Nisome nini chuoni mwaka huu 2025?

Nisome nini chuoni mwaka huu 2025?

Luca Paguro

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2023
Posts
476
Reaction score
1,060
Wakuu mimi ni mkazi wa Lindi nimesoma PCM shule moja uboizini huko Mbeya na nimemaliza mtihani wa taifa siku chache tu zilizopita. Hapa bado nawaza niende JKT au nipumzike home hii miezi kadhaa

Kwa nilivyofanya mtihani najua nitapata Division 1 ya point 6 hadi 8.
Sasa kuna Jambo linanitatiza hususani kwenye hii era ambayo ajira hakuna. Naomba ushauri kwa JF Experts.
Vyuo ninavyotamani kusoma ni
  • University of Dodoma
  • Dar es Salaam Institute of Technology
  • National Institute of Transport
  • Dar es Salaam Maritime Institute
  • Mbeya University of Science and Technology
  • Muhimbili University of Health and Allied Sciences
UDSM na MUHAS napapenda ila nasikia cutting point zao ni kubwa Sana

Sasahivi walimu wetu wanatuambia kuwa Biomedical Engineering ina soko ila kama ukipata ufaulu chini ya Division 1 ya 5 hupati chance ya kusoma hiyo kozi

Kwa hiyo huwa nawaza sana nisome kozi ipi ambayo ina nafasi kubwa ya kupata ajira au kujiajiri at least ukilinganisha na kozi nyingine

Watu wengine wanasema Computer Engineering ina soko, hivi ni kweli wakuu au ndo tunaingizana cha kike?

Kozi nyingine ninazowaza ni
  • Mechanical Engineering
  • Automotive Engineering
  • Electrical Engineering
  • Chemical Engineering
  • Mechatronics Engineering
  • Telecommunications Engineering

Kweli napenda Engineering ila sijui hata ipi inahitajika kwa Bongo ipi haihitajiki. Nimesoma thread nyingine nyingi ila bado sijapata majibu. Kuna muda nawaza niachane na Engineering labda nisome Accounting and Finance au Agricultural Science pale SUA ila nahisi watu wa Accounting ni wengi sana. Ajira zitakuwa ngumu mbeleni (sijui ila ninahisi tu)

Au nisome "Mechanical Engineering" Halafu nikatafute kazi JWTZ maana walisema ni kozi adimu na inahitajika jeshini. Au sijui nisome Automotive Engineering kwenye magari au hata treni nione kama ina tija 🥲

Nikisikia na watu wa mtaani wanavyotutisha kuhusu maisha ya mtaani yalivyo magumu ndo nachanganyikiwa kabisa. Hizo habari zinafanya nakosea hadi raha. Au niende chuo nikasome kwa bidii sana nipate GPA kubwa nione kama naweza kuwa lecturer. Nawaza mengi ila bado Niko njia panda Sana.

Naombeni ushauri wakuu nikasome nini chuo. Kozi yoyote Ile nzuri yenye soko la ajira Tanzania hata kama ni ngumu fresh tu, kupiga msuli naweza maana nina hamu sana na ajira.
Naombeni mawazo yenu wakuu
 
Ukisoma kozi kwa sababu ina soko utakuja kupata nsobgo wa mawazo baadae. Hizo kozi unasema zina soko leo fikiria miaka 4 au mitano baada ya wewe kumaliza chuo. Je zitaendelea kuwa na soko? Bila shaka soko linakuwa limebadilika.

Nadhani swala la muhimu ni kuangalia passion yako na utayari wa wewe kuitumia hiyo kozi maishani. Suala la Ajira linabadilika sana. Kuna kipindi niko sekondari Telecom Ilikuwa kozi matata sana. Lakini namaliza form six ikawa Petroleum, ila tulipomaliza chuo waliosoma petroleum wakjikuta mtaani
 
Chukua unachotaka kuchukua:
A. JKT ni upotevu wa muda, ratiba za jkt na kujiandikisha chuo na mikopo zinaingiliana sana utajikuta unakurupuka. Tulia (Ila usipumzike😂) fuatila kama ni chuo gani utaenda? Je mazingira utayaweza? Ukishajua chuo gani unaenda vitu vya kusoma vitajichuja

B. Angalia ndugu wa karibu waliokuzunguka wako fani gani, itakuwa rahisi wao kukuunganisha na rafiki zao wa fani hiyo utakapomaliza chuo

C. Fanya ufuatiliaji wa kina angalia matangazo ya ajira za serikalini, ni fani ipi inatangazwa kwa wingi au kwa unafuu?

Pointi zingine ntaongezea baadae au watu wengine watajazia.
 
