Nitakavyomkumbuka JK

Nitakavyomkumbuka JK

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
11,824
Reaction score
18,066
  1. Rais aliyeingia madarakani kwa ahadi lukuki na kuwapa matumaini makubwa Watanzania kuwa na maisha bora!
  2. Rais aliyeingia Ikulu kwa bwembwe kubwa na wafuasi wengi!
  3. Rais aliyeunda baraza kubwa la mawaziri kuliko wote waliomtangulia!
  4. Rais aliyeteuwa viongozi vijana wengi na hasa wanawake kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi!
  5. Rais aliyeanzisha mikoa na wilaya nyingi nchini bila kuzingatia uwezo wa kiuchumi na kiutawala wa serikali yake!
  6. Rais aliyeteuwa majaji wengi bila kuandaa mazingira mazuri ya utendaji wao na uwezo wa kifedha wa serikali yake kuwahudumia!
  7. Rais aliyeteuwa viongozi wengi wake kwa waume, wazee kwa vijana kwa kuzingatia ushwahiba badala ya uwezo na uzoefu wa kazi au taaluma husika!
  8. Rais aliyefanya safari nyingi za nje kuliko wote waliomtangulia na hata kuvunja rekodi kwa viongozi wa bara la Afrika!
  9. Rais aliyedidimiza uchumi kwa kiasi kikubwa kwa kukosa mipango sahihi!
  10. Rais aliyeshindwa kukemea maovu na waovu katika serikali yake kwa kuogopa lawama!

ATHARI KWA TAIFA:

  1. Ukubwa wa serikali umekuwa mzigo mkubwa kulingana na uwezo wa kiuchumi wa Taifa.
  2. Serikali imeshindwa kupata fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo na hivyo kusababisha miradi mingi kusuasua.
  3. Mfumuko wa bei umekuwa mkubwa na hivyo kuathiri wananchi wengi wenye kipato cha kati na chini.
  4. Wananchi wengi wamekata tamaa ya kuwa na maisha bora kama walivyoahidiwa.
  5. Taifa limekosa dira ya maendeleo kwa kutokuwa na hakika ya fedha.
 
Rais aliyejenga chuo kikuu kikubwa Afrika Mashariki na ya Kati, Hii ni college of education pekee, chuo kizima hakiingii kwenye picha moja:

udom-012-college-of-education-hostels23.jpg
 
Ni rais aliyejenga shule za sekondari nyingi hadi katika miji ya Waisilamu kuliko maraisi wote waliyomtangulia.
 
hahaha! zomba nimekukubali, wewe sio mchezo aiseee.... Dah! Hicho chuo kwa kweli kizuri kwa macho, ndio kiko wapi na kitaegemea mambo yepi? Hapo raisi wangu anastahili pongezi kwa moyo mweupe kabisa!

Asalam aleykum'
 
Rais aliyejenga chuo kikuu kikubwa Afrika Mashariki na ya Kati, Hii ni college of education pekee, chuo kizima hakiingii kwenye picha moja:

udom-012-college-of-education-hostels23.jpg

Nasikia majengo yake yameanza kuwa na nyufa.
 
hahaha! zomba nimekukubali, wewe sio mchezo aiseee.... Dah! Hicho chuo kwa kweli kizuri kwa macho, ndio kiko wapi na kitaegemea mambo yepi? Hapo raisi wangu anastahili pongezi kwa moyo mweupe kabisa!

Asalam aleykum'

ESTABLISHMENT:
The University of Dodoma was formaly established in March 2007 following the signing of the charter by the president of United republic of Tanzania. The first academic programmes commenced in september 2007.

The University has been designed on a campus college mode each of which will be semi autonomous. In its structure, six colleges are envisaged when the university if fully established by 2012/13. There are:



  • College of Education
  • College fo Hummanities and Social Sciences
  • College of Informatics and Virtual Education
  • College of Natural Sciences and Mathematics
  • College of Health and Allied Sciences
  • College of Earth Sciences


UDOM initially started with four schools, namely Education, Hummanities, Social Sciences and informatics. Currently three colleges and two schools are Operational. These are College of Education, Hummanities and Social Sciences, and College of Informatics and Virtual Education. In addition there are four chools on transition to Campus College. These are School of Natural Sciences and mathematics, on transition to College of Natural Sciences and Mathematics; School of Medicine and Nursing on transition to College of Health and Allied Sciences; and School of Mines and Petroleum to College of Earth Sciences.


Source: The University of Dodoma
 
NSSF wameisha lipwa pesa ya hicho chuo? aisee sikumbuki kumsikia Jk akikemea rushwa, wakati hili ni tatizo kubwa sana nchi mwetu...
 
Rais aliyejenga chuo kikuu kikubwa Afrika Mashariki na ya Kati, Hii ni college of education pekee, chuo kizima hakiingii kwenye picha moja:

udom-012-college-of-education-hostels23.jpg

Kwa kutumia fedha za NSSF na PPF ambazo ni michango ya walalahoi wa nchi hii. Ameshindwa kurejesha fedha hizo kutokana na serikali yake kutokukusanya kodi. Matokeo yake amekimbilia kupeleka muswada bungeni kutaka wafanyakazi wote wanachama wa NSSF na PPF kufutiwa mafao ya kujitoa na kuweka masharti kuwa mafao kwasasa ni mpaka mfanyakazi (mwanacha) atakapostaafu. Aibu kubwa sana.
 
Ni Rais pekee katika historia ya nchi yetu ambae msafara wake una AMBULANCE... mtu ambae hajui akiona msafara wake anaweza dhani wanasafirisha mgonjwa au maiti..
 
Nitamkumbuka kama rais wetu aliyefanya mambo makubwa kuliko wote waliomtangulia
1.Chuo kikuu dom hakuna mfano wake africa
2.kupandisha mishahara ya wafanyakazi
3.Sekondari kata zote nchini hakuna tena wasichana kuchukuliwa uhousgirl wote shule
4.Zahanati kila kijiji hadi 2015 vijiji vyote vina zahanati
6.uhuru wa vyombo vya habari
7.Hajafanya biashara yeyote full time yuko kuhudumia wananchi
8kapambana na mafisadi kwa uthubutu wa kipekee ambao wenzie uliwashinda(CAG,PCCB nk nk)
9.Kaboresha jeshi la polisi maslahi yao na vitendea kazi(magari VX kwa rpc,hardtop za kumwaga,deffender,majengo ya kisasa askari wanamudu maisha sasa hadi wameeza kununua magari)
10.Barabara kajenga nyiiingiii hadi 2015 zitakuwa zimekamilika
11---- ni mengi mengi mazuri tatizo ushabiki wa siasa za kizamani zisizokuwa na tija yeyote ndo mnaandika msiyoyajua hamna hata shukurani nyie wala moyo wa kusifia mazuri mnasikitisha sana kumbukeni mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
 
Kwa kutumia fedha za NSSF na PPF ambazo ni michango ya walalahoi wa nchi hii. Ameshindwa kurejesha fedha hizo kutokana na serikali yake kutokukusanya kodi. Matokeo yake amekimbilia kupeleka muswada bungeni kutaka wafanyakazi wote wanachama wa NSSF na PPF kufutiwa mafao ya kujitoa na kuweka masharti kuwa mafao kwasasa ni mpaka mfanyakazi (mwanacha) atakapostaafu. Aibu kubwa sana.

Ulitaka atumie fedha za nani? hivi ulikwenda NSSF kudai mafao yako ukaambiwa hakuna.
 
Rais aliyejenga chuo kikuu kikubwa Afrika Mashariki na ya Kati, Hii ni college of education pekee, chuo kizima hakiingii kwenye picha moja:

udom-012-college-of-education-hostels23.jpg

chuo kimejengwa na nssf, ppf, nhif kwa pesa yetu sisi na si KJ ka mnavyodhani!
 
Raisi aliyevunja rekodi kwa kupiga picha na wasanii na warembo
 
Watu aina ya Zomba wanaamini maendeleo ni vitu na sio watu.

Kuna tofuati gani na majengo ya zahanati yasiyo na dawa, vifaa wala wataalam? Au kuna tofauti gani na mejengo (dhaifu) ya vyumba vya madarasa yasiyo na walimu, nyenzo na vifaa vya kufundishia?

Najua uko kazini, lakini bila shaka kazi yako ni suluba na dhalili sana.
 
Nilikugongea like ulipomkubali JK kwa kujenga UDOM lakini kwa hili naona ni zile jazba za watu wanaokwepa kujibu hoja na kuzusha vurugu.
 
Back
Top Bottom