Uchaguzi 2020 Nitashangaa Wafanyabiashara kumnyima Magufuli kura

Mchimwachimego

JF-Expert Member
Jun 15, 2020
358
271
Kila nikikumbuka maamuzi magumu ya Rais Magufuli kuhusu Corona, sina shaka na utimamu wake na ujasiri.

Kwa kipindi kama kile ambacho nchi nyingi ziliamua kufunga biashara na shughuli nyingi za kiuchumi, mtu huyu aliamua kwamba wafanyabiashara waendelee na biashara zao na shughuli nyingine ziendelee.

Hakuna biashara iliyofungwa, lakini watanzania hawana shukrani wanasahau yote kisa mtu ambaye kwa ninavyomtazama mlengo wake si wa kimisimamo binafsi bali ya kuongozwa na anaowaamini.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Magufuli anastaili kukamilisha kipindi cha miaka 10, uongozi si wa kubadilisha kama nguo. Tukipata kiongozi mzuri basi tumuache amalize awamu zote mbili.
 
Na kila ukikumbuka biashara zilivyodorora, Mafrem yalivyofungwa kila mahali, TRA wanavyotupia kodi za ajabu na umati wa raia waliokuwa wanunuzi wa biashara hizo kukosa hela (uwezo) wa kununua tena biashara unajisikiaje kuhusu shaka na utimamu wake mkuu?
 
Yaani mfumo wa biashara ulioharibikwa kwa miaka mitano uje kusafishwa na hicho cha corona?!!! Wafanya biashara nchi nzima wako hoi!! Wengine walijiua kutokana na maamuzi ya ovyo mfano sakata la pombe za kwenye paketi(viroba) korosho mbaazi pamba!

Nenda kwa wafanya biashara wa samaki, na mazao ya misitu!!! Sio una kaa tu mjini hapo na kuja na vihoja vya kitoto!!! Leo ana kuja TRA a nakupigia hesabu za miaka 15! iliyopita eti walikuwa wme underestimate mapato yako, ki makosa hivyo hiyo tofauti unatakiwa ukailipe!
 
Wafanya biashara gani unaowazungumzia? kwasabababu biashara zilianza kufa tangu JIWE alipoingia madarakani, zilizobakia zipo ICU, sasa unataka Mtu aliyekuwepo ICU ampe kura yule aliyesababisha awepo ICU?

what a hillarious!🤣🤣
 
Yaani mfumo wa biashara ulioharibikwa kwa miaka mitano uje kusafishwa na hicho cha corona?!!! Wafanya biashara nchi nzima wako hoi!! Wengine walijiua kutokana na maamuzi ya ovyo mfano sakata la pombe za kwenye paketi(viroba) korosho mbaazi pamba!! Nenda kwa wafanya biashara wa samaki, na mazao ya misitu!!! Sio una kaa tu mjini hapo na kuja na vihoja vya kitoto!!! Leo ana kuja TRA a nakupigia hesabu za miaka 15!!!iliyopita eti walikuwa wme underestimate mapato yako, ki makosa hivyo hiyo tofauti unatakiwa ukailipe!!!
Acha uongo ni 5years back si 15. Na wanafanya kutokana na hesabu zako zilizokaguliwa na mkaguzi uliyemtafuta we we na kusainiwa na wewe.
 
Acha uongo ni 5years back si 15. Na wanafanya kutokana na hesabu zako zilizokaguliwa na mkaguzi uliyemtafuta we we na kusainiwa na wewe.
Mimi ni victim wa hilo ninalosema hadi leo hii, lipo kwenye baraza la kodi, tunavutana!! Licha ya punguzo kubwa walilopunguza bado halikubariki!! Mwishowe imekuwa kama biashara 'sasa unasemaje unataka kulipa ngapi' 'mtu ana kuta ana deni eti la bilioni tatu!!! Hahaaa, kuna maneno aliyasema zitto japo ni makali ila ndio ukweli, GENGE LA WAPORAJI
 
Kumbuka kuwa kama pangekua hakuna upinzani huenda maamuzi yake yasingekua yale.
Wapinzani walimtaka atoe ruzuku awape wafanyabiashara ili afanye Lock down na atoe laki 3 kwa kila familia.

