Nivunje vipi haya mahusiano?

Nivunje vipi haya mahusiano?

Singasinga

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2011
Posts
2,741
Reaction score
3,316
Habari wakuu

Mwaka huu niliazimia kuwa na mahusiano rasmi ambayo kama Mola akibariki tufike kwenye kujenga familia maana mwakani nnafikisha miaka30


Kweli mwaka jana mwezi november nilifanikiwa kuanza mahusiano na binti mmoja wa mtaa wa pili ambae kiukweli nafsi yangu ilimkubali sana tangu siku ya kwanza namuona hadi leo hii tulipo.

Lakini changamoto ni kuwa siku chache baada ya kuanza mahusiano yetu dadangu wa damu alipata shida kubwa ya kifedha ambayo kama nisingeingilia kati kuokoa jahazi maisha yake yangeingia doa sana kama mjuavo mambo ya mikopo yalivo,kwa hiyo nikalazimika kumkopea bank kiasi ambacho itanilazimu nikae mwaka mzima ndo nirudi kwenye mstari.

Sasa dhumuni kuu la kuandika uzi huu ni kwamba kiasi cha fedha kinachobaki baada ya makato ni kidogo sana kiasi kwamba nashindwa hata kumhudumia mpenzi wangu huyu ambae hana ajira na kwao anaishi na mamake tu nae ni maisha ya chini tu hawezi mtimizia binti mahitaji yake.


So mpaka sasa anaonesha kunivumilia sana ingawa naona kabisa kuna namna mapenzi yetu yamefubaa na hata yeye ile moyo wa kujitoa sana kwangu dizaini umepungua na simlaum kwa hilo


Kwa hiyo wakuu binafsi inaniuma sana na sina amani kabisa kuendelea na haya mahusiano maana me nna asili ya kujali sana na najihisi vibaya kwamba hata 50k ya kubaki kumsaidia mpenz wangu kwa mwezi inashindikana.

Kingine tangu march 22 hajataka tena kukanyaga hom na tupo mitaa jirani,hii ina maana kwamba kaona ntafaidika sana japo kwenye msg mnapochati yuko happy tu na kuna wakati nlijaribu kumpotezea ikawa mwano kwamba labda lengo lilikua kumpata tu wakati ule.


Mwisho naombeni ushauri njia gani bora ya kumuacha huyu dada bila kumuumiza?


Samahani kwa uzi mrefu.
 
Pole Sana
Tulia Hali Yako Ndiyo Hiyo Kwa Kipindi Ulichosema
Muhimu Mweleze Ukweli Ingawa Changamoto Hapo Usije Kuchukua Maamuzi Mabaya
Inaweza Kukuketea Shida

Lakini Umeonyesha Kukata Tamaa
Akijitokeza Mtu Yoyote Mchumba Anaondoka, Simama Eneo Lako Ongea Naye Na Akishindwa Kukuvumilia Mwache Aende. Ingawa Kanuni Sasa Hivi Hakuna
Tuelekeza Nguvu Sana Kwenye Pesa
 
Jifunze kuwa Mwanaume kamili.....huu muda ambao unapitia changamoto za kifedha ndo muda mzuri wa kujua kuwa umepata mwanamke wa aina gani ndo wakati wa kupima mapenzi yake kwako kama atakuvumilia na kutokuonesha dalili za usaliti nakushauri huyo mweke ndani.

Unachotakiwa sasa hivi ni kumweleza mpenzi wako kuwa unachangamoto za kifedha hivyo kama atakuelewa na kukuvumilia mpk hapo hali yako itakapokuwa nzuri huyo ni mke.

Kingine na kushauri acha tabia za kugawa gawa pesa ovyo ukiamini ndo mwanamke atakupenda. Unaweza kumpa na yeye akawa anampelekea msela wake ambaye hana kitu lkn ndo hivyo demu kadata kwake, kwako nikukuchuna tu!

Kipindi unachopitia sasa kifedha kinakusaidia kujua type ya mwanamke uliyenaye

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko sahihi kabisa kaka,kiukweli kama yasingekua haya majanga yalontokea ningejibebea credit sana kwake ila sasa now ni Ile tu ilimradi hamjaachana

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kwanini ujisumbue...mweleze ukweli ya yaliyotokea uone kama atakaa avumilie au atakukimbia. Hata ukioa unafikiri utakuwa stable siku zote? Kuna siku utaishiwa.

Hapo umepewa nafasi ya kumpima...kama ameonyesha changes akiwa mke (kumbuka mke ana nguvu mkononi) hizo changes zitaonekana zaid ya zilivyo.

Kikubwa hakudai....useme ni deni utalipa...mwambie huna pesa kwasasa.
 
Sidhani kama kuvunja mahusiano ni sahihi, ni vyema kumuweka wazi kuwa unapitia kipindi kigumu kiuchumi, umeweka wazi mwanzo kuwa unataka ku-stick kwenye serious relationship nahisi huu ni mtihani kwako!!
 
Mpiganie Kama anaonyesha wazi upendo kwako. Lakin jaribu kumweka wazi juu ya kipato chako kuathirika pamoja mjadili Nini la kufanya ili kuokoa jahazi.

Pesa Ni maua tu Leo ipo kesho hakuna, inabidi maisha yaendelee



Sent using Jamii Forums mobile app
Najua haya ni maoni yako ila sio kesi tukiyajadili.


Umpiganie mtu kwasababu anaonyesha dalili za kukupenda tu?

Binafsi nampongeza mtoa mada...kumpigani dada yake ni jambo la kuigwa kuliko kuendelea kumpigania huyu mdada mwingine wanayeunganishwa na kaupendo tu ka sex ya kitandani.
 
Mkiachana wakati huu wa tabu then hamkuwahi kupendana.

Umekata tamaa...unahisi huyu dem ni mzigo.

Nakuonya tu. Ukimwacha itachukua muda mfupi sana kumkumbuka.

Keep holding into love.
 
Najua haya ni maoni yako ila sio kesi tukiyajadili.


Umpiganie mtu kwasababu anaonyesha dalili za kukupenda tu?

Binafsi nampongeza mtoa mada...kumpigani dada yake ni jambo la kuigwa kuliko kuendelea kumpigania huyu mdada mwingine wanayeunganishwa na kaupendo tu ka sex ya kitandani.
Dude! Are you in relationship!?

Hujawahi mpigania mpenzi wako!??
 
Back
Top Bottom