Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,156
Serikali hii hii iliyokuwa ikiwalea na kuwaacha wamachinga wafanye watakavyo bila kuzingatia taratibu za miji, ndiyo hiyo hiyo imewafukuza na kuwavunjia vibanda vyao, bila kujali kuwa watafanya wapi shughuli zao.
Siyo siri kuwa ni serikali hii hii ya CCM ndiyo iliyowalea wamachinga na kuwafanya wengi mno, ambao wamekuwa wakijipangia bidhaa zao popote pale, hata mbele ya maduka yanayolipa kodi TRA, bila wao kulipa kodi yoyote!
Ambaye alikuwa mstari wa mbele, kuwakingia kifua wamachinga, alikuwa ni Hayati, Rais Magufuli.
Bado wengi tutaendelea kukumbuka maneno yake aliyokuwa akitoa kwenye hotuba zake mbalimbali, kuwa Hawa wamachinga, ndiyo wapiga kura wangu, kwa hiyo wasiguswe, hata kama shughuli zao wanazofanya, wanavunja sheria za nchi!
Sasa inashangaza kwa serikali hiyo hiyo inayongozwa na CCM, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, imekuja na msimamo tofauti, baada ya kufariki Rais Magufuli, kwa kuwaondoa kinyama wamachinga hao, bila kuwapangia sehemu nyingine za kufanya shughuli zao.
Matoleo yake ndiyo haya tunayoyaona kwa wamachinga hao kukaidi maagizo hayo ya serikali na kurejea kwenye maeneo yale yale na kuendelea na biashara zao!
Hii serikali ambayo haitoi ajira kwa mamilioni ya vijana wanaomaliza shule na vyuo mbalimbali, kila mwaka hapa nchini, hivi serikali inafikiri hao vijana watafanya nini, kama siyo kujitafutia Maisha kwa kuwa wamachinga??
Serikali hiyo hiyo ndiyo viongozi wake wanapokuwa kwenye majukwaa ya kisiasa, hawaishi kuhubiri kuwa vijana wasitegemee kuajiriwa na badala yake wajiajiri wao wenyewe.
Sasa Hawa vijana wanaotekeleza "maagizo" hayo ya viongozi wao, iweje leo waonekane kama wakosaji na kuadhibiwa kwa kuvunjiwa vibanda vyao vya kufanyia biashara??
Tutaendelea kuyakumbuka maneno ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, aliyesema kuwa suala la wamachinga wa nchi hii ni sawa na bomu, ambalo wakati wowote litaweza kulipuka na kutuletea maafa makubwa sisi wananchi wote wa nchi hii.
Watawala wetu nawaomba Sana muwe waangalifu Sana mnapolitafutia ufumbuzi suala hili "very sensitive and explosive" la wamachinga, ama sivyo halitatuacha salama, kwani tutatetekea wote, wamachinga na wasio wamachinga.
Ndiyo maana kwenye kichwa cha habari ya "story" yangu nimetamka kuwa watawala wetu kuwavunjia vibanda vyao wamachinga bila kwanza kuwatafutia maeneo mengine, ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu!
Siyo siri kuwa ni serikali hii hii ya CCM ndiyo iliyowalea wamachinga na kuwafanya wengi mno, ambao wamekuwa wakijipangia bidhaa zao popote pale, hata mbele ya maduka yanayolipa kodi TRA, bila wao kulipa kodi yoyote!
Ambaye alikuwa mstari wa mbele, kuwakingia kifua wamachinga, alikuwa ni Hayati, Rais Magufuli.
Bado wengi tutaendelea kukumbuka maneno yake aliyokuwa akitoa kwenye hotuba zake mbalimbali, kuwa Hawa wamachinga, ndiyo wapiga kura wangu, kwa hiyo wasiguswe, hata kama shughuli zao wanazofanya, wanavunja sheria za nchi!
Sasa inashangaza kwa serikali hiyo hiyo inayongozwa na CCM, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, imekuja na msimamo tofauti, baada ya kufariki Rais Magufuli, kwa kuwaondoa kinyama wamachinga hao, bila kuwapangia sehemu nyingine za kufanya shughuli zao.
Matoleo yake ndiyo haya tunayoyaona kwa wamachinga hao kukaidi maagizo hayo ya serikali na kurejea kwenye maeneo yale yale na kuendelea na biashara zao!
Hii serikali ambayo haitoi ajira kwa mamilioni ya vijana wanaomaliza shule na vyuo mbalimbali, kila mwaka hapa nchini, hivi serikali inafikiri hao vijana watafanya nini, kama siyo kujitafutia Maisha kwa kuwa wamachinga??
Serikali hiyo hiyo ndiyo viongozi wake wanapokuwa kwenye majukwaa ya kisiasa, hawaishi kuhubiri kuwa vijana wasitegemee kuajiriwa na badala yake wajiajiri wao wenyewe.
Sasa Hawa vijana wanaotekeleza "maagizo" hayo ya viongozi wao, iweje leo waonekane kama wakosaji na kuadhibiwa kwa kuvunjiwa vibanda vyao vya kufanyia biashara??
Tutaendelea kuyakumbuka maneno ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, aliyesema kuwa suala la wamachinga wa nchi hii ni sawa na bomu, ambalo wakati wowote litaweza kulipuka na kutuletea maafa makubwa sisi wananchi wote wa nchi hii.
Watawala wetu nawaomba Sana muwe waangalifu Sana mnapolitafutia ufumbuzi suala hili "very sensitive and explosive" la wamachinga, ama sivyo halitatuacha salama, kwani tutatetekea wote, wamachinga na wasio wamachinga.
Ndiyo maana kwenye kichwa cha habari ya "story" yangu nimetamka kuwa watawala wetu kuwavunjia vibanda vyao wamachinga bila kwanza kuwatafutia maeneo mengine, ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu!