia sana babu zetu wauza mahindi kibaigwa ,korosho mtwara na wale wafugaji kwenye minada huko Maswa
 
Zimetengenezwa kwenye backyard ya nani hapa Bongo? Rostam, Manji au Tanil?
 
hata sababu ya kubadilisha pesa haikuwepo, ndio kwa mara ya kwanza nchi inabadili pesa na kuzirudisha za thamani ileile, mara nyingi ubadilishaji wa peas hufuatana na ufutwaji wa baadhi ya pesa na pia ubadilishaji wa rangi moja kwa moja,. sasa hizi noti zimerudi ya value zilezile hakuna hela zilizofutwa ama kuongezwa, na cha ajabua hata rangi kubwa ni zile zile, kama 10000 ilikuwa nyekundu wamezirudisha vilevile

hii nchi watu hawataacha kuiba
 
Mkuu Nguli, nasikia zinachanika kirahisi sana pia; nini kifanyike sasa? Serikali izuie mzunguko wa noti hizi mapema?

Hivi hakuna testing kabla ya kupeleka kwenye mzunguko? Wanadhani watanzania ni vilaza kutoangalia ubora wa kitu walicholetewa na wamekilipia hela nyingi kufikia kinaingizwa sokoni?

Nani wanatakiwa kubebeshwa lawama hizi? BoT? Hazina? Serikali kuu?

Bongo tambarare!
Mkuu tumeisha pigwa changa la macho, hii ni kashfa nyingine imekuja. Kwani ni sababu gani za msingi zilizofanya wabadili noti za awali? Nahisi ulikuwa ni mradi wa kujipatia 10%
 
hehehe unaweza sikia RA ndo amepewa tenda ya kuzitngeneza au yeye ndo alimleta huyo aliyezitengeneza, kwan juzi si alikua asia anatafuta wawekezaje,tanzania bana tunaijenga wote inaliwa na wachahce
 

Wana-JF: Nimeipata makala hii iliyotoka katika gazeti la Mwanahalisi la 20 August 2008 yenye kichwa cha maneno kama ilivyoonyeshwa hapo chini. Makala hii ilizungumzia tishio la Dr Idris Rashid kutaka kujiuzulu ukurugenzi mkuu wa Tanesco kutokana na kile alichokiona ‘kuingiliwa na wanasiasa' katika utendaji wake wa kazi.

Sehemu ya mwisho ya makala (highlighted in red) inatoa mwanga jinsi uchakachuaji wa noti zetu ulivyoanza kutokana na kubadilisha wachapishaji na mhusika mkuu wakati ule ni huyo huyo Dr Rashid ambaye anabeba tuhuma nyingine nyingi tu bila kuwajibishwa.

Mnadhani nani atawajibishwa katika sakata hili la sasa hivi linaloanza kutokota? Hakuna! Tusubiri tuone.



____________________________



Dr Rashid: Rada na Tanesco ni rasharasha, dhoruba ilitokea zamani

Na Stanislaus Kirobo


Katika matoleo mawili yaliyopita gazeti hili lilimuweka Dr Idris Rashid katika darubini kwa kuueleza umma aina ya watendaji wakuu wa Rais Kikwete walivyo, hususan sifa zao za kiutendaji, na kwa ujumla kujibu swali la kwa nini mamilioni ya watu wa nchi hii yenye utajiri mkubwa wa mali asili wanavyozidi kudidimia katika umasikini.

Baadhi ya watendaji hawa wamekuwa wanaachiwa kuendelea kuwa madarakani, pamoja na utendaji wao mbovu na ufisadi, hali ambayo baadhi yao wamejijengea ka ujeuri ka hata kuwatukana Watanzania. Kuna waziri mmoja wa Kikwete, aliyemrithi kutoka utawala wa Awamu ya Tatu – bila shaka kwa sababu za muafaka – aliyewahi kutamka kuwa wananchi tutake tusitake, na hata ikibidi kula majani, ndege ya Rais itanunuliwa tu.

Na hakika Watanzania wengi sasa wanakula majani – kwani ni wachache sana miongoni mwetu wanaimudu bei ya nyama kwenye mabucha. Kilo moja ya nyama si chini ya Sh 3,000/- jijini hapa ambayo kwa mwezi ni Sh 90,000/- kiwango cha kima cha chini cha mshahara ambacho hadi leo serikali yenyewe inavutana mashati na wafanyakazi wake katika kuwalipa. Biashara ya mboga za majani hapa Jijini kwa mfano imekuwa inaongezeka maradufu hivi sasa.

Tuhuma za sasa zilizotolewa na gazeti hili dhidi ya Dr Rashid ni rasharasha tu, dhoruba yenyewe ilishatokea zamani. Watanzania ni mojawapo ya jamii sahaulifu sana hapa duniani kama siyo linaloongoza. Inawezekana ni kwa sababu, kama nilivyotaja ya ugumu wa maisha, hali inayowakabili kila siku kwamba hawana muda wa kukumbuka yaliyotokea – kwani wao daima huwa mbele kwa mbele kujitafutia kuishi.

Kusahau mambo kuna uzuri wake na ubaya wake – uzuri ni kwamba hatuweki kinyongo katika jambo, matukio fulani au kwa watu wengine -- hali ambayo ingeweza kuendeleza farakano. Ubaya wa kusahau ni kwamba kunatufanya kushindwa kabisa kujifunza kutokana na matukio ya nyuma yaliyopita hali inayotufanya kushindwa kuchukuwa tahadhari katika yale yajayo……………


………………Kashfa ya kuanguka kwa benki ya Meridien BIAO haikukuwa kashfa pekee kwa Dr Rashid akiwa Gavana wa Benki Kuu. Mwishoni mwa mwaka 1994, rais Mwinyi alifanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri kwa kumteua Jakaya Kikwete kuwa Waziri wa Fedha, na kumuondoa Kigoma Malima (sasa marehemu). Mchakato mzima wa ufilisi wa Meridien BIAO kwenda kwa benki nyingine ya kigeni – Stanbic Bank ulifanywa chini ya usimamizi wa Kikwete na Dr Rashid na inasemekana haukuwa wa wazi kabisa. Kulitokea minon'gono kwamba milungula ilitembea.

Pili, wakati akiwa bado Gavana wa Benki Kuu, Dr Rashid alishinikiza serikali kubadilisha kampuni ya uchapaji wa noti zetu kutoka kampuni ya zamani ya Uingereza ya Thomas de la Rue na kuingia mkataba na kampuni ya Giesecke & Devrient ya Ujerumani. Kampuni hiyo ya Uingereza imefanya biashara na Benki Kuu ya Tanzania kuanzia 1966 hadi 1996. Sababu za kubadilisha kampuni ya uchapaji wa sarafu hazikuwekwa sawa kwani wengi wanaona kuwa hii ya Ujerumani inachapa noti zisizo na ubora kama ilivyokuwa zamani, zinachakaa haraka sana.

Mapungufu haya, pamoja na ripoti katika gazeti la The East African la Agosti 13, 2001, kwamba mapema mwaka huo, 2001 Benki Kuu ililazimika kuziondoa katika mzunguko mamilioni ya noti za Sh 1,000/- kutokana na kuchapishwa vibaya na mchapishaji huyo, bado Dr Rashid aliendelea kuishinikiza serikali kufanya biashara na kampuni hiyo ya Ujerumani. Katika mwaka 1994 pekee, kampuni hiyo ilichapisha vibaya noti za Tanzania mara nne. Hizi ni zile za viwango vya Sh 500/-, 1,000/- na 10,000/-.

Aidha gazeti hilo liliripoti kwamba kampuni hiyo ya Ujerumani pia ilikuwa imekataliwa kuchapisha noti za Benki ya Umoja wa Ulaya (European Central Bank) baada ya kuchapa vibaya noti za Euro za thamani ya mabilioni katika tenda iliyokuwa na thamani ya Dola za Kimarekani milioni 32.

