Njia za uzazi wa mpango

Njia za uzazi wa mpango

Demu wangu aliwahi kuchoma sindano ya miaka miwili aisee nilisota maana kwa mwezi naweza nikawa nyapu mara tatu au ukapita hola kabisa , hatukufika mbali tulibwagana
Upwiru unaleta hasira
 
Njia mbadala hizi hapa km hutaki sindano,kijiti,
1. IUCD ya copper (Copper T)
- Haina homoni.
- Inawekwa kwenye mfuko wa uzazi na huzuia mimba hadi miaka 10.
- Baadhi hupata hedhi nzito mwanzoni, lakini ni salama kwa wengi.

2. Diaphragm au cervical cap
- Inawekwa ukeni kabla ya tendo la ndoa.
- Huzuia mbegu kuingia kwenye mji wa mimba.
- Haitumiki sana Tanzania lakini ipo.

3. kondomu za kike (female condoms)
- Hutoa ulinzi kama kondomu za kiume.
- Pia huzuia maambukizi.

Njia sahihi inategemea afya, mahitaji, na maisha yako Kwa ujumla wewe na mwenza wako!
 
Back
Top Bottom