Mulama
JF-Expert Member
- Apr 16, 2011
- 3,018
- 1,790
Ndugu zangu naombeni msaada kwenye kisa hiki cha kweli . nina mke tuliyefunga ndoa yapata miaka 11 iliyopita, mke wangu tulikutana kazini kwenye kiwanda cha kutengeneza biscuits ambapo yeye alikuwa teller mimi ni mwendesha mashine.
Baada ya kuoana nilimwendeleza kimasomo kwakuwa yeye alikuwa wa form IV nami ni darasa la saba, kwakuwa alifanya vizuri katika kozi zake alifanikiwa kupata kazi kwenye shirika moja la kimataifa kama administrative secretary.
Sisi huku kiwanda kilifungwa kutokana na biscuits kukosa masoko kutokana na ushindani uliopo hivyo nikalazimika kukaa nyumbani huku nikijitahidi kutafuta vibarua vya hapa na pale.
Issue ni kwamba mke wangu sasa amekuwa mbogo hataki kusaidia kitu chochote hapa nyumbani na ikitokea akatoa hela basi masimango yanatisha, tutaitwa majina ya kila aina mara poyoyo, mara Mario nk.
Wakati tunaoana kila mmoja alikuwa na mtoto na wote tulikuwa tunawalea kwa mapenzi bila ubaguzi, cha kushangaza yeye mtoto wake kampeleka international school wa kwangu amemwacha aendelee na hizi za kayumba!
Kinachonipa taabu sana ni kurudi usiku wa manane wakati mwingine akiwa amelewa nikimuuliza anasema walikuwa na kazi nyingi na mikutano inayoambatana na vinywaji, pia ana safari nyingi za kikazi na akifika huko huwa hataki nimpigie simu eti namsumbua!
Sasa je huyu bado anastahili kuwa mke wangu? Si kawa wa mataifa sasa niachane naye nikaoe mwingine?
Vikao vya wazee vimeshindwa kutoa ufumbuzi wanamuogopa au sijui ni kwamba anawakatia mkwanja mrefu?!
Nawasilisha
Baada ya kuoana nilimwendeleza kimasomo kwakuwa yeye alikuwa wa form IV nami ni darasa la saba, kwakuwa alifanya vizuri katika kozi zake alifanikiwa kupata kazi kwenye shirika moja la kimataifa kama administrative secretary.
Sisi huku kiwanda kilifungwa kutokana na biscuits kukosa masoko kutokana na ushindani uliopo hivyo nikalazimika kukaa nyumbani huku nikijitahidi kutafuta vibarua vya hapa na pale.
Issue ni kwamba mke wangu sasa amekuwa mbogo hataki kusaidia kitu chochote hapa nyumbani na ikitokea akatoa hela basi masimango yanatisha, tutaitwa majina ya kila aina mara poyoyo, mara Mario nk.
Wakati tunaoana kila mmoja alikuwa na mtoto na wote tulikuwa tunawalea kwa mapenzi bila ubaguzi, cha kushangaza yeye mtoto wake kampeleka international school wa kwangu amemwacha aendelee na hizi za kayumba!
Kinachonipa taabu sana ni kurudi usiku wa manane wakati mwingine akiwa amelewa nikimuuliza anasema walikuwa na kazi nyingi na mikutano inayoambatana na vinywaji, pia ana safari nyingi za kikazi na akifika huko huwa hataki nimpigie simu eti namsumbua!
Sasa je huyu bado anastahili kuwa mke wangu? Si kawa wa mataifa sasa niachane naye nikaoe mwingine?
Vikao vya wazee vimeshindwa kutoa ufumbuzi wanamuogopa au sijui ni kwamba anawakatia mkwanja mrefu?!
Nawasilisha