FDLR wahusike vipi na wameshasambaratishwa? Kagame na extremists wenzake huwa hawataki kusema idadi kamili ya interahamwe ni ngapi, idadi ya FDLR ni ngapi. Ukienda Rwanda utakuta malaki ya wahutu wamefungwa kwa kisingizio cha kwamba walikuwa interahamwe. Lakini ukiangalia idadi yao ni kubwa mno kupita kiasi, its impossible kuwa na interahamwe wote wale. Mfano CCM yote ina wanachama hawazidi mil 5, huwezi ukawa na UVCCM ndani ya CCM hiyo hiyo yenye watu mil10! Obviously hao sio wanachama wa UVCCM wala CCM yenyewe.
Kagame alikuwa muasi, vijana wazalendo hawakutaka apindue nchi, hivyo wakaingia mtaani kupigana na RPF kama wazalendo wengine tu, hilo halikuwafanya wawe nao interahamwe.
Hivyo ukisikia mtu anaitwa interahamwe ujue kwa kifupi ni adui tu wa kagame na sio interahamwe wa kweli. Idadi ya wahutu ambao kagame kawafunga akidai ndio interahamwe imeshazidi interahamwe yenyewe mara dufu!
Ukija FDLR ni hivyo hivyo tu. UN iko pale DRC kwa miaka mingapi? Hivi inawezekanaje eti waingie waburundi wa Imbonerakure waendeshe kambi za mafunzo na FDLR chini ya uangalizi wote huo wa jumuiya ya kimataifa? Wanapitia wapi? Na kwa nini taarifa za FDLR/interahamwe/imbonerakure huwa ni kagame tu ndio mwenye nazo na hutazipata sehemu nyingine yoyote ile? Hizi ni propaganda tu, shida ya huyo bwana ni kabila la Nkurunzinza sio vinginevyo.