BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Nizar Khalfan aitwa Tottenham
Imeandikwa na Anatazia Anyimike; Tarehe: 13th May 2009 @ 10:37
Imeandikwa na Anatazia Anyimike; Tarehe: 13th May 2009 @ 10:37
KIUNGO mahiri wa timu ya soka ya taifa Taifa Stars, Nizar Khalfan ameitwa na timu ya Ligi Kuu ya England, Tottenham Hotspurs kwa ajili ya kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotumwa na Mkurugenzi Mkuu wa Moro United, ambayo mchezaji huyo anachezea, Azim Dewji jana, ilieleza kuwa Nizar mwenye umri wa miaka 21, anatarajia kuondoka mwishoni wa mwezi huu, tayari kwa majaribio yatakayoanza Juni mosi chini ya kocha Harry Redknapp.
Tumefurahishwa na mwaliko wa Tottenham iliyoahidi kutoa nafasi zaidi kwa wachezaji wa Kitanzania kujaribiwa. Ni bahati na heshima ya pekee kwa klabu kama Moro United na Tanzania kupata nafasi hii. Wametuahidi hawataishia kwa Nizar, bali watashirikiana nasi kutoa nafasi ya mara kwa mara kwa wachezaji wetu.
''Nasi kwa kuwa lengo letu ni kuona nchi hii inavuka milima na mabonde ya mafanikio katika soka, hatutaichezea bahati hii,'' ilisema taarifa hiyo ya Dewji. Taarifa ilieleza kuwa moja ya mikakati ya Moro United ni kusajili wachezaji wengi wenye umri mdogo, ili wakulie mikononi mwao wakiamini wataweza kufundishika na kuwa rahisi kuwapeleka katika klabu za Ulaya na kwingineko.
Tottenham ni moja ya timu maarufu zinazocheza Ligi Kuu England na imewahi kutamba na nyota kadhaa kama Gary Lineker, Teddy Sheringham, Paul Gascoigne `Gaza, Jurgen Klinsmann, Sol Campbell na Dimirtar Berbatov.
Kama akifanikiwa kupata nafasi katika timu hiyo itakuwa bahati ya pekee, maana Tottenham ni moja ya timu za juu zinazoshiriki Ligi ya England, ambazo hazioni tabu kutoa fedha nyingi kununua wachezaji nyota na wenye uwezo.
Baadhi ya nyota ambao inao hivi sasa, wengine wakiwa wamerudi tena baada ya kwenda katika baadhi ya timu maarufu barani Ulaya ni Robbie Keane, Ledley King, Jermain Defoe, Darren Bent, Aaron Lennon, Didier Zokora, Carlo Cudicini na Pascal Chimbonda.
Hiyo itakuwa mara ya pili katika kipindi kisichozidi miezi miwili kwa mchezaji wa Tanzania kwenda kufanya majaribio kwa timu inayoshiriki Ligi Kuu ya England, baada ya mwezi uliopita mshambuliaji wa Taifa Stars na Yanga ya Dar es Salaam, Mrisho Ngassa kwenda kufanya majaribio katika timu ya West Ham United, ingawa hakufanikiwa, badala yake imeelezwa anatakiwa aende tena mwezi Julai.
Nizar ambaye timu yake ya Moro United ilinusurika kushuka daraja, ikiwa ndiyo ya mwisho baada ya timu tatu zilizoshuka daraja katika Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika mwezi uliopita, alingara katika fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) zilizofanyika Ivory Coast mapema mwaka huu.