Yanayotokea yanathibitisha Rais Samia hakuwahi kujiandaa kuwa Rais, ataliacha taifa pabaya kuliko alipolikuta

Dalton elijah

JF-Expert Member
Jul 19, 2022
207
453
Na Mwl, John Pambalu

Waswahili wanao msemo usemao kuwa, "Asiyejua aendako, njia yoyote itamfikisha anakokwenda". Ndiyo maneno mafupi ninayoweza kuyatumia kumuelezea Rais Samia ambaye mwanzoni alionyesha sura ya uungwana, udemokrasia na uadilifu lakini taratibu ameamua kuachana na mkondo huo na kulirejesha taifa kwenye mikono ya wahuni walioumiza watu katika taifa.

Mwanzoni mwa utawala wake alijitambulisha kwa falsafa ya 4R (reconciliation, resilience, reforms & rebuilding) akimaanisha Uputanishi, Ustahimilivu, Mabadiliko na Kujenga upya.

Kila Rais aliyejiandaa kuwa Rais alikuwa na falsafa yake ambayo aliitetea na kuipigania. Mwalimu aliamini kwenye ujamaa na kujitegemea, aliishi humo kwenye hiyo falsafa.

Mwinyi akaamini kwenye uhuru akatoa Ruksa ya watu kumiliki uchumi tofauti na ilivyokuwa wakati wa Mwalimu. Mkapa akaamini katika ujenzi wa taasisi akaanzisha karibuni taasisi zote mnazoziona. Mara TAKUKURU, TRA nk.

Kikwete akaamini katika Demokrasia, licha matukio kadhaa ya mashambulizi ya wakosoaji wa serikali kama mauaji ya Ally Zona, Daud Mwangosy nk, lakini angalau chaguzi za wakati wa Jakaya zilikuwa nzuri ukilinganisha na za wengine. Magufuli aliamini katika ujenzi wa vitu, kaacha vitu chungu mbovu mara Bwawa la Nyerere, Treni ya Mwendokasi nk.

Sasa ukiondoa kuuza bandari, kuwanyanyasa Wamachinga kwa kuwavunjia mali zao na kuwaumiza Wamasai na kuwanyan'ganya ardhi ambayo ni urithi wa vizazi vyao unafikiri liko jambo lipi jema Rais Samia atakumbukwa kwalo?

Awali yeye mwenyewe alisema anataka akumbukwe kwa 4R, yaani Upatanisho, Ustahimilivu, Mabadiliko na Kujenga upya. Awali alisema anawaondoa wahuni waliosababishia watu mateso na anakutana na wapinzani walioumizwa zaidi ili wazungumze kuhusu kulipatanisha taifa. Gafla akauacha huo mkondo na akaanza kuwapa nafasi za juu wakina Ramadhan Kingai, Biswalo na jana wakina Makonda.

Kwenye eneo la Ustahimilivu unagundua yeye Rais mwenyewe hana hata huo uwezo wa kustahimili ukosoaji. alikosolewa na Mhe. Mbowe akamtupa Segerea zaidi ya miezi 8, akakosolewa na Mwabukusi. Dr. Slaa na Mdude, wakatengenezewa kesi ya uhaini.

Sasa tunashuhudia attempts za wahuni kuja kuvuruga mikutano ya CHADEMA kule Mwanza na Tunduma. Tunarudi kule kule ambako washenzi walitupa mabomu na kuua watu kwenye mkutano wa CHADEMA Arusha.

Kwenye eneo Mabadiliko, alivyozungumzia tu mabadiliko. watu wakajua anamaanisha kubadili sheria kandamizi na kuleta katiba mpya, mwisho akaishia kusema katiba ni kitabu tu. Hatuandiki Katiba mpya ila watu wajifunze ile ya 1977 kwa kipindi cha miaka 3 kama wanatafuta bachelor ya Katiba.

Kwa kifupi Rais Samia hana anachokifanya ambacho kama angejiandaa kuwa Rais angeanza nacho kutokana na shauku ya kutaka kuwa Rais.

Amekuwa Rais kwa nasibu, anaendesha serikali yake kwa nasibu na ataliacha taifa kwa nasibu ikiwa poa, isipokuwa poa tu ilimradi yeye na wanae wanakula na kuishi kama wako paradise huku mamilioni ya Watanzania wakitokomea katika lindi la umasikini.

Rai yangu kwa Watanzania, taifa hupiganiwa na mabadiliko hayaji tu bali kwa mapambano yenye kujitoa sadaka kwa ajili ya maslahi ya wengi. Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa vijana kuwa, "Tunataka kuona katika Taifa hili vijana jeuri na wenye kujiamini; si vijana waoga akina "Ndiyo bwana mkubwa", vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga vita mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa".

Wasalaam,
John Pambalu,
Mwanza-Tanzania.
jpambalu@gmail.com
23.10.2023
1698062766311.jpg
 
Kwanza kwa namna ulivyo andika inaonyesha wazi kuwa wewe ni mtu uliyekosa adabu,heshima,staha na malezi mazuri kutoka kwa mama yako mzazi pamoja na baba yako au ulikosa malezi ya wote wawili baba na mama yako na kujikuta ukijikulia tu kama kifaranga kilicho telekezwa au una laana ya mama yako inayokuandama.

Hivi unaanzia wapi kusema Rais samia hana uvumilivu dhidi ya ukosoaji? Angekuwa hana uvumilivu ungeandika haya uliyoandika hapa jukwaani? Mngekuwa mnakuwa na nafasi ya kuropoka matusi mnayoropoka majukwaani kwenu? Angepata nafasi ya kupanda majukwaani kama siyo Rais samia? Unaposema habari za akina Slaa sijuwi Mdude na Mwabukusi napo nakushangaa sana.hivi wanachofanya na ambacho wamekuwa wakifanya hao wahuni ni ukosoaji au utukanaji wa matusi? Tangia lini matusi yakawa ukosoaji? Tangia lini matusi na udhalilishaji ukaitwa ukosoaji? Hayo ndio unataka yavumiliwe? Ndivyo mnavyofundishwa huko chamani kwenu? Matusi wanayotoaga hao Watu unaweza kumtolea mama yako mzazi aliyekubeba Tumboni mwake miezi tisa na kukuzaa kwa uchungu pamoja na kukunyonyesha? Ndio adabu yako hiyo? Ndio muelekeo wa chama chako? Wapi duniani kunakokubalika matusi na udhalilishaji kwa wengine kwa kigezo cha demokrasia?

Unaposema hakuna maridhiano.napo nakuona kama una pombe kichwani mwako.hivi kusingekuwa na maridhiano mngeanzia wapi kupanda majukwaani? Hiyo nafasi mngeipata wapi? Hamkukaa miaka mitano bila kupanda majukwaani? Mlifanya nini? Nchi haikusonga? Kama siyo Rais samia wakina lema na Lissu wangeanzia wapi kuleta pua na miguu yao hapa nchini? Wewe ungepanda majukwaani? Mbona hukuwa ukipanda kabla ya hapo? Kwanini usutambue ni juhudi za Rais samia kutaka tujenge Taifa kwa pamoja na kutoa nafasi kwa watu kuzungumza ya moyoni na kuishi nchini pasipo hofu wala wasiwasi?

Rais samia angekuwa hana maono au Dira au malengo au kujuwa tunaakopaswa kwenda na kuwa unafikiri tungeweza vipi kupaa kiuchumi zaidi ya nchi za kenya na Uganda kwa umoja wake? Tungeweza vipi kudhibiti mfumuko wa bei kama vile mafuta ambayo kwa sasa kwa kenya yapo juu zaidi ya Tanzania? Tungeweza vipi kuhakikisha kuwa Taifa linajitosheleza kwa chakula na kuondokana na njaa? Tungeweza vipi kupandisha mapato ya serikali mpaka Trilioni mbili kwa mwezi? Kuvutia maelfu ya watalii, wawekezaji na wafanyabishara wakubwa kutoka kila kona ya Taifa letu?

