Nipo Mwanza, haijanivutia kabisa

Jambo Tz

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
670
Reaction score
203
Habari zenu wadau,

Ni siku yangu ya pili hapa Rock City (Mwanza) kama inavyo julikana na wengi.

Kwa wale wanaotamani kufika Mwanza ambalo lish tunukiwa sifa ya jiji miaka kadhaa sasa lakini jina hilo haliendani na sifa ambayo linapewa.

Saa yangu inaonyesha ni saa 1:23 usiku ndani ya Dar lux tunaingia Mwanza, moyo unashtuka baada ya kuambiwa Nyegezi stand ndo mwisho wa safari, wakimaanisha tushafika Mwanza.

Ni giza kila sehemu stand ya Nyegezi kama dampo jamani hakuna taa barabara imejaa mashimo, taa za barabarani haziwaki.

Tunatoka Nyegezi tunaelekea Nata ambako ndio mwisho wa gari jamani city centre mashimo, viroba vya taka vimetupwa katikati ya barabara.

Hiyo ndio Mwanza unayo isikia, pana pambazuka asubuhi najiandaa kwa ajili ya mishe ilo nifikisha uwiii! Daladala zimechoka, na zinajaza balaa, vituo havieleweki kama vile hakuna mkandarasi wa jiji.

Je, mkuu wa mkoa hayupo au hajifunzi kutoka kwa Makonda?
 
Acha kudanganya watu hapa wewe.kuna daladala mbovu hapa mjini toka lini?watu mna vimaneno vya kijinga jinga kweli sijui utapata nini kuwadanganya watu.mji huu una hiace kama mchanga na zote kwa %90 ni gari mpya.mashimo barabarani umeyaona wapi?kuna uchakavu wa barabara kidogo mwanzoni mwa pamba road na Lumumba road kutokana na mapolomoko ya maji ya mvua maana kuna mwinuko kidogo basi,na hazina hata point 4 za kilometer.sasa hayo mashimo ya mpaka wewe kuleta maneno hapa umeyaona wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…