Ilielezwa kuwa katika zabuni hiyo ya mwaka 2001, wakati kampuni ya Thomas de la Rue ilikubali kuchapisha noti zetu kwa thamani ya Dola za Kimarekani 33.02 milioni, kampuni hiyo ya Ujerumani ilitaka ilipwe Dola 49.15 milioni. Hata hivyo hatimaye Wajerumani walishinda kunyakuwa zabuni hiyo.

Chanzo Mwanahalisi
 
Namimi nimesugua, rangi kwa kwenda mbele! Haya cha juu kulipia madeni ya helcopta za kampeni
 
Wakuu nilieleza hii issue ya hizi noti kabla hata hazijaingia kwenye mzunguko kuwa ni kimeo, watu wakanishambulia hapa jukwaani sana na kusema sijui technolojia ya kisasa. Mmesahau kujaribu kuchana kidogo mwone nini kitatokea.
Nadhani huo ulikuwa ni utabiri tu na wala si utafiti wa kisayansi
 
Nasikia kwa mbali ngurumo ya dhoruba kubwa inayokuja. My instincts tell me kwamba hii itaifanya Dowans kuwa cha mtoto! Ngojeni tu!!!!!!!
 

………………kashfa ya kuanguka kwa benki ya meridien biao haikukuwa kashfa pekee kwa dr rashid akiwa gavana wa benki kuu. Mwishoni mwa mwaka 1994, rais mwinyi alifanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri kwa kumteua jakaya kikwete kuwa waziri wa fedha, na kumuondoa kigoma malima (sasa marehemu). Mchakato mzima wa ufilisi wa meridien biao kwenda kwa benki nyingine ya kigeni – stanbic bank ulifanywa chini ya usimamizi wa kikwete na dr rashid na inasemekana haukuwa wa wazi kabisa. Kulitokea minon'gono kwamba milungula ilitembea.

Pili, wakati akiwa bado gavana wa benki kuu, dr rashid alishinikiza serikali kubadilisha kampuni ya uchapaji wa noti zetu kutoka kampuni ya zamani ya uingereza ya thomas de la rue na kuingia mkataba na kampuni ya giesecke & devrient ya ujerumani. Kampuni hiyo ya uingereza imefanya biashara na benki kuu ya tanzania kuanzia 1966 hadi 1996. Sababu za kubadilisha kampuni ya uchapaji wa sarafu hazikuwekwa sawa kwani wengi wanaona kuwa hii ya ujerumani inachapa noti zisizo na ubora kama ilivyokuwa zamani, zinachakaa haraka sana.

Mapungufu haya, pamoja na ripoti katika gazeti la the east african la agosti 13, 2001, kwamba mapema mwaka huo, 2001 benki kuu ililazimika kuziondoa katika mzunguko mamilioni ya noti za sh 1,000/- kutokana na kuchapishwa vibaya na mchapishaji huyo, bado dr rashid aliendelea kuishinikiza serikali kufanya biashara na kampuni hiyo ya ujerumani. Katika mwaka 1994 pekee, kampuni hiyo ilichapisha vibaya noti za tanzania mara nne. Hizi ni zile za viwango vya sh 500/-, 1,000/- na 10,000/-.

Aidha gazeti hilo liliripoti kwamba kampuni hiyo ya ujerumani pia ilikuwa imekataliwa kuchapisha noti za benki ya umoja wa ulaya (european central bank) baada ya kuchapa vibaya noti za euro za thamani ya mabilioni katika tenda iliyokuwa na thamani ya dola za kimarekani milioni 32.

Ilielezwa kuwa katika zabuni hiyo ya mwaka 2001, wakati kampuni ya thomas de la rue ilikubali kuchapisha noti zetu kwa thamani ya dola za kimarekani 33.02 milioni, kampuni hiyo ya ujerumani ilitaka ilipwe dola 49.15 milioni. Hata hivyo hatimaye wajerumani walishinda kunyakuwa zabuni hiyo.

chanzo mwanahalisi

makubwa haya
 
Kama rais ni msanii na wasaidizi aliowachagua wanamsaidia kuendeleza usanii kwa ari mpya..nguvu mpya na kasi zaidi mnategemea nini zaidi ya muendelezo wa usanii kutoka mmoja kwenda mwingine!?Kwenye usanii ndipo tulipopiga hatua!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom