Dah, ingawa mimi si muumini wa kusave wapenzi kwa majina ya baby na sweety ( phone book yangu yote kila mtu ameseviwa kwa jina lake halisi including mpenzi wangu ), ila jamaa alichokifanya siyo fair. Afadhali ungekuwa umesave jina la kueleweka, eti ukasave mzinguaji.
It is not fair, ingawaje naye hakutakiwa kupanic alivyopanic, kwa msichana mwenye uelewa ilipaswa akuulize kwa nini umemsave hivyo. Angechukua maelezo yako kisha angepima.
Kwa mwanamke aliyekomaa kiakili, kama jibu lako lingekuwa halijamridhisha, mchezo angekupa, ila baada ya hapo kibao kingegeuka yangeweza kuwa kati ya haya: Either ndo ungekuwa mwisho wenu, ama ndo ingekuwa mwanzo wa yeye kukuzingua na kubeba dhima ya uzinguaji hawa kama ulivyomuita.
Kwa bahati mbaya mlikutana nyote akili hazijatengemaa.
Wahenga walisema (hawa ni wahenga wazungu ) "Experience is a good teacher". Next time naamini hutofanya uliyoyafanya.