Naikuru
Senior Member
- Jul 29, 2015
- 167
- 226
Wakuu habari za wakati huu.
Nimelazimika kuingia humu kuomba ushauri kwa ajili ya kapata namna kumpa mke wangu amani ya moyo.
Nina mshukuru Mungu tumejenga nyumba kubwa nzuri na kufanikiwa kupaua kwa mabati ya GSM yale yasiyo ya rangi, huwa ni alluminium tupu.
Majirani zetu nao wamejenga nyumba zao nzuri kwa mabati ya rangi tofauti tofauti ili mradi tu kila mtu nyumba yake iwe kivutio kwa kila apitaye jirani macho yake yaelekee kwenye mapaa yao Jambo ambalo Mimi sikuzingatia.
Kilichonileta humu ni mke wangu hana amani kabisa na hili paa letu, anatamani lipate rangi lifanane na majirani wakati huo uwezo wa kusema ninunue bati 192 ya rangi ili tubadilshe kwa kweli sina na wala mpango hapo. Nimeona maeneo fulani watu wanapaka paa rangi ila baada ya muda rangi zinababuka na paa kuwa mbaya zaidi na bora ingebaki hivyo hivyo. Sasa mke wangu hana amani anataka tupake rangi paa letu.
Ombi langu wanajamvi nipake rangi gani ambayo itaweza kuendana na mabati ya GSM na ambayo hayata babuka?
Nimelazimika kuingia humu kuomba ushauri kwa ajili ya kapata namna kumpa mke wangu amani ya moyo.
Nina mshukuru Mungu tumejenga nyumba kubwa nzuri na kufanikiwa kupaua kwa mabati ya GSM yale yasiyo ya rangi, huwa ni alluminium tupu.
Majirani zetu nao wamejenga nyumba zao nzuri kwa mabati ya rangi tofauti tofauti ili mradi tu kila mtu nyumba yake iwe kivutio kwa kila apitaye jirani macho yake yaelekee kwenye mapaa yao Jambo ambalo Mimi sikuzingatia.
Kilichonileta humu ni mke wangu hana amani kabisa na hili paa letu, anatamani lipate rangi lifanane na majirani wakati huo uwezo wa kusema ninunue bati 192 ya rangi ili tubadilshe kwa kweli sina na wala mpango hapo. Nimeona maeneo fulani watu wanapaka paa rangi ila baada ya muda rangi zinababuka na paa kuwa mbaya zaidi na bora ingebaki hivyo hivyo. Sasa mke wangu hana amani anataka tupake rangi paa letu.
Ombi langu wanajamvi nipake rangi gani ambayo itaweza kuendana na mabati ya GSM na ambayo hayata babuka?