Rais samia angeweza vipi kuboresha Secta za afya kwa kutiririsha zaidi ya Trilioni Sita ndani ya muda mfupi,kujenga vituo vya afya na zahanati pamoja na kiakili nguvu kazi ya kutosha kuwahudumia wananchi? Rais wetu angeweza vipi kuajiri maelfu ya vijana katika kada mbalimbali kama asingekuwa na maono na Dira yakutaka kuona baada ya miaka michache ijayo tutengeneze kila kitu na kufanya kila kitu kwa kutumia wasomi wetu tuliozalisha nakusomesha wenyewe hapa nchini? Angeweza vipi kujenga miundombinu nakukamilisha miradi ya kimkakati itakayo tupa faida kwa miaka mingi ijayo kama ilivyo kwa bwawa la mwalimu Nyerere ambalo mpaka sasa lipo 92% na litatupatia mega watti 2115? Kuzalisha ajira maelfu kwa maelfu?

Suala la watendaji au wateule .nalo hapa naona unaumwa ukichaa.utaanzaje kutupangia CCM watu au Viongozi wetu.ninj kinakuwasha na kukuuma? Kwani wanakuja kufanya kazi kwenye Sacco's yenu hiyo? Kwanini mpate hofu na kupata uwendawazimu kiasi hicho kama siyo hofu ya kutambua uwezo mkubwa wa viongozi wetu?

Kaa kwa kutulia na uwe na adabu maana ulisha zoea kuropoka ropoka kama vutabangi na jitu lenye laana ya mama yake .
 
Na Mwl, John Pambalu

Waswahili wanao msemo usemao kuwa, "Asiyejua aendako, njia yoyote itamfikisha anakokwenda". Ndiyo maneno mafupi ninayoweza kuyatumia kumuelezea Rais Samia ambaye mwanzoni alionyesha sura ya uungwana, udemokrasia na uadilifu lakini taratibu ameamua kuachana na mkondo huo na kulirejesha taifa kwenye mikono ya wahuni walioumiza watu katika taifa.

Mwanzoni mwa utawala wake alijitambulisha kwa falsafa ya 4R (reconciliation, resilience, reforms & rebuilding) akimaanisha Uputanishi, Ustahimilivu, Mabadiliko na Kujenga upya.

Kila Rais aliyejiandaa kuwa Rais alikuwa na falsafa yake ambayo aliitetea na kuipigania. Mwalimu aliamini kwenye ujamaa na kujitegemea, aliishi humo kwenye hiyo falsafa.

Mwinyi akaamini kwenye uhuru akatoa Ruksa ya watu kumiliki uchumi tofauti na ilivyokuwa wakati wa Mwalimu. Mkapa akaamini katika ujenzi wa taasisi akaanzisha karibuni taasisi zote mnazoziona. Mara TAKUKURU, TRA nk.

Kikwete akaamini katika Demokrasia, licha matukio kadhaa ya mashambulizi ya wakosoaji wa serikali kama mauaji ya Ally Zona, Daud Mwangosy nk, lakini angalau chaguzi za wakati wa Jakaya zilikuwa nzuri ukilinganisha na za wengine. Magufuli aliamini katika ujenzi wa vitu, kaacha vitu chungu mbovu mara Bwawa la Nyerere, Treni ya Mwendokasi nk.

Sasa ukiondoa kuuza bandari, kuwanyanyasa Wamachinga kwa kuwavunjia mali zao na kuwaumiza Wamasai na kuwanyan'ganya ardhi ambayo ni urithi wa vizazi vyao unafikiri liko jambo lipi jema Rais Samia atakumbukwa kwalo?

