FT: Yanga SC 3-0 TRA United| Ligi kuu NBC | KMC Complex

FT: Yanga SC 3-0 TRA United| Ligi kuu NBC | KMC Complex

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,925
Reaction score
6,574
Yanga wanashuka dimbani muda huu kucheza mchezo wake wa ligi kuu NBC dhidi ya TRA.

Moja ya mchezo mzuri na muhimu kwa Yanga kujihakikishia ubingwa

Lakini pia hata TRA nao wanataka kumaliza top 4
===========
Klabu ya Yanga imeendelea kuonyesha ubora wake katika Ligi Kuu ya NBC baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya TRA United katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa KMC Complex.

Nyota wa mchezo alikuwa Allan Okello aliyefunga mabao yote matatu (hat-trick), na kuihakikishia Yanga pointi tatu muhimu huku ikiendeleza rekodi yake nzuri katika mbio za ubingwa wa ligi msimu huu. Ushindi huo unaendelea kuifanya Yanga kuwa miongoni mwa timu zinazoonyesha kiwango bora katika ligi.
 
Watanganyika wengi mzuka wa kushabikia mpira umeshuka kwa kiwango cha kuhuzunisha. Ingekuwa kabla ya mauaji ya Oktoba 29, hadi muda huu uzi ungekuwa umejaa comments za mashabiki.

All in all, naitakia Yanga ushindi. Kwa sababu wakifanya tu uzembe wa kudondosha point kama kwenye ile mechi na Dodoma Jiji, simba wanawavua ubingwa.
 
Uzi una comments 12. Kweli maisha yanabadilika
Siku watayovaa vitambaa vyeusi wakasimama dakika moja ya maombelezo kuwakumbuka Watanzania na mashabiki wao waliopoteza maisha October 29 kuna mambo yatarejea.
 
Back
Top Bottom