Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Naomba kujua hili swala la kuwasha gari asubuhi au likiwa limekaa muda mrefu bila ya kutembea,kuna wanaosema inabidi usubiri kama dkk 2 ndio uondoke na wengine wanasema unaweza tu kuondoa gari,tupe ufafanuzi hapa lipi hasa ni kweli na sababu ni nini...?

Jibu la Boeing 747 ni sawa kabisa; dakika mbili bado ni nyingi sana. Kwenye nchi za baridi sana engine huweza ku-contract na kusababisha vipimo cha parts mbalimbaliza injini visilingane kama ilivyokusudiwa, hivyo kusababisha injini isiweze kustart vizuri.

Watu wa huko huweka engine block heaters za umeme kuhakikisha injini inapata joto la kuweza kustart. Ikisha start, unahitaji kuipa sekunde 20 tu kusukuma oil kwenye sehemu mbalimbali za injini kabla ya kuanza safari; ni muda wa kutosha wewe kuvaa mkanda na kupuliza hewa ja joto kwenye windshield kukausha umande kabla hujaanza safari.

Ukikaa nchi za baridi unaweza kuona jirani anawasha gari analiacha linawaka wakati anakula breakfast; nia ya kufanya hivyo ni kuweka joto ndani ya gari kabla hajaingia, na kwa bahati mbaya huo sio utaratibu mzuri kwa sababu wakati injini iko kwenye idling conditions kwa muda mrefu, huweka masizi mengi sana kuliko wakati inatembea.
 
Mkuu Kichuguu, naomba unishauri kuhusu Nissan X trail, Hi ni gari ambayo navutiwa nayo sanaa hasa Nissan X trail Axis. Je, unaweza kunishauri chochote kabla sijanunua hii gari maana napenda sana magari ya SUV.
Ntashukuru kama utanijibu kwa nafasi yako.
Hayo magari huku Marekani hayapo, nadhani equivalent yake ni Nissan Rogue. Unapenda kuilinganisha na gari gani, na kwa kulinganisha vitu gani, comfortability, reliability, stability, au fuel consumption? Muonekano wa nje tu siyo factor kubwa sana
 
ENGINE YA BEAM 2000 (1G Fe) ILIKAPA T.BELT IKAPASUA PISTON NAMBA MOJA. NIMEBADILISHA CYLINDER HEAD NA HIYO PISTON GARI HAIJARUDIA MLIO WA MWANZO SASA NAFIKIRIA KUBADILISHA MSWAKI UNANISHAURI NINI MKUU

Kosa kubwa ni kuchelewa kubadilisha timing belt. Je, ilipasua piston au ilivunja valve rods? Huenda pia hakukuwa na haja ya kubadilisha Cylinder head iwapo haikupasuka popote. Kama ilipasua piston kweli basi matatizo yalikuwa ni makubwa sana kwani hiyo itakuwa ni pamoja na connecting rods zote na pia crankshaft bearings. Ili kusuka upya injini yako, ondoa piston zote uweke mpya za aina moja, na Connecting rods zote pia uweke za aina moja, vile vile na crankshaft bearings zote uweke za aina moja. fanya hivyo hata kama kuna unavyoona kuwa havina madhara; usichange parts za zamani na mpya kwenye injini.
 
Mkuu Kichuguu mimi gari yangu nikiwasha,ikiwa imepoa engine kabisa au asubuhi kuna kamlio kama kitu kinagonga,ni kama vile kichuma kinagonga,kinachukua kama dkk 2 halafu kinaacha,na ninapoiwasha gari ikiwa gari ilishatembea huwa hakitoi mlio,na mlio unatokea maeneo yanapokutana engine na gearbox,hii shida itakuwa ni nini,mara nyingi sana ni wakati wa asubuhi..?
 
