Nishikeni mkono wadau naanguka

Nishikeni mkono wadau naanguka

MBEBA MAONO KAJA

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2013
Posts
365
Reaction score
195
Ndugu wanajamii.

Nimevumilia sana hatimae nimeona kuwa mficha ugonjwa mauti umuumbua na yamkini aliegundua ngazi alikuwa ni mfupi wa kimo. Nasema hayo kwa kuzingatia hali yangu ya maisha inavyozidi kudidimia kadri siku zinavyoenda kutokana na ukosefu wa ajira rasmi na hata mtaji wa kujiajiri.

Mimi ni msichana mwenye shahada ya fedha na uhasibu niliyoipata mwaka 2012. Kwakweli nimejitahidi kuomba kazi sehemu mbali mbali na kufanikiwa kupata kazi ambazo kihakika hazijawa msaada kwangu ikizingatiwa kuwa nina majukumu ya kulea wadogo zangu baada ya mzazi kutoweka.

Ombi langu kwenu wanajamvi, mnisaidie kupata kazi katika taasisi yoyote ya umma au binafsi ambayo no sustainable niweze kuokoa wadogo zangu kielimu, lakini pia hata kama mnaweza kunisaidia namna gani nipate mtaji nina uwezo pia wa kufanya na kusimamia mradi. Nimependelea taasisi ambayo ni sustainable kwasababu nimefanya kazi na taasisi binafsi ambayo ilikufa baada ya miezi sita kutokana na ubadhilifu hivyo kuniathiri sana.

Natanguliza shukrani.
 
Da ndugu kweli kazi ipo, yaani wewe chuo umemaliza 2012 halafu bado unakulia lia huku, wakati kuna watu humu toka 2010 na wanatafuta hata sehem ya kujishikiza tu wapate ujuzi hawapati tafadhali ndugu mshukuru Mungu kwa upendeleo anaokupa mpaka sasa hivi, 2012 tayari unapata kazi though hazikulipi vizuri still ni good opportunity, tatizo ni kwamba haiwezi kutimiza mahitaji ya ndugu au wadogo zako hio nafikiri sio sawa wewe toka ulipomaliza chuo mpaka sasa hivi hautaweza make hela ya maana sana kutokana na experience bado huna kwa hio hizo kazi ndio bridge ya kukupa experience ili baadae uweze lipwa hela nzuri, sasa hivi we chakuomba ni muumba uendelee kupata hizo work experience na kupata hela kidogo ya chakula, hivyo vingine vitakuja tu, tatizo mtoto wa kike hizo haraka za mihela ya fasta itakuweka pabaya especially hizo PM humu kuna midudu imetega midomo kama mamba wakisubiri watoto wakike kama wewe watakula hio papuchi ya sasa hivi wakupe na zawadi ya ka HIV
 
Ndugu wanajamii,
nimevumilia sana hatimae nimeona kuwa mficha ugonjwa mauti umuumbua na yamkini aliegundua ngazi alikuwa ni mfupi wa kimo.
nasema hayo kwa kuzingatia hali yangu ya maisha inavyozidi kudidimia kadri siku zinavyoenda kutokana na ukosefu wa ajira rasmi na hata mtaji wa kujiajiri.
Mimi ni msichana mwenye shahada ya fedha na uhasibu niliyoipata mwaka 2012 .
kwakweli nimejitahidi kuomba kazi sehemu mbali mbali na kufanikiwa kupata kazi ambazo kihakika hazijawa msaada kwangu ikizingatiwa kuwa nina majukumu ya kulea wadogo zangu baada ya mzazi kutoweka.
ombi langu kwenu wanajamvi, mnisaidie kupata kazi katika taasisi yoyote ya umma au binafsi ambayo no sustainable niweze kuokoa wadogo zangu kielimu.lakini pia hata kama mnaweza kunisaidia namna gani nipate mtaji nina uwezo pia wa kufanya na kusimamia mradi.
nimependelea taasisi ambayo ni sustainable kwasababu nimefanya kazi na taasisi binafsi ambayo ilikufa baada ya miezi sita kutokana na ubadhilifu hivyo kuniathiri sana .
natanguliza shukrani.

only trust in GOD and believe him....bz ktk maisha kila mtu ana mda wake na wakati wake wa kufanikiwa haijalishi umewahi au umechelewa.....IMEANDIKWA AMELAANIWA AMTEGEMEAYE MWANADAMU NA KUMFANYA KIMBILIO LAKE.....
 