Kama unataka ajira ya uhakika soma Agricultural Engineering au irrigation Engineering. Wahitimu wachache, vyuo vichache ajira kila mwaka.

Take your time ufanye uchambouzi wa soko la ajira ndani ya miaka 3-5. Anzia PSRP utapata data za kazi zinazotangazwa kila mwaka na kiasi cha wahitajika ujionee mwenyewe.

Huo ndio ushauri wangu. Takwimu hazidanganyi.
 
Kama unataka ajira ya uhakika soma Agricultural Engineering au irrigation Engineering. Wahitimu wachache, vyuo vichache ajira kila mwaka.

Take your time ufanye uchambouzi wa soko la ajira ndani ya miaka 3-5. Anzia PSRP utapata data za kazi zinazotangazwa kila mwaka na kiasi cha wahitajika ujionee mwenyewe.

Huo ndio ushauri wangu. Takwimu hazidanganyi.
Umemaliza
 
Chukua unachotaka kuchukua:
A. JKT ni upotevu wa muda, ratiba za jkt na kujiandikisha chuo na mikopo zinaingiliana sana utajikuta unakurupuka. Tulia (Ila usipumzike😂) fuatila kama ni chuo gani utaenda? Je mazingira utayaweza? Ukishajua chuo gani unaenda vitu vya kusoma vitajichuja

B. Angalia ndugu wa karibu waliokuzunguka wako fani gani, itakuwa rahisi wao kukuunganisha na rafiki zao wa fani hiyo utakapomaliza chuo

C. Fanya ufuatiliaji wa kina angalia matangazo ya ajira za serikalini, ni fani ipi inatangazwa kwa wingi au kwa unafuu?

Pointi zingine ntaongezea baadae au watu wengine watajazia.
Aende Jkt hawa wa sayansi wenye ufaulu mkubwa huwa wanabaki, wanawasomesha wenyewe
 
Wakuu mimi ni mkazi wa Lindi nimesoma PCM shule moja uboizini huko Mbeya na nimemaliza mtihani wa taifa siku chache tu zilizopita. Hapa bado nawaza niende JKT au nipumzike home hii miezi kadhaa

Kwa nilivyofanya mtihani najua nitapata Division 1 ya point 6 hadi 8.
Sasa kuna Jambo linanitatiza hususani kwenye hii era ambayo ajira hakuna. Naomba ushauri kwa JF Experts.
Vyuo ninavyotamani kusoma ni
  • University of Dodoma
  • Dar es Salaam Institute of Technology
  • National Institute of Transport
  • Dar es Salaam Maritime Institute
  • Mbeya University of Science and Technology
  • Muhimbili University of Health and Allied Sciences
UDSM na MUHAS napapenda ila nasikia cutting point zao ni kubwa Sana

Sasahivi walimu wetu wanatuambia kuwa Biomedical Engineering ina soko ila kama ukipata ufaulu chini ya Division 1 ya 5 hupati chance ya kusoma hiyo kozi

Kwa hiyo huwa nawaza sana nisome kozi ipi ambayo ina nafasi kubwa ya kupata ajira au kujiajiri at least ukilinganisha na kozi nyingine

Watu wengine wanasema Computer Engineering ina soko, hivi ni kweli wakuu au ndo tunaingizana cha kike?

Kozi nyingine ninazowaza ni
  • Mechanical Engineering
  • Automotive Engineering
  • Electrical Engineering
  • Chemical Engineering
  • Mechatronics Engineering
  • Telecommunications Engineering

Kweli napenda Engineering ila sijui hata ipi inahitajika kwa Bongo ipi haihitajiki. Nimesoma thread nyingine nyingi ila bado sijapata majibu. Kuna muda nawaza niachane na Engineering labda nisome Accounting and Finance au Agricultural Science pale SUA ila nahisi watu wa Accounting ni wengi sana. Ajira zitakuwa ngumu mbeleni (sijui ila ninahisi tu)

Au nisome "Mechanical Engineering" Halafu nikatafute kazi JWTZ maana walisema ni kozi adimu na inahitajika jeshini. Au sijui nisome Automotive Engineering kwenye magari au hata treni nione kama ina tija 🥲

Nikisikia na watu wa mtaani wanavyotutisha kuhusu maisha ya mtaani yalivyo magumu ndo nachanganyikiwa kabisa. Hizo habari zinafanya nakosea hadi raha. Au niende chuo nikasome kwa bidii sana nipate GPA kubwa nione kama naweza kuwa lecturer. Nawaza mengi ila bado Niko njia panda Sana.

