Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

asanre sana mkuu wa uzi mzuri
hakika una tusaidia sana.


mkuu naomba kuuliza.

gari yangu ni IST
kila nikiwasha kuna kama mswaki wa bluu unatokeza kwenye dash board na kujifuta baada kama ya dakika 3 hivi



hii alama ina maana gani ?





pili naweza aje kugundua kupitia dash board kua engine oil imepungua sana ili nibadilishe ?


asante
 
Engine Check ikiwaka ni lazima kuwe na hitilafu fulani. Jibu sahihi litapatikana tu kwa kuinganshia na computer scanner kusoma code zake.

Kama gari inatembea vizuri wala haionyeshi hitilafu yoyote, basi sababu mojawapo ya engine light inaweza kuwa ni catalytic converter kwenye exhaust kuishiwa nguvu, haichuji gesi chafu kutoka kwenye Moshi wa exhaust sawasawa.

Kama hauendeshi kwenye barabara za California, hilo litakuwa siyo tatizo kubwa sana, ila sasa ujue gari yako inachafua mazingira sana. Hiyo ndiyo sababu inayoonekana mara kwa mara hasa gari likisha kuwa na umri wa kuanzia miaka minane.
Vip kuhusu ractis new model
 
asanre sana mkuu wa uzi mzuri
hakika una tusaidia sana.


mkuu naomba kuuliza.

gari yangu ni IST
kila nikiwasha kuna kama mswaki wa bluu unatokeza kwenye dash board na kujifuta baada kama ya dakika 3 hivi



hii alama ina maana gani ?





pili naweza aje kugundua kupitia dash board kua engine oil imepungua sana ili nibadilishe ?


asante
Bila shaka taa unayoiona ni hii
...Hii ni taa ya joto la engine...ikiwaka blue means engine ipo katika hali ya baridi, injini ikipata moto taa hii inatoweka.

Injini ikipata joto lililopitiliza kiwango au gari likichemsha taa hiyo itawaka nyekundu..

Kuhusu kujua kama oil inahitajika kubadilisha au imepungua kwa kuangalia signal kwenye dash board, si magari yote yenye option hiyo.. Magari mengi tuliyonayo ni lazima upime kiwango cha oil kwa deep stick iliyopo kwenye engine..

Kujua kama muda wa kumwaga oil umefika, hapa unaweza kutumia clock ya gari lako kupiga hesabu za umbali uliotembea tangu ubadilishe oil kwa mara ya mwisho..
Kwa mfano

Mile age ya gari lako inasoma Km 40000 nw umeweka oil mpya na filter kwenye mile age hiyo...inategemea na aina ya oil ila mara nyingi tunakadiria km 3000 ndipo umwage tena oil...

Hivyo utachukua mileage ya km 40000 +3000=43000.....maana yake utaendesha gari lako likifikisha km 43000 kwenye clock, utabadilisha tena oil....
images%20(1).jpg
 
Suzuki Swift inawaka taa ya EPS kwenye dashboard halafu usukani unakuwa mgumu, mafundi wangu wameshindwa kutengeneza utansaidiaje kwa hilo mkuu.
Ulitatua hili tatizo mkuu, nimeface the same problem kwa suzuki swift.
 
Mkuu Safi Sana Kwa Uzi...

Naomba Unisaidie Gari Yangu Ni IST, Huwa Nikiiwasha Asubuhi Au Hata Muda Wa Jioni Wa Kutoka Kazini Kuna Kamlio Flani Kama Ka Mluzi Kanakwenda Sambamba Na Starter Ya Engine...
Na Hata Nikianza Kukanyaga Mafuta Kidogo kidogo Kanaendelea Na Badae Gari Ikichanganya Kanapoteaa...
Tatizo Linaweza Kuwa Nini?
 
Mkuu Safi Sana Kwa Uzi...

