Nombeni mnishauri nifanyeje


Achana nae punguza visits! mtumie hela inapobidi, thats all
 
Pole dada yangu hapo kwa jinsi nilivyoona utalaumu mama,mume na hautapata majibu katika ali ya kibanadamu,mm nnacho ona kuna supirit of rejection inakutesa tafuta makanisa ya kiroho kwa jina la yesu itatoka coz umekataliwa na mume na wazazi pia
A.K.A jini mikosi, nuksi......wabongo huwa tunakimbilia huku mapema sana...kwa staili itabidi umtafute ustaadh Michael ......mtaalamu wa Diamond akupatie jini mvuto.......utani tu!
 



kweli kabisa ,zingatia haya.
 
Mama yako ana-roho mtaka vitu

Pole sana my dear, endelea kumuomba Mungu naamini atakuonesha malango wa kutokea. Huyu mama maybe ana pepo la hela, nyumba 5, bado anakusumbua na umejenga kwa pesa yako

NI mama yangu kabisaaaaaa, na ni msomi mzuri na ana nyumba Tano hapa Dar, na kapangisha zote, Lakini sijui ni nn kwa kweli, niombeeni, maana nimeanza kufunga na kusali ili Mungu anionyeshe ni nn kipo ndani yake.
 
Haya nayo maneno mamtoto.......

 
hata mimi naona ni bora aachane na huyo mama yake akaanze upya ni maisha tu
 

Huna sababu ya kujiua na kuua watoto wako. unatakiwa kujua neno moja tu, mara unapofanikiwa, maadui huongezeka hata wake usiowatarajia. cha msingi cha kufanya tafuta kiwanja sehemu nyingine, ukishapata nunua na anza mchakato wa kujenga nyumba ya kuishi kwanza. ukishamaliza, kama hizo nyumba hujapiga plasta mpaka nje, ukimtafuta fundi anaweza kutoa tofali vizuri na ukatumia kujenga kitegauchumi kingine katika kiwanja chako utakachonunua. Itafaa pia umjulishe hilo baba yako ili asije akapata tafsiri potofu juu yako.

kumbuka mtegemea nduguye hufa maskini

usiogope huo ni mwanzo wa kuwa na mahali pako penye amani ya muda mrefu
 
Hayo makanisa yenyewe laana tupu hata wachungaji wenyewe laana mshauri lingine.

usipende ku-generalize eti makanisa na wachungaji ni laana tupu otherwise unatafuta HASIRA YA MUNGU! maana naona unafika mbali ktk comment yako! Take care my dear!!!
 
usipende ku-generalize eti makanisa na wachungaji ni laana tupu otherwise unatafuta HASIRA YA MUNGU! maana naona unafika mbali ktk comment yako! Take care my dear!!!

Wewe ni nani mbele ya MUNGU kwani hujui siku hizi hayo makanisa yenu yanawachukulia sh 500 za walalahoi kwa kutumia jina la Yesu?
kuna wachungaji ni zaidi ya mafisadi kwa vitendo vyao hao ndo ninaowazungumzia.
Sijamanisha nimejenerize ila nawafocus hao wakiana kakobe types na utapeli wao kwa kutumia jina la Yesu.So kamanda tuliza munkali hatupo kwenye vita hapa.
 

Pole sana rafiki kwa wakati mgumu ulionao.

Kujiua au kukatiza maisha si sulihisho la kudumu au muafaka wa tatizo lako. Jaribu kuwafikiria watoto wako wa 4,utakapokatiza maisha huku nyuma hali itakuwaje? Km uko hai mama yako ameanza kuwabagua, ukifa si ndo itakuwa werse.

Cha kufanya, changanya akili haraka haraka but kwa siri kubwa. Wakati huu kabla mama hajakufukuza, maana ndo kunakoelekea,Kodi unayochukua nunua kiwanja, jenga hata vyumba viwili (km possiblity ipo, ikitegemea na gharama za ujenzi za mahali ulipo) then hama.

Au sbbu nyumba umejenga wewe, na hati za nyumba unazo, nenda katafute nsaada wa kisheria, km umejenga nyumba kwenye viwanja vya ukoo, sheria inasemaje ili ujue mbivu na mbichi.

Japo umefanya kosa kubwa sana kujenga kwenye viwanja vya kifamilia, but usithubutu kukatiza maisha hata siku moja.Chukulia hli jaribu kama changamoto ya maisha inayohitaji kutafutiwa ufumbuzi.

Remember una watoto wanaokupenda sana na wanaokur=tegemea pia.
 
Mhhhh! Pole sana bi dada. Huyo mama yako ana roho mbaya sana na ameweka mbele tamaa ya pesa kuliko watoto wake na wajukuu zake. Hata sijui nikushauri nini maana kama title deeds zinaonyesha majina yake basi huna haki ya kudai chochote hapo. Pole sana maana maisha ya kupanga nayo nyanyaso yako si ya kawaida.
 

Rudia kusoma comment yako ya awali then soma comment yangu ya awali kuhusu comment yako ya awali. Utaona wazi kuwa uli-generalize kuwa makanisa na wachungaji ni laana! Ndio maana nikakwambia usitafute hasira ya Mungu, chechezea mambo yooote ya kibinadamu lakini sio kazi ya Mungu! Kwa comment yako ya awali it is as if una-support hata uchomaji wa makanisa na mauaji ya viongozi wa madhehebu ya kikiristo maana ni laana. Lastly, sina vita na wewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…