Pole na changamoto dadangu cha msingi ni maombi kingine unaweza kujiunga na businesss ya forever living ukaongeza kipato dadaangu kwa kuanzia mtaji wa laki 3 tu unaweza kunipm kama utakuwa interested na business uweze kuongeza kipato
 
Usije mtegemea mtu kua ndie atakae kutoa katika maisha yako...
 
amini usiamini UTAISHIA KUAMBIWA NI PM ALAFU UTATOA NAMBA, NA KUAMBIWA UTUME CV AU MUONANE MWISHOWE UTAANZA KUOMBWA KITUMBUA...

Mpenzi Aminata Una visa kweli kweli, nilitaka nimtumie PM apeleke CV mahali lakini sasa, dah!
 
Usikate tamaa mazuri yanakuja yote yasiyo na mpango hujichunja
 
Aisee tutaanza kuziogopa PM sasa, maana inaonekana ni mtego wa HIV
 
Pole na changamoto dadangu cha msingi ni maombi kingine unaweza kujiunga na businesss ya forever living ukaongeza kipato dadaangu kwa kuanzia mtaji wa laki 3 tu unaweza kunipm kama utakuwa interested na business uweze kuongeza kipato

matatizo ya wenzenu nyie mnageuza business opportunity,unataka umpeleke wakulipe commission sio?,shame on you!!!!
 
MUNGU akujalie upate kazi mapema kabisa,endelea kusali na utafanikiwa all the best
 
Usiache kumuomba mungu ipo cku atakuinua coz anajua wewe ndo kiungo cha familia ana namna ya kukuinua!
 
Elimu ya juu lengo lake kuu ni kukupa uwezo wa kupambanua jambo hasa maisha,elimu ya juu tanzania ni kufaulu mitihani na kuajiriwa,hilo ni tatizo na janga la kitanzania.
Dada kama upo dar nenda udsm kuna darala la ujasiriamali pale UDEC,litakujenga na kubadili mtazamo wako juu ya ajira na kipato kwa ujumla.
kama upo nje ya Dar ni PM ntakushauri zaidi.
Ndugu wanajamii.

Nimevumilia sana hatimae nimeona kuwa mficha ugonjwa mauti umuumbua na yamkini aliegundua ngazi alikuwa ni mfupi wa kimo. Nasema hayo kwa kuzingatia hali yangu ya maisha inavyozidi kudidimia kadri siku zinavyoenda kutokana na ukosefu wa ajira rasmi na hata mtaji wa kujiajiri.e

Mimi ni msichana mwenye shahada ya fedha na uhasibu niliyoipata mwaka 2012. Kwakweli nimejitahidi kuomba kazi sehemu mbali mbali na kufanikiwa kupata kazi ambazo kihakika hazijawa msaada kwangu ikizingatiwa kuwa nina majukumu ya kulea wadogo zangu baada ya mzazi kutoweka.

Ombi langu kwenu wanajamvi, mnisaidie kupata kazi katika taasisi yoyote ya umma au binafsi ambayo no sustainable niweze kuokoa wadogo zangu kielimu, lakini pia hata kama mnaweza kunisaidia namna gani nipate mtaji nina uwezo pia wa kufanya na kusimamia mradi. Nimependelea taasisi ambayo ni sustainable kwasababu nimefanya kazi na taasisi binafsi ambayo ilikufa baada ya miezi sita kutokana na ubadhilifu hivyo kuniathiri sana.

Natanguliza shukrani.
 
Kila mtu analia na maumivu yake tu,na kuna watu wana shida kuliko zako hizo dada,afadhali unapo hata pakushika. Mtukuze MUNGU kwa hilo,na kesho ni majaaliwa yake.
 
Kuna jamaa yangu anaendesha hotel & bar anatafuta mhasibu baada ya aliyekuwepo kumuibia. Je wewe unaweza kufanya kazi hiyo? Pili je unaishi sehemu gani ili nikuelekeze sehemu ya kupeleka appilication yako?
 
Naomba unipe taarifa kuhusu utaratibu wa UDEC hizo entrepreneurship course zinakuwaje
 
pole sana mamito

ila kuwa makini na watu watakojiokeza kukusaidia
MTEGEMEE MUGU ZAID tupo wengi ambao hatuna kazi
 
God z great mdada muombe mungu utafanikiwa tu hayo ni majaribu tu so jipe moyo utayashinda.
 
Back
Top Bottom