Nitawaletea Mwanaharamu wa Kuchi

Nitawaletea Mwanaharamu wa Kuchi

Malila

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2007
Posts
5,372
Reaction score
5,124
Tembea uone,
Leo nilipiga kwata pwani kijiji fulani kutafuta kuku aina ya kuchi. Baada ya kuona kuchi original hawapatikani mpaka kisiwani Juani mafia ikabidi nibadili mpango, nikaomba waniuzie Chotara wa Kuchi. Kila nikiwaambia nataka Bokea ( Bokea ni jina la chotara wa kuchi kwa baadhi ya maeneo ya Pwani), wenyeji wangu hawakunielewa, baadae nikafafanua kuwa ni kuku ambaye jogoo alikuwa kuchi na mtetea ni hawa wa kawaida.

Mara moja yule mzee kasema "kumbe unataka mwanaharamu wa Kuchi" hao wapo wengi utawapata mwanangu !!!. Ilibidi nicheke kidogo, kumbe hata kuku wanazaa haramu.

Nimepata hawa haramu wa kuchi mitaa ya Ikwiriri na Rufiji, nitawakusanya na kuwaleta Dar, atakayetaka basi tuwasiliane ili siku wakifika namjulisha ili awachukulie kwangu. Na nitaendelea kuwakusanya hawa Bokea pamoja na majogoo original ya kuchi taratibu, ila bei imesimama. Ambao hawajaanza kuwika bei ni Tsh 20,000/ pale Ikwiriri na Rufiji, ila Kuruti bei ni nzuri kiasi ni Tsh 15,000/ gharama ya Kuruti ni usafiri wa boti.

Je unataka Haramu wa kuchi nikupee!!!!!
 
hahaaaa,, hilo jina la mwanaharam nimelipenda. Ila mkuu ningependa kujua ubora wa hao kuchi hadi kupelekea kuwatafuta hivyo
 
Malila kuna kuch wengi singida vijijini pia nilitembea huko nikashangaa kuku wakubwa ajabu nilichukua wa kwangu wawili wakufuga,
 
Last edited by a moderator:
Nawahitaji sana hao bastards wa kuchi mkuu

Poa, be online, hawa wanaharamu wa kuchi ni wazuri, mpaka jioni hii jamaa kaniambia wapo 25 hivi. Nataka wafike 50 ili niwalipie nauli waje, na huku nikiandaa chanjo na uzio wao kwanza. Wakifika nitakupa pm.
 
Malila kuna kuch wengi singida vijijini pia nilitembea huko nikashangaa kuku wakubwa ajabu nilichukua wa kwangu wawili wakufuga,

Asante,
Mwaka juzi tulichukua kuchi hao 85 toka singida kwa ajili ya shule pale Mkuranga, walifariki mmoja mmoja hadi wakaisha, nadhani tulichukua msimu mmbaya, sasa hawa wa humu pwani hawasumbui sbb mabadiliko ya hali ya hewa si makubwa, mfano toka Mafia mpaka Dsm si mbali kivile.

Hata hivyo, mipango ya kuwaleta toka Singida haijafa, kinachofanyika ni maandalizi ya shamba la kisasa.
 
hahaaaa,, hilo jina la mwanaharam nimelipenda. Ila mkuu ningependa kujua ubora wa hao kuchi hadi kupelekea kuwatafuta hivyo

Kwanza wana size kubwa sana,halafu majogoo yao ni mababe na magomvi sana, kwa hiyo ni kivutio. Pia majogoo yake bei imefikia laki moja na nusu kwa wanaopenda michezo.

Kuna siri nyingine, Wapemba wanawataka kwa ajili ya michezo ya kitalii huko kwa wenzetu. Kuchi wa uhakika unampata kwa laki mbili.
 
Huku kuanzia mwezi wa 11-3 usichukue kuku kabisa Malila
 
Last edited by a moderator:
Huku kuanzia mwezi wa 11-3 usichukue kuku kabisa Malila

Naam ndio kipindi kibaya sana kama hujajua, sisi tulichukua kipindi hicho. Nifanyie utafiti, mitetea ambayo haijaanza kutaga kwa sasa inatembea bei gani huko Singida?
 
Inategemea na maeneo ukiweza kuingia vijijini ndani kabisa ni kuanzia 6000-9000 inategemea na eneo ukifika huku mjini ni 8000-10000
Naam ndio kipindi kibaya sana kama hujajua, sisi tulichukua kipindi hicho. Nifanyie utafiti, mitetea ambayo haijaanza kutaga kwa sasa inatembea bei gani huko Singida?
 
Inategemea na maeneo ukiweza kuingia vijijini ndani kabisa ni kuanzia 6000-9000 inategemea na eneo ukifika huku mjini ni 8000-10000

Moja ya makosa tunayofanya wafugaji ni kutozingatia tiba, nimetenga chumba kwa ajili ya kuku wageni ili watibiwe kabla ya kuingizwa shambani waliko wengine.
 
Back
Top Bottom