Pole, naona dalili za manyoya. Mchunie mwezi mzima, akipiga wala usipokee uone kama atakuhangaikia.
Ukiona hahangaiki jua wewe si wa moyoni, ni wa mfukoni tu. Ukiona anahangaika jua huyo aliyenaye huko Mwanza ni mshika mapembe tu, anakusaidia kulea ila wewe ndio muwojaji.
Cha msingi, je mko wangapi?
Lady doctor,
Umetoa ushauri mzuri sana, lkn wasiswasi wangu ni kuwa uliyempa huo ushauri anaonekana hazimtoshi. With all vitimbi aliyoeleza kwenye thread yake bado anaomba ushauri badala ya kuamua kuachana na huyo binti msanii? Nachukia watu wenye akili nzito namna hii! Ni mzigo kwa jamii.
mkuu wala usipoteze pesa yako kwenda mwanza coz unaweza patwa na mshituko huko ukafa kwa presha ukawapa tabu wazazi wako kukutafuta, cha msingi usimpigie simu wala kumtumia sms kwa japo wiki moja.kama ukiona naye amekausha basi piga chini na usirudi nyuma. kama atakutafuta basi endelea nae ila mpe onyo kali kuhusu hizo tabia zake na umuweke kwenye probation.
dah kweli kaka nilikua nawaza kwenda mwanza coz yuko huru kabisa kanikaribisha ila ndo hivo vitabia tu kaka.
Matatizo ya kuanza mapenzi ukubwani Hayo.
Ukimwambia I LOVE YOU anasema Poa, nimechekaje.
Tatizo wewe bahili
habari za siku, habari za coastal region.