Nishaurini tafadhali

I dont see the problem now! Kama aliijua hiyo tabia ya mumewe kabla hawajaoana, why safer? anatakiwa ajue kwanini mumewe amekua ikicheat marakwa mara. halafu funny enough hili njemba likibanwa mbavu linakili makosa. Hapo dada yangu aliloliunganisha Mungu mwanadamu hawezi kutenganisha (yeye alijua kabla hizo tabia) Akaechini na mumewe, asipanic, amuulize mumewe in friendly manner ni kitugani hasa anakikosa kwake, asifanye ikawa kesi (hakuna anayependa kushindwa kesi)
 
ninaye jirani yangu mahali ninapoishi kanijia na kisanga kilichomkuta,in short amekuta meseji za mapenzi kwenye simu ya mumewe na baada ya kufanya uchunguzi akagundua kuwa ni kweli mumewe alikuwa na mahusiano na mwanamke mwingine, mume akukubali na msamaha kaomba., ndoa yao ni changa miaka 2, bibie jirani yangu nimejaribu kumshauri atulize moyo konde amssamehe mumewe anasema amechoka kwani hii si mara ya kwanza kwa mume huyo kucheat amekuwa akimcheat hata kabla hawajaoana na bwana amekuwa akiomba msamaha lakini baada ya muda anarudia tena, sasa anachodai bibie amechoka kuvumilia maana hivyo vitendo vinamkwaza kiasi kwamba mapenzi kwa huyo bwana yamepungua sana hata ila hamu ya ku-do na mumewe imeikwisha.., kwa sasa wanalala mzungu wa nne! jamani wandugu nipeni mawazo niweze kumuelimisha huyu dada aokoe ndoa yake namwonea huruma ni mdogo to call the marriage off!!!!!!

Aondoke tuu ataingia mwingine. Alipogundua si mwaminifu kabla ya kuoana kwanini hakufanya uamuzi? Kama alikubali boga atakataa ua lake? Yeye cha maana ajitafiti nini mumewe anapata kwa wanawake wa nje na nini anakosa kwake? Meseji si ushahidi wa udhinifu, watu hutaniana kwenye meseji. Wanawake wengi hawajiamini wanaona kama ilitokea mwujiza yeye kuolewa na huamini kuna wengine wakati si kweli
 
kama aligundua ni cheater hata kabla ya kuoana akajipa moyo, wakaoana hiyo mbinu ai2mie ktk kutoa limsamaha, waendelee na maisha
 
Daaa pole yake huyo dada, lakini kabla sijajitaidi kushauri chochote, kuna kitu nakiona huyu dada alikosea kukiangalia kwa makini kabla ya kuamua kufunga ndoa na huyo kaka.

Alishamuona tangu mwanzo kwamba yeye sio mwaminifu, na sio mara moja kwa nini alikubali kuolewa nae? Ilitakiwa ajipime moyoni mwake tangu mwanzo kama anaweza akuchukuliana na hiyo tabia ya mume wake.

Kama alimuona sio mwaminifu tangu mwanzo na akajiona anaweza kuibeba hiyo tabia akamsamehe basi na ajitaidi kuivumilia huku akimshauri kwa upendo labda atajirekebisha.

Lakini swali kubwa hapa Kwa nini alimkubali mtu mwenye tabia mbaya kama hio ya kukosa uaminifu kwenye mahusiano hata kabla ya kufunga ndoa???

Daa tusubiri na wengine washauri lakini nasikitika kwa uamuzi wa huyu dada kukubali ndoa na mtu mwenye tabia ambayo hawezi kuibeba. Wanawake sa ingine inabidi tufikirie vizuri.

