NIPASHE kamwe msiwajali watu kama akina Zarina Madabida. Kuweni wakweli siku zote, andikeni ukweli siku zote kwa sababu KWELI NDIYO INAYOMWEKA MTU HURU!! Huyo mama amezungukwa na maovu kibao, anateseka kwelikweli na wao kama viongozi tena wa chama tawala wamezoea kuishi kwa deal za ujanjaujanja kwa gharama za wanyonge!!
Anapotokea mtu au chombo cha habari kinagusa deal zao, matokeo yake ni haya wanawaka ile mbaya na kukuona wewe unayekosoa mwenendo na matendo yao ni adui. Katika hili jambo zuri ni moja kuwa hawana ubavu wa kupeleka malalamiko yao katika chombo huru cha kisheria ili wapate haki yao ya kuonewa/kusemwa/kuandikwa kwa uongo. Ndiyo maana hana hata habari kuwa kuna eneo la kupeleleka malalamiko yako dhidi ya chombo chochote cha habari kwa kuandika kwa kumchafua mtu au taasisi yoyote i.e mahakamani au (MCT?) nk
Lakini kina Madabida wameona Bunge ni forum sahihi ya kusafishia uchafu wao,jambo ambalo sio sahihi kwa sbb ndo tu wamewasha moto. Ona sasa, mimi hata nilikuwa sijui kuwa TPI ya kina Madabida wanahusika na uuzaji wa sukari fake achilia mbali ARV ambalo kila mtu na karibu kila m-tz anajua!!
Mtu anayeongea kwa kujaribu kuficha ukweli utamjua tu. Zarina wakati anachangia bungeni huku akijaribu kujisafisha kwa kulituhumu gazeti la NIPASHE wakati huohuo akiikataa bajeti ya serikali yake chini ya CCM chama chake!!. Hapo hakuwa smart, alijichanganya na kuwachanganya hata wenzake,wana CCM kwa sababu ni wazi hawakumwelewa!!
NIPASHE keep on going........FORGET MADABIDAS.......THEY WILL NEVER STOP YOU...THEY WILL NEVER STOP THE TRUTH UNLESS THEY FACE AND ACCEPT IT....BECAUSE THE TRUTH WILL SET ANYONE FREE!!.