haswaaaaWajerumani walipokuja Tanganyika walijenga Ikulu Bagamoyo. baadaye wakajenga ikulu ndogo Dar. na ikulu kubwa sana Lushoto. Mahali pale walipaita WILHEMSTAL. wasambaa walishindwa kabisa kutamka neno hili geni wakakatisha wakaita USHOTO. wasambaa kwenye LU wana ondondoa L wanabaki na U. waswahili wakajua wasambaa wanakosea hivyo wakaunga ile L na mji wa shemeji zangu ukabatizwa jina na LUSHOTO
Karibuni wadau wa Jf uliza ujibiwe kuhusu wilaya ya Lushoto na maeneo yake. Hii ni moja ya wilaya nzuri kabisa ndani ya mkoa wa Tanga. Karibuni...
CC: mshana jr
hapo ndipo ulipokosea, wasambaa ni mchanganiko wa makabila mbali mbali waliosambaa katika milima ya usambara baada ya kuhama sehemu zao na kwenda usambaani kwenye ardhi yenye rutuba,
mwanzoni kabisa kabla ya milima ya usambara kuvamiwa na binadam, kulikuwa na msitu mkubwa uliosheheni kila aina ya wanyama na ndege wa kila namna, walikuwepo simba, tembo na wanyama wengine wengi sana,
wambugu ni kabila la kwanza kuhamia milima ya usambara wakitokea arusha ambako walipigana na jamii nyingine ya wamasai, wambugu walipofika moshi na mifugo yao walifukuzwa na walipofika upareni walifukuzwa na wapare ndipo walipohamia milima ya usambara, makabila mengine yaliofika lushoto ni wazigua, wabondei, wapare na wakenya toka taita ndo maana kuna wasambaa wanatumia jina la ukoo WATAITA, Kimweri alitokea handeni na akaja kuwa mtawala wa maeneo yote ya lushoto Enzi hizo japo kiukweli kimweri si wakwanza kufika lushoto, wasambaa wanaojiita WAKILINDI (mimi mmojawapo) tumetokana na kizazi cha chief Kimweri, ambapo asili ya jina wakilindi ni kwamba baba yake kimweri ana asili ya bara asia japo yeye alizaliwa na mama mwafrika mzigua ndo maana wakilindi ni watu weupe sana coz ni machotara wenye asili ya kiarabu.
CC. Elli , MANI , Paloma , mshana jr
Kimweri hakutokea bara. alizaliwa Soni ni mjukuu wa Mbegha chotara aliyetokea wilaya ya kilindi karibu na milima ya Nguu.
Rudia tena kusoma post yangu mkuu, hakuna seheme nimesema kimweri katokea bara, ila nimesema ana asili ya bara la ASIA,Kimweri hakutokea bara. alizaliwa Soni ni mjukuu wa Mbegha chotara aliyetokea wilaya ya kilindi karibu na milima ya Nguu.
Natafuta kiwanja au shamba karibia na Sekuko university. Vinapatikana? Una no ya dalali tafadhali?Karibuni wadau wa Jf uliza ujibiwe kuhusu wilaya ya Lushoto na maeneo yake. Hii ni moja ya wilaya nzuri kabisa ndani ya mkoa wa Tanga. Karibuni...
CC: mshana jr
Kuna viwanja pale jirani na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa Milioni 40, sema neno.Natafuta kiwanja au shamba karibia na Sekuko university. Vinapatikana? Una no ya dalali tafadhali?
Mimi mwenyewe upande wa mama ni msambaa wa kwetonge -Mashewa Korogwe ila kwa wewe Bategereza hatuna shemeji.
Hayo ni maneno yako. waifu ananiamini mia kwa mia
. Magari yetu yote ni jina lake. nyumba ya pili na mashamba ni jina lake. ATM zote anatunza yeye. saa mbili usiku nishafika home. Jumapili tunakua wote masaa 24. Akija mjinga hapa kwetu kkufuata mali zangu nikifa amegonga mwamba. cha zaidi we love each other. sasa kama unasema huna shemeji ni maneno yako na maneno hata kwenye kanga yapo
Hayo ni maneno yako. waifu ananiamini mia kwa mia
. Magari yetu yote ni jina lake. nyumba ya pili na mashamba ni jina lake. ATM zote anatunza yeye. saa mbili usiku nishafika home. Jumapili tunakua wote masaa 24. Akija mjinga hapa kwetu kkufuata mali zangu nikifa amegonga mwamba. cha zaidi we love each other. sasa kama unasema huna shemeji ni maneno yako na maneno hata kwenye kanga yapo
hapo umempatia mkuu...
Vipi kuhusu manyau ya meeda ,corner bar bwana shemeji.
inatengenezwa kwa miwa...inapatikana kwa bei rahisi tuu
Yale manyau mara moja moja sio mbaya. kaka ikiwa hata mawaziri wana michepuko itakua mimi mtu wa kawaida. Nipe jina la mtu mmoja ambae hana mchepuko na mimi ntaacha MEEDA