Niulize chochote kuhusu Jiografia

Niulize chochote kuhusu Jiografia

Lavit

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
15,864
Reaction score
36,192
Nakaribisha maswali kwenye hili eneo kuhusu tabia nchi, hali ya hewa, mabonde, milima, mito, bahari, mazingira, majanga ya asili, anga na mengine yaliyomo. Lolote linalokutatiza uliza, majibu utapata hata kama siyo kwangu wengine watasaidia.

1469768410131.jpg
 
Je kuna tofauti kati ya mji mkuu na makao makuu ya nchi? Na je mji mkuu wa tanzania ni upi na makao makuu ni wap?
Hakuna tofauti, mara nyingi makao makuu ya nchi yanakuwa katika mji mkuu! Hivyo basi mji mkuu ambao unakuwa makao makuu ya nchi shughuli zote kuu za serikali zapaswa kufanyika hapo!
Kwa tafsiri hiyo hapo juu, mji mkuu kwa Tanzania ni Dodoma na makao makuu pia, na ndiyo maana zinasikika harakati za kuhamishia shughuli kuu za serikali huko!!
 
je kama dunia inazunguka kwann maji ya bahari hayamwagiki?
 
Dah kumbe wengi tuko tunaopenda kujua mambo ya ki-jiografia! Nasikia South Africa kuna sehemu ambayo maji ya moto kabisa na maji baridiii yamepakana imasababishwa na nini. Na kikubwa inakuwaje joto halisambai kwenye maji baridi?
 
Tunaaminishwa kuwa dunia hulizunguka jua kutoka magharibi kwenda mashariki; lakini sijawahi kuta mlango wa ghetto langu umegeukia upande mwingine hata siku moja, kwa nini isiwe hivyo kama dunia hujizungusha kweli?
 
Hakuna tofauti, mara nyingi makao makuu ya nchi yanakuwa katika mji mkuu! Hivyo basi mji mkuu ambao unakuwa makao makuu ya nchi shughuli zote kuu za serikali zapaswa kufanyika hapo!
Kwa tafsiri hiyo hapo juu, mji mkuu kwa Tanzania ni Dodoma na makao makuu pia, na ndiyo maana zinasikika harakati za kuhamishia shughuli kuu za serikali huko!!
Mji mkuu ni mahali ambako shughuli nyingi za kiuchumi, kijamii na pengine kisiasa zinafanyika. Makao makuu ni mahali ambako shughuli za kisiasa na kiutawala kwa ujumla zinafanyika. Kwa muktadha wa Tanzania, mji mkuu ungali Dar es Salaam. Makao Makuu ya nchi ndiyo yapo Dodoma.
 
Tunaaminishwa kuwa dunia hulizunguka jua kutoka magharibi kwenda mashariki; lakini sijawahi kuta mlango wa ghetto langu umegeukia upande mwingine hata siku moja, kwa nini isiwe hivyo kama dunia hujizungusha kweli?
Suala la dunia kuzunguka dunia siyo suala la imani, tayari imethibitishwa hivyo!!
Suala la gheto kugeukia upande mwingine haliwezi kutokea sababu sisi tupo kwenye surface ya dunia, hivyo position ya vyote vilivyomo vikichagizwa na nguvu ya uvutano(gravitational force) haviwezi kubadili position!
 
je kama dunia inazunguka kwann maji ya bahari hayamwagiki?
Maji ya bahari hayawezi kumwagika kwasababu ya nguvu ya uvutano kuelekea katikati ya dunia!!
Vile vile nguvu ya uvutano kati ya mwezi na dunia pia inainfluence maji ya bahari kuendelea kuwepo katika position yake!
Pia nguvu ya uvutano ya mwezi na dunia ndiyo inayopelekea kupwa na kujaa kwa maji baharini!!
 
Nini kinasababisha anga kuwavla blue na white?
Kikubwa cha kufahamu ni kwamba mwanga wa jua una rangi tofauti tofauti japo kwa macho ya kawaida unaonekana ni white..
Red
Orange
Yellow
Green
Blue
Violet

Pia molecules za mwanga wa blue zinasaambaa zaidi zaidi kuliko molecules za rangi zilizobakia na hii ndiyo inafanya anga kuwa na rangi ya blue!!
 
Hapa utakimbia mwenyewe kwa maswali Baba
Si umeomba uulizwe chochote juu ya jografia
Elewa hili ndio somo la vilaza
Sema unaetaka kuulizwa kuhusi historia hajapatikana bado
 
sayari zinaangaliwa na nini? Kuna wakati tuliambiwa kuna sayari 7 alafu badae tukasikia zimeongezeka nyingine 2 manake zimekuwa 9.. Je kipimo gani kinachotumika kuziona hizo sayari na kwa nini hazikuonekana zote tangu awali? Je kuna uwezekano wa kugunduliwa sayari zingine zaidi ya hizo 9?
 
Back
Top Bottom