Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,190
- 34,526
NISAMEHE MPENZI
Mtunzi:Juma Hiza
0712988278
Hali ya hewa ilikuwa shwari katika jiji la Daresalaam. Ndani ya chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kilichokuwepo maeneo ya Posta mtaa wa Shaaban Robert, msichana mrembo aliyejulikana kwa jina la Evelyne alionekana akitoka darasani huku akiwa anakimbia, machozi yalikuwa yakimdondoka kwa wakati huo.
“Evelyne! Evelyne! Evelyne,” ilisikika sauti ya msichana mwingine ambaye alikuwa akimfuata nyuma Evelyne baada ya kutoka darasani.
Evelyne aliongoza moja kwa moja mpaka kwenye kimbweta, alipofika hapo aliketi na kuanza kulia huku akiwa amejiinamia.
“Evelyne kuna nini mbona sikuelewi?” aliuliza msichana huyo aliyekuwa akimfuata nyuma Evelyne, alionekana kutoelewa chochote kilichokuwa kikiendelea kwa wakati huo.
“Hapana Happy siwezi kuendelea kuwa eneo hili acha niondoke zangu,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio cha kwikwi.
“Unaondoka unaenda wapi sasa na wakati darasani kuna kipindi?” aliuliza Happy huku akimtazama Evelyne ambaye aliendelea kulia muda wote huo.
“Narudi zangu nyumbani,” alijibu Evelyne.
“Unajua sikuelewi Evelyne,” alisema Happy lakini kabla ya Evelyne kumjibu lolote aliinuka na kuondoka eneo hilo la chuo, Happy alibaki akimtazama Evelyne huku asijue ni nini kilichokuwa kikiendelea.
Evelyne na Happy walikuwa ni marafiki wakubwa sana katika chuo hicho, walikuwa wakisaidiana mambo mengi sana, walishiriki kusaidiana katika masomo na hata katika mipango yao ya kimaisha pia walishirikishana. Happy alikuwa akimfahamu vyema rafiki yake huyo tangu walipoanza kusoma katika chuo hicho mpaka kufikia mwaka wao wa mwisho wa Degree ambao ndiyo walikuwa wameubakiza. Walikuwa wakisomea Uhasibu.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, Happy alikifahamu na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Happy, Evelyne naye alikifahamu, kwa kifupi walikuwa ni marafiki waliyoshibana. Walikuwa wakiishi pamoja katika chumba kimoja walichokuwa wamepanga maeneo ya Kigamboni.
Wakati Happy akiwa bado amesimama eneo lile ghafla! aliisikia sauti ya kiume ikimuita nyuma yake, haraka aligeuka na kukutana na mtu aliyekuwa akimuita. Alikuwa ni Richard.
“Niambie Shem.”
“Poa tu! vipi mbona Evelyne ametoka darasani kuna nini?”
“Sijui.”
“Yuko wapi?”
“Ameondoka, ameniambia anarudi nyumbani hawezi kuendelea kuwa eneo hili.”
“Mbona unanichanganya?”
“Richard kwani kuna kitu gani kimetokea kati yenu?”
“Hakuna kitu.”
“Mbona sasa Evelyne amebadilika ghafla! baada ya kukuona.”
“Mimi mwenyewe sielewi chochote.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo Happy inamaana huniamini?”
“Nakuamini sana,” alijibu Happy.
Richard alikuwa ni mvulana aliyekuwa akitokea katika familia ya kitajiri sana, alikuwa ni mtanashati, mwenye mwili uliyojengeka vyema kimazoezi uliyosindikizwa na muonekano nadhifu ambao ulimpagawisha kila msichana aliyemuona katika chuo hicho.
“There’s something I want to tell you,” (Kuna kitu nataka kukuambia Richard,) ilikuwa ni sauti ya msichana mmoja aliyejulikana kwa jina la Monalisa ambaye alimuita Richard chemba na kuzungumza naye.
“What’s that Monalisa?” (Kitu gani hicho Monalisa?) aliuliza Richard huku akimtazama Monalisa ambaye alikuwa akijing’atang’ata kucha za vidole vyake kwa wakati huo.
“But I feel like I’m going to make a mistake,” (Lakini nahisi kama nitakukosea,) alisema Monalisa huku akijishtukia, macho yake alikuwa ameyalegeza.
“No, tell me do not be afraid,” (Hapana niambie usiogope,) alisema Richard huku akiwa makini kumsikiliza. Kwa muonekano ambao aliuona kwa Monalisa akilini mwake alikwisha fahamu ni kitu gani ambacho msichana huyo alitaka kumueleza lakini hakutaka kuwa na papara ya kukurupukia mambo, alihitaji kumpa muda msichana huyo wa kujieleza ili asahili kile alichokuwa kikifikiria.
“Richard to say the truth I love you so much and I’m ready to do anything for you, please say yes do not let my kid,” (Richard kusema kweli mimi nakupenda sana na nipo tayari kufanya lolote kwa ajili yako, tafadhali sema ndiyo usinikatalie ombi langu,) alisema Monalisa huku akianza kumsogelea Richard kwa lengo la kumbusu.
“No, don’t do that,” (Hapana usifanye hivyo,) alisema Richard huku akimzuia Monalisa, kitendo hicho kikamkwaza Monalisa, akahisi kukataliwa, alijisikia vibaya mno.
Monalisa hakuwa msichana wa kwanza na wa mwisho kumsumbua Richard, kila msichana alitamani kuwa naye kimapenzi na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kupokea usumbufu kila kukicha lakini hakukuwa na msichana aliyewahi kuipata nafasi hiyo kwa Richard.
Moyo wa Richard ulizama kimapenzi kwa msichana mmoja ambaye ndiye alikuwa ameishikilia nafasi hiyo ya kimapenzi na kuwazibia wasichana wengine wote waliyokuwa wakiitamani kuipata. Hakukuwa na mtu ambaye alitaka kuamini kuwa Evelyne msichana aliyeonekana kuwa na uzuri wa kawaida ndiye ambaye alifanikiwa kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Richard, wengi wao waliamini kuwa kwa muonekano wa kuvutia aliyokuwa nao Richard pamoja na kutokea katika familia ya kitajiri basi ni lazima angekuwa na msichana ambaye alitikisa chuo kizima kwa uzuri wake au aliyetokea katika familia ya kitajiri lakini haikuwa hivyo.
“Huyu kinyago ndiyo anatuzibia riziki yetu,” alisema Monalisa huku akiwaambia wasichana wenzake watatu walipokuwa hostel wameketi kitandani, wote walikuwa wakimtamani Richard.
“Nani ndiyo huyu Evelyne?” aliuliza mmoja wao.
“Ndiyo hivi ana uzuri gani yule msichana mpaka wa kutembea na Richard kama sio uchawi,” alisema Monalisa huku akiwa ameubetua mdomo wake.
“Atakuwa mwanga yule sio bure,” alisema msichana mwingine maneno yaliyowafanya wote wakacheka kwa sauti kubwa huku wakigongeana.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuibuka kwa chuki kati ya wasichana hao na Evelyne, walitokea kumchukia sana pale chuoni baada ya kugundua kuwa alikuwa akijihusisha na mahusiano ya kimapenzi na Richard, hilo lilizidi kumuumiza kila msichana ambaye aliwahi kumtamkia neno NAKUPENDA Richard au kuibuka kwa chembechembe zozote za kimapenzi kwa mvulana huyo aliyetokea kuipagawisha mioyo ya wasichana wengi pale chuoni.
Je, ni nini kitaendelea katika maisha ya wasichana hao?
Na nini kimemkuta Evelyne?
Vipi kuhusu Richard?
Mtunzi:Juma Hiza
0712988278
Hali ya hewa ilikuwa shwari katika jiji la Daresalaam. Ndani ya chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kilichokuwepo maeneo ya Posta mtaa wa Shaaban Robert, msichana mrembo aliyejulikana kwa jina la Evelyne alionekana akitoka darasani huku akiwa anakimbia, machozi yalikuwa yakimdondoka kwa wakati huo.
“Evelyne! Evelyne! Evelyne,” ilisikika sauti ya msichana mwingine ambaye alikuwa akimfuata nyuma Evelyne baada ya kutoka darasani.
Evelyne aliongoza moja kwa moja mpaka kwenye kimbweta, alipofika hapo aliketi na kuanza kulia huku akiwa amejiinamia.
“Evelyne kuna nini mbona sikuelewi?” aliuliza msichana huyo aliyekuwa akimfuata nyuma Evelyne, alionekana kutoelewa chochote kilichokuwa kikiendelea kwa wakati huo.
“Hapana Happy siwezi kuendelea kuwa eneo hili acha niondoke zangu,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio cha kwikwi.
“Unaondoka unaenda wapi sasa na wakati darasani kuna kipindi?” aliuliza Happy huku akimtazama Evelyne ambaye aliendelea kulia muda wote huo.
“Narudi zangu nyumbani,” alijibu Evelyne.
“Unajua sikuelewi Evelyne,” alisema Happy lakini kabla ya Evelyne kumjibu lolote aliinuka na kuondoka eneo hilo la chuo, Happy alibaki akimtazama Evelyne huku asijue ni nini kilichokuwa kikiendelea.
Evelyne na Happy walikuwa ni marafiki wakubwa sana katika chuo hicho, walikuwa wakisaidiana mambo mengi sana, walishiriki kusaidiana katika masomo na hata katika mipango yao ya kimaisha pia walishirikishana. Happy alikuwa akimfahamu vyema rafiki yake huyo tangu walipoanza kusoma katika chuo hicho mpaka kufikia mwaka wao wa mwisho wa Degree ambao ndiyo walikuwa wameubakiza. Walikuwa wakisomea Uhasibu.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, Happy alikifahamu na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Happy, Evelyne naye alikifahamu, kwa kifupi walikuwa ni marafiki waliyoshibana. Walikuwa wakiishi pamoja katika chumba kimoja walichokuwa wamepanga maeneo ya Kigamboni.
