Nisamehe Rais wangu Magufuli

Nisamehe Rais wangu Magufuli

Nimeiona hii picha nimelia sana hadi muda huu machozi yananilengalenga hadi nashindwa kuona vizuri herufi kwenye keyboard.Nikikumbuka namna nchi inavyoharibiwa na kuuzwa Kwa waarabu ambao ni kichaa pekee anaweza kukubali hayo matwakwa yao.pumzika Kwa amani mzalendo.ulisema kweli tutakukumbuka
 
Hakuna lolote, Rais asiyetoa ansurance ya usalama wa wananchi wake hata wale wanaomkosoa basi huyo hafai hata kidogo.

Bora ulale njaa ila una uhakika wa haki ya kuishi.
Kanyima haki za kuishi kwa baadhi ya watu ambao hatunao leo.

Apumzike anapostahili.
 
Wewe unajisemea upande wako mkuu, ambao ni upande wa Magufuli. Kuna "wala Bata" ambao hawasikii lolote kuhusu mtu wao huyo, hata kama huwasikii mara kwa mara. Akina JK hadi leo wanao wafuasi, usisahau.

Ngoja nisiondoke bila kukupa ushauri huu.
Ni vizuri kumkumbuka kiongozi mliyeona anafanya kazi nzuri kwa maoni yenu. Hiyo haitoshi, hasa katika wakati huu.
Kumuenzi kiongozi wenu ni kufanya juhudi ya kuondoa yale mnayoona kiongozi huyo hakuyapenda. Ni jukumu lenu sasa kujipanga kuhakikisha kuwa haya msiyoyapenda yaondoke haraka. Haitoshi kubaki mnalalama tu na kumlilia kiongozi. Lindeni 'legacy' yake kwa kuhakikisha aliyokuwa akiyasimamia hayavurugwi kama yanavyovurugwa sasa hivi.
Anzieni kampeni zenu huko ndani ya chama chenu.
Any chama gani unaongelea maana mie niko chamaless
 
Nimeiona hii picha nimelia sana hadi muda huu machozi yananilengalenga hadi nashindwa kuona vizuri herufi kwenye keyboard.Nikikumbuka namna nchi inavyoharibiwa na kuuzwa Kwa waarabu ambao ni kichaa pekee anaweza kukubali hayo matwakwa yao.pumzika Kwa amani mzalendo.ulisema kweli tutakukumbuka
Kama zingekuwepo hata barua kwenda Mungu walu ningemwambia jinsi hawa viongozi uchwala wanavyo iharibu yoyote aliunda upya jembe letu na kumnoa jembe ambaye akija atafyeka wala rushwa zaidi ya kim jong
 
Mimi ni kati ya Watanzania ambao tulikuwa hatukuelewi kipindi ukiwa hai. Ni kweli, kama mwanadamu ulikuwa na mapungufu yako. Lakini jambo moja ni hakika, uliipenda Tanzania na Watanzania kwa moyo wako wote.

Kila nikisikiliza ule wimbo wa Msechu huwa ninatokwa na machozi. Pumzika kwa amani Rais Magufuli. Hakika tunakulilia kama ulivyosema tutakukumbuka kwa mema yako.
"Na Mimi nataka niseme Watanzania mtanikumbuka na mtanikumbuka kwa mazuri na si kwa mabaya kwasababu nimesacrifice maisha yangu kwa wananchi masikini"
 
Hayo yote unayoeleza watu wameyasikia tokea Magufuli akiwa hai ila bado watu wanamkumbuka Magufuli. Athari za mapungufu ya Samia ziko wazi na zinawagusa watu kiuhalisia kuliko mengi yaliyoelezwa kuhusu Magufuli.
Kama yapi? Taja moja tu
 
Wahuni wameshika Hatamu.
Wale walioitwa Washamba wamewekwa kando.
Wakati wa maongezi ya simu yaliyovuja wale wazee walisema; "anajua, ndio maaana anaogopa kuja Dar"! Unadhan alikua anaogopa nini hicho!

Ni kupigwa matukio kila upande kama vile hatuna tena kesho
 
umeanza kuwasikia toka akiwa hai hadi leo ila kadri siku zinavyosogea watu wanazidi kumkumbuka Magufuli halafu wewe bado unazungumzia kufichua maovu? Wewe kweli
Nini kukumbukwa?. Kwani Iddi Amini na Mobutu hawakumbukwi? Au Adolph Hitler na Benito Mussolini hawakumbukwi?

Suala unakumbukwa kwa kitu gani. Mimi nitamkumbuka Magufuli kwa kujenga Airport kijijini kwake na sasa imebaki useless kama Gbadolite ya Mobutu. Nitamkumbuka pia kwa kutuma kikosi cha Makonda kwenda kumshambulia Tundu Lissu.

Na nyie wajinga mna yenu ya kumkumbuka
 
Wewe mburura nenda kwanza kajiandikishe MEMKWA ili ukiandika tukuelewe. "Kupiga kula" ndiyo nini?

Mtu wa Darasa la 7 B, ukija JF utajidhalilisha tu, bakia Facebook tu kwa wajinga wenzio
Sasa we naona unakuwa mjuaji huku ulisoma chechea mkondo D
 
Back
Top Bottom