Nini Tofauti ya TB Joshua na Mwingira??

Nini Tofauti ya TB Joshua na Mwingira??

Inawezekana ikawa ni miujiza ya Mungu kwa vile anayetenda ni Mungu sio wao. Neno la Mungu linasema siku ya mwisho wengi watanililia wakisema nilikuwa nahubiri sana au nilikuwa naponya wagonjwa kwa jina lako au kazi yeyote ile lakini Bwana atasema siwajui ninyi!! Kikubwa ni kuishi maisha ya utauwa. Mungu anaweza akakutumia ufanye kazi yake lakini matendo yako yakienda kinyume na mapenzi yake siku ya mwisho ni hukumu tu! Kama hao uliowataja hawatendi mapenzi ya Mungu Mungu mwenyewe anajua. Mwachie yeye aamue. We shika neno na ulitende period. Usimkashifu mtumishi wake maana Mungu hapendi. Kasome kitabu cha Hesabu 12: 1-15 utaona jinsi Mungu alivyomuadhibu Miriam kwa ajili ya kumsema mtumishi wake Musa.
Wanajamvi,

Mimi ni muumini wa dini ya kikristo, dhehebu langu nitataja nikihitajika kufanya hivyo.

Naomba ufafanuzi kwa wale wenye uelewa zaidi kuhusu hawa viongozi wa dini wanaoibuka siku hizi hapa nyumbani mpaka kwingineko ulimwenguni!

Hapa nyumbani tunao wengi, kuwataja wachache ni Kakobe, Mwingira, Mama Rwakatare na Mzee wa Upako (Lusekelo)

Naomba tofauti ya mitume/watumishi hawa; Mwingira wa Tanzania na TB Joshua wa Nigeria.

Kwa uelewa wangu, hawa wote na wengineo wanatumia neno la Mungu kujitajirisha! Ni nini kinamfanya TB Joshua awe maarufu zaidi?

Miujiza wanayoitenda ni kweli ina mkono wa Mungu au ni mapepo?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Utofauti ni kuwa Mwingira yupo Tz na TB Nigeria ila wote ni matapeli wanaocheza na saikolojia ya watu waliokosa imani na Mungu.
 
Kwa uelewa wangu, hawa wote na wengineo wanatumia neno la Mungu kujitajirisha! Ni nini kinamfanya TB Joshua awe maarufu zaidi?

Hakuna mwandamu atakayeweza kumuelewa au kulielewa NENO la KRISTO kwa kutumia uelewa wake...

Nakueleza wazi kabisa upate kusoma, wewe mleta mada si MKRISTO hata kama unaenda kanisani na kusoma BIBLIA...
 
Mwacheni atukane na kuvumisha uongo apendavyo maana huyu ni mteja mojawapo wa jehanamu ya moto,kazana ndugu ujira wako unakusubiri.".......heri ninyi watapowanenea kila neno baya kwa ajili yangu thawabu yenu ni kubwa Mbinguni."
 
Nenda kasome kwa makini Biblia Takatifu, inayo majibu yooote juu ya haya tunayoyashuhudia kasha simama ulipo na kutenda mapenzi ya Mungu ili kuutafuta uzima wa Milele.
 
Wanajamvi,

Mimi ni muumini wa dini ya kikristo, dhehebu langu nitataja nikihitajika kufanya hivyo.

Naomba ufafanuzi kwa wale wenye uelewa zaidi kuhusu hawa viongozi wa dini wanaoibuka siku hizi hapa nyumbani mpaka kwingineko ulimwenguni!

Hapa nyumbani tunao wengi, kuwataja wachache ni Kakobe, Mwingira, Mama Rwakatare na Mzee wa Upako (Lusekelo)

Naomba tofauti ya mitume/watumishi hawa; Mwingira wa Tanzania na TB Joshua wa Nigeria.

Kwa uelewa wangu, hawa wote na wengineo wanatumia neno la Mungu kujitajirisha! Ni nini kinamfanya TB Joshua awe maarufu zaidi?

Miujiza wanayoitenda ni kweli ina mkono wa Mungu au ni mapepo?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Tofauti ipo kubwa sana, mwingira kila anapofungua mlango wa kanisa lake lazima kila muumini atoe sadaka hata kama ni masikini hana kitu, lakini Tb joshua yeye ndie anaye toa misaada kwa wenye uhitaji kama ni fedha, chakula au hata ada za shule kwa wenye mahitaji.
 
FYI, hukuwa na muda wa kusoma swali ukalielewa! Umelijibu kwa jazba pasipo kutaka kulifikiri kwa ndani zaidi!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

hivi ndivyo swali lilivyo Quote: "Kwa uelewa wangu, hawa wote na wengineo wanatumia neno la Mungu kujitajirisha! Ni nini kinamfanya TB Joshua awe maarufu zaidi?
Miujiza wanayoitenda ni kweli ina mkono wa Mungu au ni mapepo?"

sasa hapo nimekurupuka vipi? ni sawa na mtu amuulize muislamu:
"kwa uelewa wangu mimi waislamu wote ni magaidi" halafu amalizie "je uislamu unatoka mbinguni au motoni?" unadhani muislamu atajibuje?
 
Tofauti ipo kubwa sana, mwingira kila anapofungua mlango wa kanisa lake lazima kila muumini atoe sadaka hata kama ni masikini hana kitu, lakini Tb joshua yeye ndie anaye toa misaada kwa wenye uhitaji kama ni fedha, chakula au hata ada za shule kwa wenye mahitaji.

1. "maskini asiye na kitu" anatoaje?
2. huyo TB joshua yeye hela zake anazotoa misaada zinatoka wapi mbinguni? misaada anayotoa ndio ushahidi kuwa anakusanya sadaka kubwa kuliko mwingira.
 
Wanajamvi,

Mimi ni muumini wa dini ya kikristo, dhehebu langu nitataja nikihitajika
kufanya hivyo.

Naomba ufafanuzi kwa wale wenye uelewa zaidi kuhusu hawa viongozi wa
dini wanaoibuka siku hizi hapa nyumbani mpaka kwingineko ulimwenguni!

Hapa nyumbani tunao wengi, kuwataja wachache ni Kakobe, Mwingira, Mama
Rwakatare na Mzee wa Upako (Lusekelo)

Naomba tofauti ya mitume/watumishi hawa; Mwingira wa Tanzania na TB
Joshua wa Nigeria.

Kwa uelewa wangu, hawa wote na wengineo wanatumia neno la Mungu
kujitajirisha! Ni nini kinamfanya TB Joshua awe maarufu zaidi?

Miujiza wanayoitenda ni kweli ina mkono wa Mungu au ni mapepo?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

all are false prophetes
 
Kiukweli ndugu hakutaka kujua tofauti yao sababu analo jibu ndani yake kwamba wanataka kujitajirisha, So kwa ushauri si vema sana kuwajadili hawa wapakwa mafuta, na kama wewe si mtu wa rohoni huwezi kutambua kama ni Mungu kweli au usanii, wakati mwingine unaweza kujitafutia laana kwa ulimi wako tu, angalia mada nyingine, hawa watu waache wao na Mungu wao watajuana naye, huna mamlaka ya kuwanyooshea vidole! Be carefully, maana utakula matunda ya ulimi wako.
 
"we linda sana moyo wako kuliko yote uyalindayo!" hayo mengine ni urembo tu! ikiwa unakaa ndani ya Yesu (yaani roho wa Mungu) na Yesu yumo ndani yako, huko nje unatafuta nini? nje kuna wachawi, wanyang'anyi, wazinzi, manabii wa uongo wanaopora masikini kidogo walichonacho, nk. Enendeni kwa roho nanyi hamtazitimiza tamaa za mwili!
 
Ukiwasikiliza sana Wahubiri/wachungaji halafu na skendo zao ndo unapoteza imani kabisa na kuona heri usimame na imani yako mwenyewe bila kuchafuliwa

jiulize wewe uonae skendo za wenzako hizo za kwako ndio imani iliyosafi? pili hizo skendo unazodai una uhakika nazo au ni huo ushabiki wako kwa mambo ya kusikia tena yasiyo na msingi?jitafakari kwani yawezekana unafanya kazi ya shetani bila kujitambua...
 
Hakuna mwandamu atakayeweza kumuelewa au kulielewa NENO la KRISTO kwa kutumia uelewa wake...

Nakueleza wazi kabisa upate kusoma, wewe mleta mada si MKRISTO hata kama unaenda kanisani na kusoma BIBLIA...

Exactly huyu si mkristo sijui alitaka baba yake ahubiri ndio aamini kuwa hawa watu ni watumishi wa Mungu na Mungu ndiye atendaye miujiza?dah binadamu sisi kwakweli Mungu azidi kuturehemu tu
 
Siku izi bila muujiza imekula kwako we uliza tu hata washabiki wao wanafata nini wkt kuna wachungaji kibaaaao




Sent from Nokla using Jf app
 
Mwacheni atukane na kuvumisha uongo apendavyo maana huyu ni mteja mojawapo wa jehanamu ya moto,kazana ndugu ujira wako unakusubiri.".......heri ninyi watapowanenea kila neno baya kwa ajili yangu thawabu yenu ni kubwa Mbinguni."

Mzee wa kweli kuweka huru upo? Hivi kwa nini siku izi bila miujiza neno haliendi?




Sent from Nokla using Jf app
 
Inawezekana ikawa ni miujiza ya Mungu kwa vile anayetenda ni Mungu sio wao. Neno la Mungu linasema siku ya mwisho wengi watanililia wakisema nilikuwa nahubiri sana au nilikuwa naponya wagonjwa kwa jina lako au kazi yeyote ile lakini Bwana atasema siwajui ninyi!! Kikubwa ni kuishi maisha ya utauwa. Mungu anaweza akakutumia ufanye kazi yake lakini matendo yako yakienda kinyume na mapenzi yake siku ya mwisho ni hukumu tu! Kama hao uliowataja hawatendi mapenzi ya Mungu Mungu mwenyewe anajua. Mwachie yeye aamue. We shika neno na ulitende period. Usimkashifu mtumishi wake maana Mungu hapendi. Kasome kitabu cha Hesabu 12: 1-15 utaona jinsi Mungu alivyomuadhibu Miriam kwa ajili ya kumsema mtumishi wake Musa.

utakua. na uhakika gani kama ni watumishi wa Mungu? shida ndo hiyo tu..maana hata walimu wa uongo wameandikwa tumeambiwa tutumie akili kuwatambua..
 
Hakuna mwandamu atakayeweza kumuelewa au kulielewa NENO la KRISTO kwa kutumia uelewa wake...

Nakueleza wazi kabisa upate kusoma, wewe mleta mada si MKRISTO hata kama unaenda kanisani na kusoma BIBLIA...

Ukiona makelele mengi namna hii na vilio ujue ule ufalme wa giza umetikiswa.Wanajaribu kujiinua
 
Mzee wa kweli kuweka huru upo? Hivi kwa nini siku izi bila miujiza neno haliendi?




Sent from Nokla using Jf app

Neno katika Biblia linakubaliana na Miujiza.Soma Marko 16:17.
Na hata Yesu mwenyewe aliwaambia wafuasi wake kuwa watatenda miujiza mikubwa zaidi aliyofanya.Japo sikatai kuna ule upande wa giza wanajaribu kuiga watakatifu na hilo lipo wazi katika Bible.Ukiwa Mkristo wa kweli hupaswi kukosoa au kuhukumu.Mwache Roho Mtakatifu akuongoze katika kuujua ukweli
 
Back
Top Bottom