Naombeni ushauri wakuu nikasome nini chuo. Kozi yoyote Ile nzuri yenye soko la ajira Tanzania hata kama ni ngumu fresh tu, kupiga msuli naweza maana nina hamu sana na ajira.
Naombeni mawazo yenu wakuu
Nenda DIT, piga IT, au, electrical,
Mdogo wangu ilibidi ujue mapema haya Mambo, mi nilipanga kusomea, uhandisi, nikiwa darasa, LA saba!
Kozi, yoyote,inakutoa, kwa, maisha, ya, sasa, hata, kama, una degree ya kitu Fulani, ongeza hata ujuzi wa kupiga picha, music production, kupiga, rangi,kuchomelea, kitu chochote cha ufundi we jifunze tu
 
Kama unataka ajira ya uhakika soma Agricultural Engineering au irrigation Engineering.
Wanangu wawili wamemaliza kozi hizo bado wapo mtaani wanahangaikia ajira mwaka wa tatu huu.

Siku hizi hakuna ajira iliyo wazi kwamba ukimaliza straight forward mzigoni.

Kozi yoyote unayosoma unasota kweli kweli halafu ukija mtaani unasota tena kupambania ajira.

Waulize madaktari kama kuna ajira za moja kwa moja siku hizi ndipo utapata majibu ugumu wa ajira ulivyo kwasasa.
 
Wakuu mimi ni mkazi wa Lindi nimesoma PCM shule moja uboizini huko Mbeya na nimemaliza mtihani wa taifa siku chache tu zilizopita. Hapa bado nawaza niende JKT au nipumzike home hii miezi kadhaa

Kwa nilivyofanya mtihani najua nitapata Division 1 ya point 6 hadi 8.
Sasa kuna Jambo linanitatiza hususani kwenye hii era ambayo ajira hakuna. Naomba ushauri kwa JF Experts.
Vyuo ninavyotamani kusoma ni
  • University of Dodoma
  • Dar es Salaam Institute of Technology
  • National Institute of Transport
  • Dar es Salaam Maritime Institute
  • Mbeya University of Science and Technology
  • Muhimbili University of Health and Allied Sciences
UDSM na MUHAS napapenda ila nasikia cutting point zao ni kubwa Sana

Sasahivi walimu wetu wanatuambia kuwa Biomedical Engineering ina soko ila kama ukipata ufaulu chini ya Division 1 ya 5 hupati chance ya kusoma hiyo kozi

Kwa hiyo huwa nawaza sana nisome kozi ipi ambayo ina nafasi kubwa ya kupata ajira au kujiajiri at least ukilinganisha na kozi nyingine

Watu wengine wanasema Computer Engineering ina soko, hivi ni kweli wakuu au ndo tunaingizana cha kike?

Kozi nyingine ninazowaza ni
  • Mechanical Engineering
  • Automotive Engineering
  • Electrical Engineering
  • Chemical Engineering
  • Mechatronics Engineering
  • Telecommunications Engineering

Kweli napenda Engineering ila sijui hata ipi inahitajika kwa Bongo ipi haihitajiki. Nimesoma thread nyingine nyingi ila bado sijapata majibu. Kuna muda nawaza niachane na Engineering labda nisome Accounting and Finance au Agricultural Science pale SUA ila nahisi watu wa Accounting ni wengi sana. Ajira zitakuwa ngumu mbeleni (sijui ila ninahisi tu)

Au nisome "Mechanical Engineering" Halafu nikatafute kazi JWTZ maana walisema ni kozi adimu na inahitajika jeshini. Au sijui nisome Automotive Engineering kwenye magari au hata treni nione kama ina tija 🥲

Nikisikia na watu wa mtaani wanavyotutisha kuhusu maisha ya mtaani yalivyo magumu ndo nachanganyikiwa kabisa. Hizo habari zinafanya nakosea hadi raha. Au niende chuo nikasome kwa bidii sana nipate GPA kubwa nione kama naweza kuwa lecturer. Nawaza mengi ila bado Niko njia panda Sana.

Naombeni ushauri wakuu nikasome nini chuo. Kozi yoyote Ile nzuri yenye soko la ajira Tanzania hata kama ni ngumu fresh tu, kupiga msuli naweza maana nina hamu sana na ajira.
Naombeni mawazo yenu wakuu
Ungekuwa na hela ungetafuta chuo duniani kinachotoa degree ya blockchain technology na issue za cryptocurrency maana ndipo uelekeo dunia ilipo.
kama hiyo option ya 1 ngumu kuwezekana ningekuwa wewe ningesoma computer science/engineering baadae ningesoma hizo field nilizomention hapo juu plus cyber security
 
Hii inaonesha jinsi Gani familia na watanzania tulivokuwa hatuna maono Wala mwelekeo wa maisha.

Hadi unaenda PCM ulikuwa hujui unataka kusoma kitu Gani au kuwa nani?. Sad!!