Kama kawaida JPM hua hapangiwi.
Kutokusikiliza hoja za wapinzani ndiko kulikopelekea maamuzi Yale. Lakini yeye mwenyewe alikwenda kujificha zaidi ya mwezi.

Yote kwa Yote Wapinzani walikua na Nia nzuri mana lock down lilikua ni takwa la kitaalam hasa upande wa afya ili kupunguza maambukizi.
JPM naye akakataa kwa kuwa serikali haikuwa na uwezo wa kuwapa watu chakula. Wote walikua na nia ya kuangalia uhai wa watu.

Ni wapumbavu tu ndio wanaopuuza mchango wa wapinzani Ndani na nje ya Bunge. Hata CCM wakiwa chama cha upinzani watapinga na itakua ni haki yao kupinga. Yote kwa yote hatutaki kuona watanzania wanauawa kwa dhulma za wakurugenzi. Mkurugenzi atakayegeuza matokeo anapaswa kubeba laana ya mauti yeye mwenyewe sio wapiga kura.

Ni ujinga mkubwa kila uchaguzi kuna wakurugenzi wanapindua matokeo kwa sababu ya Rushwa wanazopewa kisha watu wengine ndio wanauawa kwa kupigwa risasi huo ni umwagaji wa damu isiyo na hatia kwa kuacha yule mwenye hatia akila raha kama vile amefanya jambo zuri.

Tuwaambie ukweli wakurugenzi watende haki ili kulinda amani ya watanzania. Vyama visiwafanye wakashindwa kutii hata amri za Mungu anayesema kuwa Haki huinua Taifa. Bali dhambi ni aibu kwa watu wote. Dhambi ya Utawala wa Gadaf kuua watu imekua ni aibu kwa walibya wote sasa hakuna mwenye amani.

Watanzania tujifunze kwa wenzetu waliovunja haki na sasa wote wanapata adhabu kwa usawa. Kila mmoja analia kwa sababu ya wachache waliovunja haki kwa manufaa yao huku wakisifiwa na wachache kwa manufaa ya madaraka.
 
Kila nikikumbuka maamuzi magumu ya Rais Magufuli kuhusu Corona, sina shaka na utimamu wake na ujasiri.

Kwa kipindi kama kile ambacho nchi nyingi ziliamua kufunga biashara na shughuli nyingi za kiuchumi, mtu huyu aliamua kwamba wafanyabiashara waendelee na biashara zao na shughuli nyingine ziendelee.

Hakuna biashara iliyofungwa, lakini watanzania hawana shukrani wanasahau yote kisa mtu ambaye kwa ninavyomtazama mlengo wake si wa kimisimamo binafsi bali ya kuongozwa na anaowaamini.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Magufuli anastaili kukamilisha kipindi cha miaka 10, uongozi si wa kubadilisha kama nguo. Tukipata kiongozi mzuri basi tumuache amalize awamu zote mbili.
Kama kuna watu wanatakiwa kuponda kichwa cha nyoka ni wafanyabiashara; wamenyanyaswa kwa utitiri wa kodi, wamedulumiwa, wamefilisiwa...
 
Kila nikikumbuka maamuzi magumu ya Rais Magufuli kuhusu Corona, sina shaka na utimamu wake na ujasiri.

Kwa kipindi kama kile ambacho nchi nyingi ziliamua kufunga biashara na shughuli nyingi za kiuchumi, mtu huyu aliamua kwamba wafanyabiashara waendelee na biashara zao na shughuli nyingine ziendelee...
Umetumwa kupima upepo? Kamwambieni huyo kibwengo wenu kuwa HATUMTAKI. Na nawakilisha wafanyabiashara 90+% wadogo (SMEs) wa nchi hii.
 
Tena msitukumbushe machungu wafanyabiashara hatuwezi kumchagua huyo jamaa ametuumiza sana.
 
Back
Top Bottom