mwehu mwanaume huyo
ninaye jirani yangu mahali ninapoishi kanijia na kisanga kilichomkuta,in short amekuta meseji za mapenzi kwenye simu ya mumewe na baada ya kufanya uchunguzi akagundua kuwa ni kweli mumewe alikuwa na mahusiano na mwanamke mwingine, mume akukubali na msamaha kaomba., ndoa yao ni changa miaka 2, bibie jirani yangu nimejaribu kumshauri atulize moyo konde amssamehe mumewe anasema amechoka kwani hii si mara ya kwanza kwa mume huyo kucheat amekuwa akimcheat hata kabla hawajaoana na bwana amekuwa akiomba msamaha lakini baada ya muda anarudia tena, sasa anachodai bibie amechoka kuvumilia maana hivyo vitendo vinamkwaza kiasi kwamba mapenzi kwa huyo bwana yamepungua sana hata ila hamu ya ku-do na mumewe imeikwisha.., kwa sasa wanalala mzungu wa nne! jamani wandugu nipeni mawazo niweze kumuelimisha huyu dada aokoe ndoa yake namwonea huruma ni mdogo to call the marriage off!!!!!!
Daaa pole yake huyo dada, lakini kabla sijajitaidi kushauri chochote, kuna kitu nakiona huyu dada alikosea kukiangalia kwa makini kabla ya kuamua kufunga ndoa na huyo kaka.
Alishamuona tangu mwanzo kwamba yeye sio mwaminifu, na sio mara moja kwa nini alikubali kuolewa nae? Ilitakiwa ajipime moyoni mwake tangu mwanzo kama anaweza akuchukuliana na hiyo tabia ya mume wake.
Kama alimuona sio mwaminifu tangu mwanzo na akajiona anaweza kuibeba hiyo tabia akamsamehe basi na ajitaidi kuivumilia huku akimshauri kwa upendo labda atajirekebisha.
Lakini swali kubwa hapa Kwa nini alimkubali mtu mwenye tabia mbaya kama hio ya kukosa uaminifu kwenye mahusiano hata kabla ya kufunga ndoa???
Daa tusubiri na wengine washauri lakini nasikitika kwa uamuzi wa huyu dada kukubali ndoa na mtu mwenye tabia ambayo hawezi kuibeba. Wanawake sa ingine inabidi tufikirie vizuri.
si mara ya kwanza kwa mume huyo kucheat amekuwa akimcheat hata kabla hawajaoana
nalazimika kuamini ni ngumu kumbadilisha mtu tabia mkiwa tayari mshaoana.
Avumilie tu, maana hadi kuingia kwenye ndoa ina maana alishakubaliana na tabia ya jamaa maana aliijua kabla.
kwani kama ammemcheat ndo kamwambia hampendi?
hivi huwa mnatucheat huku bado mnatupenda eeh?
hehehehe...ukweli mweupe ndo huo...kucheat ni jambo moja, kupenda jambo jengine kabisa...muulize mwalimu wako wa Praktiko Klorokwini, na principle yake ya seriousness kwenye life...hahahahaha
aaah!
Mwalimu yupo kwenye sredi fulani kuleee. Ila ananiboa boa. Lol!
Nitamsemea kwa mwalimu mkuu.