Kuna haja ya kuwa na carrier counselling mashuleni.

For me, Tele au Computer engineering inafaa (cyber security)

Kutokana na Dunia inakoenda.

All in all, there must be an inner voice that talks to you about a certain course, please listen to it and go for it, because that is where your destiny will shine. Huku kwingine na maushairi utapoteana Bure mdogo wangu.
 
Kama unataka usiangaike na ajira means hata ukitoka chuoni unaweza kupata sehemu ya kujishikiza kasome electrical engineering hii ukiwa nayo Mtaani huwezi lala njaa!! Lakini kama unataka kusubiri mpaka ajira soma mechanical engineering au Mechatronics engineer hizi kozi Zina soko japo Kuwa watu ni wengi sana so competition ni kubwa mno unaweza ukasota mno.

Kuhusu Biomedical engineering hii course naweza kusema ni course ambazo zimeletwa kisiasa kama zile sijui Petroleum engineer, Marine engineer Bsc. Of Biological nk ni course kwa Bongo hapa hazina access za ajira zimeletwa kwa Siasa za bongo tu lakini upatikanaji wake wa ajira ni mgumu sana hata upande wa masomo yake kwa vitu vingi hamfundishwi mnakula theory kwa sababu hamna vifaa vya kutosha.

Kwa Tanzania course ambayo Ina ajira ambayo ukimaliza unaenda Moja Kwa Moja kufanya kazi na unaajiriwa ni Aircraft Engineering hii inatolewa pale NIT ada yake ni 6M kama upo vizuri kasome hii kozi maana ajira zake ni uhakika Asilimia 100.

Point to note: unapo chagua course zingatia chuo mfano kwa upande wa Engineer DIT is the best lakini mazingira yake ya kuishi ni magumu mno. kwa DSM chuo ambacho mazingira yake ni mazuri kwa kuishi na Elimu yake ni nzuri ni NIT tu huko utapata vyumba vya kupanga misosi kwa 1000 tu unakula unashiba tofouti na vyuo vingine.

Kila la kheri.
 
Ukisoma kozi kwa sababu ina soko utakuja kupata nsobgo wa mawazo baadae. Hizo kozi unasema zina soko leo fikiria miaka 4 au mitano baada ya wewe kumaliza chuo. Je zitaendelea kuwa na soko? Bila shaka soko linakuwa limebadilika.

Nadhani swala la muhimu ni kuangalia passion yako na utayari wa wewe kuitumia hiyo kozi maishani. Suala la Ajira linabadilika sana. Kuna kipindi niko sekondari Telecom Ilikuwa kozi matata sana. Lakini namaliza form six ikawa Petroleum, ila tulipomaliza chuo waliosoma petroleum wakjikuta mtaani
Duh ni kweli.... Huenda 4 years to come Biomedical Engineering itakuwa haina soko tena
 
Kasome Civil engineering
Hii si Ndio mpaka mwenyewe ujiajiri na mtaji inabidi uwe mkubwa sana. Watu wanatuambia hapo ndo ugumu wake ulipo
Miradi mingi tenda wanapewa Chinese engineers kuliko African engineers
 
Chukua unachotaka kuchukua:
A. JKT ni upotevu wa muda, ratiba za jkt na kujiandikisha chuo na mikopo zinaingiliana sana utajikuta unakurupuka. Tulia (Ila usipumzike😂) fuatila kama ni chuo gani utaenda? Je mazingira utayaweza? Ukishajua chuo gani unaenda vitu vya kusoma vitajichuja

B. Angalia ndugu wa karibu waliokuzunguka wako fani gani, itakuwa rahisi wao kukuunganisha na rafiki zao wa fani hiyo utakapomaliza chuo

C. Fanya ufuatiliaji wa kina angalia matangazo ya ajira za serikalini, ni fani ipi inatangazwa kwa wingi au kwa unafuu?

Pointi zingine ntaongezea baadae au watu wengine watajazia.
Shukrani nitajitahidi kufuatilia ndani ya kipindi hiki
 
Aende Jkt hawa wa sayansi wenye ufaulu mkubwa huwa wanabaki, wanawasomesha wenyewe
Nilikuwa nawaza hivyo ila juzi niliona taarifa ya habari wanasema "VIJANA WALIOHITIMU JKT WAPEWA SOMO WAACHE KUTEGEMEA KUAJIRIWA JWTZ BADALA YAKE WAJITEGEMEE"
Hii habari ikanitisha kidogo kuwa huenda imekuwa kero huko JKT kila mtu anataka kubaki hadi JKT inaamua kuingilia kati kuwatoa matumaini hayo
 
Back
Top Bottom