Katika lugha ya kiswahili,kuna aina ya maneno inaitwa NOMINO.....nomino imegawanyika katika makundi au aina kuu nne....ya kwanza ni nomino za PEKEE, ya pili ni nomino za KAWAIDA, ya tatu ni nomino za jamii na ya nne ni nomino dhahania....sasa neno Mungu linaangukia katika aina ya kwanza yaani nomino za PEKEE na maneno yote ambayo ni nomino za pekee lazima yaanze na herufi kubwa hata pale yanapoanza katikati ya sentensi.....so huwezi kuandika nomino hii kwa kuanza na herufi ndogo yaani mungu' badala yake lazima uandike kwa kuanza na herufi kubwa....Mungu.