Yaani wewe umeiba mawazo yangu yote muone kwanza, sasa huyu LD tusemeje kagongwa au kafanyajwe???
 
si mara ya kwanza kwa mume huyo kucheat amekuwa akimcheat hata kabla hawajaoana

nalazimika kuamini ni ngumu kumbadilisha mtu tabia mkiwa tayari mshaoana.
Avumilie tu, maana hadi kuingia kwenye ndoa ina maana alishakubaliana na tabia ya jamaa maana aliijua kabla.
 
nalazimika kuamini ni ngumu kumbadilisha mtu tabia mkiwa tayari mshaoana.
Avumilie tu, maana hadi kuingia kwenye ndoa ina maana alishakubaliana na tabia ya jamaa maana aliijua kabla.


eti eeh,,nashangaa, hata miye, kwamba aliingia akijua kabisa

Au ndo ile mtu kuwa desparate na ndoa? Then hiyo ndo opportunity cost yake....akubali kuishi tu na hiyo cost sana sana kama ulivosema avumilie sidhani kama tunaweza kumshauri kingine

by the way, kwani kama ammemcheat ndo kamwambia hampendi?
 
Mimi suala la kuachana siliungi mkono kabisa. Sasa ataacha wanaume wangapi? Wanaume wote ndio walivo kwa bahati mbaya huyo alikamatwa. Atamuacha huyo mumewe leo, kesho ataenda kwa mwingie, mlevi na mpigaji, atamuacha huyo ataenda kwa mwingine mara ataambiwa ni shoga...!

Jamani msimshawishi mwenzenu aachane na mumewe...! Mwanaume kukamatwa ana cheat sio jambo geni katika jamii yetu kwa sasa, haya mambo yanaweza yakazungumzwa na yakaishia kimya kimya ndani ya nyumba kwa kushirikisha watu wenye busara. Lasivyo huyo dada anaweza kuondoka kwa muda ili akapunguze hasira then anaweza akarudi tena kwa mumewe.

Tusitumie hisia, hasira au kinyongo katika kushauri watu, tutumie busara na hekima tunapowashauri watu katika mambo kama haya.
 
Huyo shoga yako kwa nini apekenyue cm ya mumewe, kama anataka ndoa yake idumu aache kushika simu ya mume
 
hivi huwa mnatucheat huku bado mnatupenda eeh?


hehehehe...ukweli mweupe ndo huo...kucheat ni jambo moja, kupenda jambo jengine kabisa...muulize mwalimu wako wa Praktiko Klorokwini, na principle yake ya seriousness kwenye life...hahahahaha
 
Huyo bibie akae chini na mume amuulize tatizo ni nini la yeye kufanya hvyo?na pia kama aliweza kuvumilia
mpaka ndoa basi ajitahidi kuvumilia huenda ikawa yeye,huyo ndio Mungu kampa ambadilishe kwahiyo
ajaribu kila awezavyo kuokoa ndoa yake kwani hapo sidhan ikama kuachana ndo solution,hapana ndoa yahitaji uvumilivu
na ni kitu ambacho vijana wengi hatuna na ndio maana ndoa za siku hizi huvunjika kwa kukosa uvumilivu,mbona
enzi za wazazi wetu walikuwa wavumilivu mno katika ndoa zao?
 
hehehehe...ukweli mweupe ndo huo...kucheat ni jambo moja, kupenda jambo jengine kabisa...muulize mwalimu wako wa Praktiko Klorokwini, na principle yake ya seriousness kwenye life...hahahahaha

aaah!
Mwalimu yupo kwenye sredi fulani kuleee. Ila ananiboa boa. Lol!
Nitamsemea kwa mwalimu mkuu.
 
Nadhani wamtafute mshauri nasaa (counsellor) inawezekana mme wake ni sex addict, au kuna mambo yanaenda ndivyo sivyo kati yao. Sasa wakiongea na professional kila mtu kwa muda wake baadae wote pamoja anaweza akawasaidia kuwambia tatizo liko wapi in a professional manner. Mimi na wewe ni vigumu kushauri kwani tutaingiza personal experiences na interests. Kama msemavyo aliolewa na cheater, well, may be there are ways of changing those cheaters. Hamjawahi kusikia jamaa toka ameoa katulia. Aah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom