Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Nimepeleka cheki yangu NMB, aliyenilipa ana akaunti Barclays. Zimepita wiki 2 salio halisomeki. Haimaye nimeenda kuulizia wakabofya kompyuta na kuniambia kuwa nina elfu kumi tu kwenye akaunti. Nikauliza sasa elfu kumi na cheki yangu vina uhusiano gani? Wakanijibu lazima niwe na zaidi ya elfu kumi na tano kwa sababu gharama ya kuingiza cheki toka benki nyingine ni 15,000. Nikauliza mbona hawakuniambia jambo hilo wakati ninawakabidhi, wakaniambia 'pole'. Nikawajulisha kuwa, mbona CRDB huwa napeleka cheki ya benki nyingine na kupata kiasi kamili cha pesa, wakasema kama vipi wanirudishie cheki yangu. Nikakubali. Kuipokea ina mihuri yao nyuma na mbele - HII SI SAWA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!