This is a very poor way of using your brain for thinking.
Kama ndivyo unaamini ufikiri wako huo uko timamu maana yake kama chadema ingeshinda huo urais mwaka 2015, wale wote waliokipigia debe chadema kishinde, chama hicho kingewalinda katika uharifu wo wote watakoufanya, ikiwamo kufanya biashara ya madawa ya kulevya, biashara ya meno ya tembo, ujambazi, uzinzi, ulawiti, kutokulipa kodi n.k. Kisa: 'Ni wenzetu hawa maana ndiyo walituwezesha kushinda urais, hawatakiwi kusoma namba'.
Maana yake pia ni kwamba chadema ingeshinda, uharifu nchini ungeongezeka sana. Na waharifu wakijua kuwa kukipigia debe chama cha siasa kushinda urais ni kujipatia kinga dhidi ya mkondo wa sheria kwa uharifu walioufanya na watakaoendelea kuufanya, basi wapiga kampeni za chaguzi hizo karibu wote wangekuwa waharifu sugu.