Naomba Unisaidie Gari Yangu Ni IST, Huwa Nikiiwasha Asubuhi Au Hata Muda Wa Jioni Wa Kutoka Kazini Kuna Kamlio Flani Kama Ka Mluzi Kanakwenda Sambamba Na Starter Ya Engine...
Na Hata Nikianza Kukanyaga Mafuta Kidogo kidogo Kanaendelea Na Badae Gari Ikichanganya Kanapoteaa...
Tatizo Linaweza Kuwa Nini?
hiyo ni belt ya oltanetor
 
Mkuu Safi Sana Kwa Uzi...

Naomba Unisaidie Gari Yangu Ni IST, Huwa Nikiiwasha Asubuhi Au Hata Muda Wa Jioni Wa Kutoka Kazini Kuna Kamlio Flani Kama Ka Mluzi Kanakwenda Sambamba Na Starter Ya Engine...
Na Hata Nikianza Kukanyaga Mafuta Kidogo kidogo Kanaendelea Na Badae Gari Ikichanganya Kanapoteaa...
Tatizo Linaweza Kuwa Nini?
Inaweza kuwa ni belt imelegea kama ulivyoshauriwa hapo juu au kuna sehemu hewa inavuja kidogo kwenye intake manifold, au spark plugs zina masizi sana kiasi kuwa zinapokuwa baridi haziwaki sawasawa na kusababisha misfire ndogo ndogo. Ni vigumu kukupa jibu kamili bila kusikia mlio wenyewe
 
Mcheki huyu LEGE
Hilo tatizo la la electronic Power Steering nilimjibu huyu; labda hajapata mafundi wa wazuri wa kuangalia vile vitu vidogovidogo nilivyomtajia kabla ya kuangalia yale makubwa. Lama mpaka leo bado analo, basi nlinasababishwa na mambo madogomadogo tu; yapo kadhaa
 
Electronic Power Steering (EPS) failure inapotokea maana yake ni kuwa ile motor inayokusaidia kuzungusha steering wakati wa kupiga kona inakuwa haifanyi kazi sawasawa, kwa hiyo hupeleka data kwenye computer ya injini (ECU) ambayo hukata umeme usiende kwenye motor hiyo kabisa, ndiyo maana steering yako inakuwa ngumu sana.

Hii motor hufanya kazi kwa kusoma nguvu inayotakiwa na steering kwenye kupiga kona fulani wakati wewe unazungusa hiyo steering, halafu huamua kiasi cha umeme wa kuepelea kwenye motor hiyo kusudi ibebe mzigo huo badala yako. Sasa basi, wakati mwingine hutokea kwa bahati mbaya tu kwamba computer ilipata spike ya data mbaya lakini hakuna tatizo; ukizima injini na kuondoa waya mmoja wa betri kwa robo saa na kustart gari tena itafanya kazi tu. Ila kama haifanyi kabisa hata ukishazima injini na kuondoa waya mmoja wa betri, basi kwa kisi kikubwa itakuwa ni steering torque sensors zinahitaji kubadilishwa, au kwa kiasi kidogo sana labda ni motor yenyewe imechoka.

Kiwango kidogo zaidi na ambacho ndicho serious sana ni pale ile gearbox inayoendesha steering yako itakuwa ndiyo imekufa. Hayo ndiyo maeneo makubwa matatu ya kuangalia.

Kupata jibu halisi, ipeleke gari yako ikafanyiwe coomputer scanning kujua tatizo halisi linatoka wapi. Kama sehemu zote hizo ni sawa kabisa, basi inawezekana alternator yako ndiyo imechoka haipeleki umeme wa kutosha unaohitajiwa kuendesha motor hiyo.
Seen, umemjibu vizuri mkuu
 
Mkuu, swali langu ni kwamba unawezaje kutambua kuwa hii oil ukiiweka kwenye engine kuja kubadilisha ni mpaka maili au km kadhaa mpaka zipite.. 3000, 5000 au 10000.??

Swali lingine ni kuhusu oil grades zinavyoelezewa...
Mfano hii 15w40, wanasema oil huwa thin (15w) ilikuwe na uwezekano wa kuiwasha engine kwa urahisi na engine ikisha waka at normal operating temp ile oil hugeuka na kuwa nzito (40) nahitaji kujua je kweli??

Swali la mwisho ni kuhusu oil zinazoandikwa kwa kupewa viscosity moja tu mfano hii SAE 40, Je hii inamaanisha oil itabaki katika viscosity hiyohiyo bila kujalisha joto la engine litakuwa namna gani???
 
Mkuu, swali langu ni kwamba unawezaje kutambua kuwa hii oil ukiiweka kwenye engine kuja kubadilisha ni mpaka maili au km kadhaa mpaka zipite.. 3000, 5000 au 10000.??

Swali lingine ni kuhusu oil grades zinavyoelezewa...
Mfano hii 15w40, wanasema oil huwa thin (15w) ilikuwe na uwezekano wa kuiwasha engine kwa urahisi na engine ikisha waka at normal operating temp ile oil hugeuka na kuwa nzito (40) nahitaji kujua je kweli??

Swali la mwisho ni kuhusu oil zinazoandikwa kwa kupewa viscosity moja tu mfano hii SAE 40, Je hii inamaanisha oil itabaki katika viscosity hiyohiyo bila kujalisha joto la engine litakuwa namna gani???
Maswali yako yote nilishayajibu huko nyuma, Nitaanza na maswali mawili ya mwisho kurudi nyuma.

Oil zinazotumika katika nchi za baridi pia huwa zina namba mbili, kwa mfano 10W-30. Ile namba inyoishia W ni kwa ajili ya nchi za baridi wakati wa Winter. Ile namba ya pili ndiyo ya kwetu zaidi wakati gari linafanya kazi vizuri. Ila kwa vile kuna sehemu hapa kwetu (kama Mufindi) ambako baridi hufikia lile la nchi za Scandinavia, basi oil nzuri kwako itakuwa ni 5W-30; ila ukitumia SAE 30 uko salama pia lakini siyo wakati wa baridi Mufindi.

Ubadilishaji wa oil hautegemei aina ya oila uliyoweka bali unategemea injini yenyewe. Kila gari ina kitabu kinachoonyesha utabadilisha oil kila baada ya muda gani. Watengenezaji wa magari hujua vyuma vyao vinasagikaje na ndio maana wanasema baada ya muda fulani oil inakuwa imejaa vumbi la vyuma, hivyo ibadilishwe.
 
Wadau Nina swali, Hivi Toyota Kluger yenye cc3000 ukinunua yenye km 120,000 unaweza kaa nayo miaka hata 8? Matumizi ni kutembea km let say 9,000 kwa mwaka. Wazoefu wa hii gari msaada wenu tafadhali.
 
Hivi engine hii ya gari dogo la petrol unaweza weka mafuta ya kupikia badala ya oil ikiwa umezidiwa sana?mafuta ya Korie siyo haya ya alizeti.
 
Hivi engine hii ya gari dogo la petrol unaweza weka mafuta ya kupikia badala ya oil ikiwa umezidiwa sana?mafuta ya Korie siyo haya ya alizeti.
SIjui, ila nimeshasikia kweli kuwa kuna mafuta mengine ya kupikia yanaweza kutumika kama oil kwenye injini ndogondgo, hasa mafuta ya mizeituni. Lakini hayawezi kudumu kwa mufa mfrefu.
 
SIjui, ila nimeshasikia kweli kuwa kuna mafuta mengine ya kupikia yanaweza kutumika kama oil kwenye injini ndogondgo, hasa mafuta ya mizeituni. Lakini hayawezi kudumu kwa mufa mfrefu.
So yanaweza tumika kama dharura? Je nikiwasha gari ikawaka then nikachomoa battery itazima?gari za miaka ya 2000 kushuka chini.
 
Back
Top Bottom