Mkuu Kichuguu mimi gari yangu nikiwasha,ikiwa imepoa engine kabisa au asubuhi kuna kamlio kama kitu kinagonga,ni kama vile kichuma kinagonga,kinachukua kama dkk 2 halafu kinaacha,na ninapoiwasha gari ikiwa gari ilishatembea huwa hakitoi mlio,na mlio unatokea maeneo yanapokutana engine na gearbox,hii shida itakuwa ni nini,mara nyingi sana ni wakati wa asubuhi..?

Sijui aina ya mlio unaopata; ila magari mengi yanayotumia hydarulic valve lifter yakiwa ya baridi yanaweza kustart na mlio kama misfire lakini baada ya muda kila kitu kinakuwa sawa tu, jambo hio husababishwa na oil chafu kutofungua valve sawasawa. Check Oil yako kama ni safi na una oil ya kutosha kwenye samp. kama imeshakuwa chafu au haitoshi basi mwaga oil yote uweke mpya na ubadilishie oil filter; misfire hizo zitakwisa baada ya muda mfupi tangu kuweke oil mpya, haziishi mara moja.

Kama ni kelele ya kama vyuma vinagongana, angalia chini karibu na gear box kwenye njia ya exhaust, huwa kuna bati la aluminum la kuzuia joto la exhaust lisiingine kwenye cabin ya gari lako. Inawezekana nati za bati hilo zimelegea, na linapopata jota lina expand na kushikilia kiasi kidogo cha kufanya usisikie mlio huo. Kama hali ni hiyo, kaza nati zile.
 
Unaweza kubadili engine 1NZ-FE(1.5L) NA kuweka 2NZ-FE (1.3L) kwenye toyota IST ya mwaka 2002?
Ndiyo kwa kiasi fulani lakini kuwa makini kwa sababu TOYOTA IST (kwa marekani zinaitwa scion) zenye injini za 1NZ-FE zipo za 4WD na za Front Wheel Drive. Kwa hiyo kama IST yako ni ya front Wheel Drive, unaweza kubadilisha na 2NZ-FE bila tatizo, ila kama ni 4WD, utapata matatizo ya kuibadilisha.
 
Mkuu , gari kuwa nzito kuchelewa kuchanganya, yaani ukikanyaga mafuta inakua nzito haikimbii sana. Toyota raum, hii inaweza ikasababishwa na nini?
Fuel Pump imechoka; ukibadilisha fuel pump, badilisha pia fuel pressure regulator na fuel filter kama gari yako inayo. Kuna magari ambayo hayana fuel filter bali imejengewa ndani ya fuel pressure regulator tu.
 
N
Sijui aina ya mlio unaopata; ila magari mengi yanayotumia hydarulic valve lifter yakiwa ya baridi yanaweza kustart na mlio kama misfire lakini baada ya muda kila kitu kinakuwa sawa tu, jambo hio husababishwa na oil chafu kutofungua valve sawasawa. Check Oil yako kama ni safi na una oil ya kutosha kwenye samp. kama imeshakuwa chafu au haitoshi basi mwaga oil yote uweke mpya na ubadilishie oil filter; misfire hizo zitakwisa baada ya muda mfupi tangu kuweke oil mpya, haziishi mara moja.

Kama ni kelele ya kama vyuma vinagongana, angalia chini karibu na gear box kwenye njia ya exhaust, huwa kuna bati la aluminum la kuzuia joto la exhaust lisiingine kwenye cabin ya gari lako. Inawezekana nati za bati hilo zimelegea, na linapopata jota lina expand na kushikilia kiasi kidogo cha kufanya usisikie mlio huo. Kama hali ni hiyo, kaza nati zile.
Nitalifanyia kazi ingawa kuna mtu aliniambia kuwa yawezekana ni kichuma kinachogonga kutoka kwenye starter kwenda kwenye flywheel kinachelewa kurudi ndio maana kinatoa huo mlio...
 
Ningependa kujua je kuna ulazima wa gari iliyotembea umbali mrefu kuachwa katika idle position kwa muda fulani kabla ya kuzimwa?

Na kama ulazima upo, gari iwe udle kwa mda gani, na baada ya kutembea kwa umbali kuanzia km ngapi/masaa mangapi?
 
Back
Top Bottom