Nisipokuambia wewe nimuambie nani?

Nisipokuambia wewe nimuambie nani?

mahirtwahir

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2013
Posts
614
Reaction score
322
Miaka 7 iliopita nilikua na mahusiano ya kimapenzi na msichana 1 kwa hakika alionekana kunipenda tofauti na ninavyompenda mimi lengo lilikua ni kumuoa ila alipoona nachelewa basi alikubali kuolewa na mtu mwengine sijui kwa nini?

Baada ya maandalizi ya ndoa aliniambia kua anaolewa niliumia kiasi ila sikujali sana akaniomba mchango wa harusi nilimpa pesa ambazo alishangaa kwani hakutarajia.

Baada ya ndoa na mwezi kupita malalamiko yakaanza ooooooh mume wangu hanipi raha kama zile za kwako maraaa naishi nae ila simpendi ooooooh nataka niachike kwa kweli lawama zilikua nyingi mi nikawa namshauri kumvumilia kwandi ndio mume wake na ni mwili mmoja kwa sasa anamimba ya miezi 3 amevimba miguuu anaumwa umwa kila siku , na shida kwake haziishi mara nimpe hela ya kula mume wake amempa pesa finyu mara anaumwa hana hela ya matibabu hapiti mwenzi bila ya kunitangazia shida ninapomuambia sasa mume wake ndio anajukumu la kumuhudumia na sio mimi basi ananuna na kusema kua asiponiambia mm shida zake amuambie nani?

Kwa kweli nashindwa kumuelewa yeye na mume wake wanaishije ?

Naombeni ushauri hii mizinga nimeichoka
 
Wewe, acha kuharibu ndoa ya watu, anchana na huyo binti.

anajuaje! kwamba anayokuambia ni kweli.?
 
Acha wenge wewe kila siku kutuletea stori za uongo...

25 Machi 2014

https://www.jamiiforums.com/mahusia...aaada-jamani-ndoa-iko-hatarini-kuvunjika.html

Habari wana wakubwa

Kwa kweni nakuja mbele yenu kutaka msaada niko na mke wangu mwaka wa 8 sasa na tumebahatika kupata watoto 2 wa kike na wa kiume.
...........

Leo

Miaka 7 iliopita nilikua na mahusiano ya kimapenzi na msichana 1 kwa hakika alionekana kunipenda tofauti na ninavyompenda mm lengo lilikua ni kumuoa ila alipoona nachelewa basi alikubali kuolewa na mtu mwengine sijui kwa nini?
 
toa sadaka 2! si mbaya tena akikuomba laki zidisha mara tatu... utabarikiwa
 
Kijana,hujui kumpa hela mke wa mtu bila sababu ya msingi ni hatari?

Achana na mke wa mtu na kuwa mkali ili mazoea yaishe,unamzoea hivyo mke wa mtu ......!!!!!!!!!!!!???????????????????

Acha utoto dogo ....!!
 
Afu ukimsoma vizuri unakuta anademand kitu indirect hapo.

Udomo zege imekua janga la taifa!!!!!


Ngoja tumsaidie kulainisha mdomo, single ladies wooooote jf, this guy is akchuale free! Come one come all and pick him up.
 
Back
Top Bottom