Mngurimi
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 819
- 789
Habari za wakati huu wadau wa JF.
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Mara nyingi katika vyanzo mbalimbali vya habari na tambo za mashabiki wa mpira nchini, kumekuwa na majivuno baina ya mashabiki wa timu mbili hapa nchini (Yanga & Simba) ambao hujitapa huku kila shabiki akidai kuwa timu yake ndiyo ina mashabiki wengi kuliko timu nyingine.
Simba na Yanga ni klabu ambazo zinaonekana kuongoza kwa kuwa na idadi kubwa sana ya mashabiki lakini hadi leo sijui ni klabu ipi ndiyo inao mashabiki wengi. Kingine, bado sijui takwimu zinazothibitisha ukweli wa kuwa klabu fulani ina mashabiki wengi huwa zinapatikana wapi.
Kwa mantiki hiyo, niombe sasa wadau, serikali na vilabu viungane na wazo langu ili sensa ya watu na makazi ijayo, wachukue takwimu nyumba hadi nyumba ili ubishi usiwepo.
Naomba kuwasilisha.
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Mara nyingi katika vyanzo mbalimbali vya habari na tambo za mashabiki wa mpira nchini, kumekuwa na majivuno baina ya mashabiki wa timu mbili hapa nchini (Yanga & Simba) ambao hujitapa huku kila shabiki akidai kuwa timu yake ndiyo ina mashabiki wengi kuliko timu nyingine.
Simba na Yanga ni klabu ambazo zinaonekana kuongoza kwa kuwa na idadi kubwa sana ya mashabiki lakini hadi leo sijui ni klabu ipi ndiyo inao mashabiki wengi. Kingine, bado sijui takwimu zinazothibitisha ukweli wa kuwa klabu fulani ina mashabiki wengi huwa zinapatikana wapi.
Kwa mantiki hiyo, niombe sasa wadau, serikali na vilabu viungane na wazo langu ili sensa ya watu na makazi ijayo, wachukue takwimu nyumba hadi nyumba ili ubishi usiwepo.
Naomba kuwasilisha.