Awali yeye mwenyewe alisema anataka akumbukwe kwa 4R, yaani Upatanisho, Ustahimilivu, Mabadiliko na Kujenga upya. Awali alisema anawaondoa wahuni waliosababishia watu mateso na anakutana na wapinzani walioumizwa zaidi ili wazungumze kuhusu kulipatanisha taifa. Gafla akauacha huo mkondo na akaanza kuwapa nafasi za juu wakina Ramadhan Kingai, Biswalo na jana wakina Makonda.

Kwenye eneo la Ustahimilivu unagundua yeye Rais mwenyewe hana hata huo uwezo wa kustahimili ukosoaji. alikosolewa na Mhe. Mbowe akamtupa Segerea zaidi ya miezi 8, akakosolewa na Mwabukusi. Dr. Slaa na Mdude, wakatengenezewa kesi ya uhaini.

Sasa tunashuhudia attempts za wahuni kuja kuvuruga mikutano ya CHADEMA kule Mwanza na Tunduma. Tunarudi kule kule ambako washenzi walitupa mabomu na kuua watu kwenye mkutano wa CHADEMA Arusha.

Kwenye eneo Mabadiliko, alivyozungumzia tu mabadiliko. watu wakajua anamaanisha kubadili sheria kandamizi na kuleta katiba mpya, mwisho akaishia kusema katiba ni kitabu tu. Hatuandiki Katiba mpya ila watu wajifunze ile ya 1977 kwa kipindi cha miaka 3 kama wanatafuta bachelor ya Katiba.

Kwa kifupi Rais Samia hana anachokifanya ambacho kama angejiandaa kuwa Rais angeanza nacho kutokana na shauku ya kutaka kuwa Rais.

Amekuwa Rais kwa nasibu, anaendesha serikali yake kwa nasibu na ataliacha taifa kwa nasibu ikiwa poa, isipokuwa poa tu ilimradi yeye na wanae wanakula na kuishi kama wako paradise huku mamilioni ya Watanzania wakitokomea katika lindi la umasikini.

Rai yangu kwa Watanzania, taifa hupiganiwa na mabadiliko hayaji tu bali kwa mapambano yenye kujitoa sadaka kwa ajili ya maslahi ya wengi. Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa vijana kuwa, "Tunataka kuona katika Taifa hili vijana jeuri na wenye kujiamini; si vijana waoga akina "Ndiyo bwana mkubwa", vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga vita mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa".

Wasalaam,
John Pambalu,
Mwanza-Tanzania.
jpambalu@gmail.com
23.10.2023View attachment 2790256
Hapa tulipo ndani ya miaka mitatu yake, taifa liko pazuri kuliko wakati wowote ule.


Kama huna macho basi hata masikio huna? Kama huna masikio basi hata akili huna?

kazi ya Mungu haina makosa.
 
Hapa tulipo ndani ya miaka mitatu yake, taifa liko pazuri kuliko wakati wowote ule.


Kama huna macho basi hata masikio huna? Kama huna masikio basi hata akili huna?

kazi ya Mungu haina makosa.
Umeme unakatika kila siku kwa muda wa masaa 16 au 18.
 
Yaani akili a watu wengine, ni matope kabisa.

Mtu anajiandaa Rais afe ili eye awe Rais?


CCM ima sera zake, ndizo zinazofatwa, kinachobadilika ni staili ya uongizi tu lakini siyo nini kinachotakiwa kifikiwe.


Hivi husikii siku zote? Sera, sera, sera...
 
Wahafidhina na Magufulist wamemtoa Samia kwenye 4R's zake na kumpeleka kusikojulikana.

Siasa za Chuki zinarejeshwa kwa kasi 5G Kinana nae kajiunga lini na UMagufulist?

Lakini wajue this time The Haig inawahusu.
 
Back
Top Bottom