Wakati Happy akiwa bado amesimama eneo lile ghafla! aliisikia sauti ya kiume ikimuita nyuma yake, haraka aligeuka na kukutana na mtu aliyekuwa akimuita. Alikuwa ni Richard.
“Niambie Shem.”
“Poa tu! vipi mbona Evelyne ametoka darasani kuna nini?”
“Sijui.”
“Yuko wapi?”
“Ameondoka, ameniambia anarudi nyumbani hawezi kuendelea kuwa eneo hili.”
“Mbona unanichanganya?”
“Richard kwani kuna kitu gani kimetokea kati yenu?”
“Hakuna kitu.”
“Mbona sasa Evelyne amebadilika ghafla! baada ya kukuona.”
“Mimi mwenyewe sielewi chochote.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo Happy inamaana huniamini?”
“Nakuamini sana,” alijibu Happy.
Richard alikuwa ni mvulana aliyekuwa akitokea katika familia ya kitajiri sana, alikuwa ni mtanashati, mwenye mwili uliyojengeka vyema kimazoezi uliyosindikizwa na muonekano nadhifu ambao ulimpagawisha kila msichana aliyemuona katika chuo hicho.
“There’s something I want to tell you,” (Kuna kitu nataka kukuambia Richard,) ilikuwa ni sauti ya msichana mmoja aliyejulikana kwa jina la Monalisa ambaye alimuita Richard chemba na kuzungumza naye.
“What’s that Monalisa?” (Kitu gani hicho Monalisa?) aliuliza Richard huku akimtazama Monalisa ambaye alikuwa akijing’atang’ata kucha za vidole vyake kwa wakati huo.
“But I feel like I’m going to make a mistake,” (Lakini nahisi kama nitakukosea,) alisema Monalisa huku akijishtukia, macho yake alikuwa ameyalegeza.
“No, tell me do not be afraid,” (Hapana niambie usiogope,) alisema Richard huku akiwa makini kumsikiliza. Kwa muonekano ambao aliuona kwa Monalisa akilini mwake alikwisha fahamu ni kitu gani ambacho msichana huyo alitaka kumueleza lakini hakutaka kuwa na papara ya kukurupukia mambo, alihitaji kumpa muda msichana huyo wa kujieleza ili asahili kile alichokuwa kikifikiria.
“Richard to say the truth I love you so much and I’m ready to do anything for you, please say yes do not let my kid,” (Richard kusema kweli mimi nakupenda sana na nipo tayari kufanya lolote kwa ajili yako, tafadhali sema ndiyo usinikatalie ombi langu,) alisema Monalisa huku akianza kumsogelea Richard kwa lengo la kumbusu.
“No, don’t do that,” (Hapana usifanye hivyo,) alisema Richard huku akimzuia Monalisa, kitendo hicho kikamkwaza Monalisa, akahisi kukataliwa, alijisikia vibaya mno.
Monalisa hakuwa msichana wa kwanza na wa mwisho kumsumbua Richard, kila msichana alitamani kuwa naye kimapenzi na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kupokea usumbufu kila kukicha lakini hakukuwa na msichana aliyewahi kuipata nafasi hiyo kwa Richard.
Moyo wa Richard ulizama kimapenzi kwa msichana mmoja ambaye ndiye alikuwa ameishikilia nafasi hiyo ya kimapenzi na kuwazibia wasichana wengine wote waliyokuwa wakiitamani kuipata. Hakukuwa na mtu ambaye alitaka kuamini kuwa Evelyne msichana aliyeonekana kuwa na uzuri wa kawaida ndiye ambaye alifanikiwa kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Richard, wengi wao waliamini kuwa kwa muonekano wa kuvutia aliyokuwa nao Richard pamoja na kutokea katika familia ya kitajiri basi ni lazima angekuwa na msichana ambaye alitikisa chuo kizima kwa uzuri wake au aliyetokea katika familia ya kitajiri lakini haikuwa hivyo.
“Huyu kinyago ndiyo anatuzibia riziki yetu,” alisema Monalisa huku akiwaambia wasichana wenzake watatu walipokuwa hostel wameketi kitandani, wote walikuwa wakimtamani Richard.
“Nani ndiyo huyu Evelyne?” aliuliza mmoja wao.
“Ndiyo hivi ana uzuri gani yule msichana mpaka wa kutembea na Richard kama sio uchawi,” alisema Monalisa huku akiwa ameubetua mdomo wake.
“Atakuwa mwanga yule sio bure,” alisema msichana mwingine maneno yaliyowafanya wote wakacheka kwa sauti kubwa huku wakigongeana.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuibuka kwa chuki kati ya wasichana hao na Evelyne, walitokea kumchukia sana pale chuoni baada ya kugundua kuwa alikuwa akijihusisha na mahusiano ya kimapenzi na Richard, hilo lilizidi kumuumiza kila msichana ambaye aliwahi kumtamkia neno NAKUPENDA Richard au kuibuka kwa chembechembe zozote za kimapenzi kwa mvulana huyo aliyetokea kuipagawisha mioyo ya wasichana wengi pale chuoni.
Je, ni nini kitaendelea katika maisha ya wasichana hao?
Na nini kimemkuta Evelyne?
Vipi kuhusu Richard?