Nitumie dawa/lotion/mafuta gani?

Nitumie dawa/lotion/mafuta gani?

Sarcomere

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
214
Reaction score
442
IMG_20260521_173451.jpg
Salaam wakuu
Mtu wangu wa karibu (ke) ana changamoto ya kutokwa na vitundu vidogo vidogo (pores) kama inavoonekana hapo kwenye picha...hiyo ni sehemu ya uso shavuni
Akivikamua/akiviminya izo pores zinatoa kitu kama mafuta mgando mweupe

Anaomba ushauri kwa wataalam wa ngozi na wengine waliowahi kuwa na ngozi kama hiyo atumie lotion gani au mafuta gani au sabuni gani au dawa gani ili ngozi yake iwe smooth/nyororo na ivo vitundu viondoke?
 
kabla hatuja kushauri unatakiwa utueleze skin type ya huyo ndugu yako,, je ni ngozi Kavu au yenye mafuta?,,, kama ni ngozi yenye mafuta hatakiwi kutumia product zenye mafuta mengi na kama ni ngozi Kavu anatakiwa atumie product zenye mafuta,,, na pia unatakiwa ujue kama ngozi yake ni ile nyepesi au ngumu maana kuna product anaweza kutumia pia zikamharibu zaidi badala ya kumsaidia
 
Hizo ni acne tiba yake ni ya mateso na ni dozi ya miezi 6 unakomesha kabisa tatizo, ila sasa wengi hushindwa na kukatisha dozi!!
 
Acha kujiwekea gharama za bure na kumuekea wife chemical ambazo mwisho wa siku utakuja utibu kwa gharama kubwa.
Kama kuna mwalovera na ununue vaseline mgando. Kila cku asuhuhi na jioni anapaka hayo maji usoni akae nusu saa au hata lisaa lizima kama haendi sehem after hapo anawe uso apake hiyo vaseline tu asiongeze chochote hiyo shda itaisha. Kuna vidude veusi vinatokeaga usoni mzee mwingne akaambiwa kuwa vinang'olewa kweli akawa anang'olewa akiambiwa kuwa vitaisha kumbe ndo kuviongeza zaidi sa ivi uso umekuwa kama chura wa gredi toka china yaani ngozi ina layer ya juu na ya ndani
 
Acha kujiwekea gharama za bure na kumuekea wife chemical ambazo mwisho wa siku utakuja utibu kwa gharama kubwa.
Kama kuna mwalovera na ununue vaseline mgando. Kila cku asuhuhi na jioni anapaka hayo maji usoni akae nusu saa au hata lisaa lizima kama haendi sehem after hapo anawe uso apake hiyo vaseline tu asiongeze chochote hiyo shda itaisha. Kuna vidude veusi vinatokeaga usoni mzee mwingne akaambiwa kuwa vinang'olewa kweli akawa anang'olewa akiambiwa kuwa vitaisha kumbe ndo kuviongeza zaidi sa ivi uso umekuwa kama chura wa gredi toka china yaani ngozi ina layer ya juu na ya ndani
Shukrani sana
 
Back
Top Bottom